Songwe: Mfamasia akutwa amefariki, mwili wadaiwa kuokotwa ukiwa na majeraha

Songwe: Mfamasia akutwa amefariki, mwili wadaiwa kuokotwa ukiwa na majeraha

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Agostino Senga amesema uchunguzi wao kuhusu kifo cha aliyekuwa Mfamasia wa Kituo cha Afya cha Isansa, Wilayani Mbozi, Mkoani Songwe aliyetambulika kwa jina la Daudi Kwibuja (30) hakijatokana na ajari kama ilivyodhaniwa kutokana na mwili kuokotwa kando ya barabara Kuu itokayo Mbeya kwenda Tunduma katika eneo la Mlowo.

Amesema kuwa mwili wa mtumishi huyo wa idara ya afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi ulikutwa ukiwa na majereha mwilini mwake ambayo amedai kuwa katika uchunguzi wao majeraha hayo hayana viashiria vya ajali.

Akitoa taarifa ya kifo hicho, Kamanda, Senga, amesema kuwa wanaendelea na uchunguzi zaidi kubaini sababu halisi ya kifo hicho na kuchukua hatua kulingana ripoti ya uchunguzi wa kifo hicho kilichodaiwa kutokea usiku wa Julai 3, 2024.

“Uchunguzi unaendelea ili kuweza kubaini ni ajali kweli au mauaji, kwa hiyo tunaendelea kuchunguza na tutakapopata ukweli kupitia matabibu tutauhabarisha umma chanzo cha kifo cha ndugu yetu huyu (marehemu) kimetokana na nini ”, amesema Kamanda Senga.

Chanzo: Matukio Daima Media
 
Laba amekula "vitu" vya watu
Kuna sababu nyingi. Inawezekana ni vibaka tu walimwotea, alikuwa na bifu na mtu au watu nk. THADHARI: Msitu wa Kongowe ni sehemu ya kutupa maiti sasa hivi. Wanapekekwa kwa magari na polisi wakitaarifiwa wanawaambia wanakijiji ''zikeni''. Maiti nyingi ni za vijana. Angalia HAKI TV uone mahojiano.
 
Duuh pole saana kwa wafiwa kaondoka akiwa bado kijana mdogo mno
 
Kuna sababu nyingi. Inawezekana ni vibaka tu walimwotea, alikuwa na bifu na mtu au watu nk. THADHARI: Msitu wa Kongowe ni sehemu ya kutupa maiti sasa hivi. Wanapekekwa kwa magari na polisi wakitaarifiwa wanawaambia wanakijiji ''zikeni''. Maiti nyingi ni za vijana. Angalia HAKI TV uone mahojiano.
Weka link ya Haki tv tuone
 
Kuna sababu nyingi. Inawezekana ni vibaka tu walimwotea, alikuwa na bifu na mtu au watu nk. THADHARI: Msitu wa Kongowe ni sehemu ya kutupa maiti sasa hivi. Wanapekekwa kwa magari na polisi wakitaarifiwa wanawaambia wanakijiji ''zikeni''. Maiti nyingi ni za vijana. Angalia HAKI TV uone mahojiano.
Kongowe ya kibaha au ile km unaelekea mkuranga
 
Back
Top Bottom