Pre GE2025 Songwe: Shule na walimu wapewa zawadi kwa kuinua ufaulu

Pre GE2025 Songwe: Shule na walimu wapewa zawadi kwa kuinua ufaulu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Wakati Serikali ikiendelea kuboresha miundo mbinu ya sekta ya elimu, uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songwe iliyopo mkoani Songwe, katika kuunga mkono jitihada hizo umetoa zawadi mbalimbali zikiwemo pikipiki, komputa mpakato (laptops), mashine za kunakili (photo copy mashine), kwa shule na walimu ambao wamesababisha ufaulu kupanda kwa madarasa ya mitihani ya taifa kwa shule za msingi na sekondari kwa mwaka wa masomo 2024.

Mkurugenzi wa halmashauri hiyo CPA Cecilia Kavishe, amesema wamekuja na ubunifu huo ukiwa na lengo la kuthamini mchango wa walimu pamoja na kuwapa motisha ya kufanya vizuri zaidi hasa katika sekta ya elimu ambapo halmashauri hiyo kwa kipindi cha miaka minne hali ya elimu imezidi kupanda huku walimu waliopata zawadi hizo wakipongeza ubunifu huo.

 
Benevolent teachers at low wages.Teachers do you know the life experience after retiring?Anyway,congrats for the Songwe's achievements.
 
Back
Top Bottom