Special Thread: Je, utamkumbuka Freeman Mbowe kwa mambo gani katika utumishi wa CHADEMA?

Special Thread: Je, utamkumbuka Freeman Mbowe kwa mambo gani katika utumishi wa CHADEMA?

Joined
Nov 19, 2024
Posts
94
Reaction score
307
mbowe.jpg

Freeman Aikael Mbowe​

Freeman Aikael Mbowe, kiongozi mwenye msimamo thabiti na maono makubwa, alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa mara ya kwanza mwaka 2004. Kwa takriban miaka 21, Mbowe aliongoza chama hicho kwa ujasiri na ustadi mkubwa, akifanya kazi bila kuchoka ili kuboresha siasa za upinzani na kuimarisha demokrasia nchini Tanzania. Uongozi wake ulijikita katika kujenga chama chenye mshikamano wa kitaifa huku akilenga kupigania haki, usawa, na uwajibikaji wa viongozi wa umma.

Hata hivyo, Januari 22, 2025, Freeman Mbowe alikabidhi kijiti kwa Tundu Lissu baada ya kushindwa kutetea nafasi yake.

Je, kama Mtanzania, ni mambo gani utayakumbuka kutoka kwa Freeman (FAM) katika utumishi wa CHADEMA kwa nafasi ya Mwenyekiti?

Pia soma
- Breaking News: - Pre GE2025 - Freeman Mbowe akubali kushindwa, awapongeza Lissu na Heche kwa ushindi
 
Nitamkumbuka kwa kuwalisha wajumbe miguu ya kuku kwenye mikutano yao.

Source: Mgombea uenyekiti aliyepata kura moja 😎
 
vijana wa lissu wataendelea kumtukuana, Ila ukweli utaendelea kubaki kuwa Mbiowe ndie aliyeijenga CHADEMA.
 
IMG-20220304-WA0042.jpg


Mimi nitamkumbuka hii siku alipopita mlango wa nyuma kutoka gerezani, moja kwa moja ikulu kulambishwa asali, huku wenzake wakiwa wanamsubiria lango kuu la Segerea.
 
Back
Top Bottom