Hisopo
Member
- Jun 28, 2021
- 21
- 39
Marekani na washirika wake hawakuwa sahihi kwenye suala la CUBA. Walitumia ubabe.
Pia hawakuwa sahihi kuivamia Libya. Tena ni tukio la kishenzi sana la Mmarekani alilowahi kufanya. Hawakuwekewa vikwazo kwa sababu hapakuwa na nchi yenye huo ubavu wa kufanya hivyo. Dunia yote ilinyamaza ikamuacha afanye yak...
Kwanza mkuu achana na porojo za magharibi (propaganda) kuwa "urusi imewekewa vikwazo na DUNIA YOTE""
Hiyo dunia yote ni ipi?! Hizi ni propaganda dhaifu sana mkuu, urusi amewekewa vikwazo na nchi za magharibi ambazo hazichukui hata nusu ya eneo la dunia, yaani ulaya magharibi na amerika kaskazini tu! Sasa hiyo ndio DUNIA YOTE?
Hebu tuache kuwa brainwashed na hawa western, dunia ni kubwa sana kuliko hao NATO, Tayari mataifa ya CHINA na INDIA yalikuwa ABSTAINED kupiga kura kwenye baraza la umoja wa mataifa kuilaani urusi that means kwamba yalikataa matakwa ya marekani , mpaka urusi ikawasifia,
Asia, Africa, Latin amerika, zote hizo hakuna hata nchi moja iliyotangaza vikwazo kwa urusi. Unasemaje dunia yote?! Dunia ni mataifa ya magharibi au?! Tuache kuwa brainwashed na western media, dunia ni kubwa kuliko NATO na western countries!