Kwa hizi siku mbili Ukraine ni kama kuna msiba - hata BBC inaonekana wana huzuni sana - kipigo cha Poltava kimewashtua watu juu ya hatari wanayochezea..na hapo zumetumika Iskander mbili tu.
West wameshtuka ni kama wanachezea sharubu za simba..Sweden huko kuna msiba mzito mpaka mtu kang'atuka.
Ukraine hawaamini kilichotokea - na mbaya zaidi makombora yameendelea kuvurumushwa miji mingine e.g.Kiev na Odessa.
Kule Donbass vijiji na miji inazidi kupotea..kwa spidi ambayo hata Urusi wanashangaa.
Watu vocal na waliochangia hii vita ya kijinga kupiganwa mtu kama KULEBA eti anatangaza kujiudhuru - anaenda zake US au Germany huko kula pension baada ya kusababisha mauaji ya watu wake wengi.
Hivi hawa wazungu walitutawalaje - mbona hawana akili, na wana ujinga mwingi - wao ndo wanaandika statistics...na wametufundisha kupitia western education tufanye maamuzi kwa kutegemea na statistics - SASA hivi kweli walitarajia UKRAINE ampige URUSI kweli??? Kweli kabisa...kwa hesabu zipi?? Hivi kweli ushinde vita kwa kutembeza bakuli wakati mwenzako anatengeneza mwenyewe??
Kingine et wanashauriana waingie Kursk..then so what??? Matokeo yake watu wao wazuri wamekufa bila sababu za msingi...hivi kweli unaweza ukaamuru military operation just for funny na kujaribu kushawishi watu??? Hivi ile Kurst ilivyo steppe vile kama uwanja wa mpira walitarajia wataenda mpaka wapi???
Hivi aisee hawa wazungu wana-jielewa kweli au wanafanya maamuzi kwa hisia????
Haya Sweden kaonja moto - kashtuka - naona alikua anahisi watu wanatania, Poland drones na makombora yaliishamfanyia harassment, akastuka, Romania aliguswa huyu akaelewa kidogo maana ya vita na nani wanapigana naye..
USA kwenye hii vita imejitahidi kutuliza fuvu, ingawa wanatoa pesa, lkn unaona wanajitahidi kucalculate risks na wakati mwingine wanawashauri Ukraine kutuliza akili.
Baadhi ya nchi za Ulaya ndo kama machizi vile - kula hivi vibaltic states- Estonia,Lativia, Lituania..vinachochea moto balaa havijua vinavhokitafuta, mwingine ni Uingereza huyu ndo alisababisha hii vita ikaendelea Boris alikataa mapendekezo ya amani akaishawishi Ukraine ipigane...miaka mingi warussi wamekua wakisema wanahitaji just 2 missiles kuzamisha visiwa hivyo na Uingereza ikafutika..lkn ni kama hawaelewi.
Najaribu kuwaza:
1. Zelensky ni agent wa Urusi - kwanza kakaa sana Moscow huyu..wanamtumia kuimaliza Ukraine.Hesabu zake hata mtoto mdogo hawezi chukua hizo risks
2.Boris Johnson ni agent huyu naye - kwanza hilo jina tu..Boris....huwezi ukawa na akili timamu ukalazimisha Ukraine ipigane na Urusi.
Biden huu msala hayumo tutamuonea tu..wakati vita vilianza Biden alimpa hifadhi Zelensky...na angeondoka vita ingekoma..
WAZUNGU WANAFANYA MAAMUZI KWA DATA KWELI AU WANATUMIA HISIA??