Spika Dkt. Tulia ajuzwe Wabunge 19 hawajawahi kuteuliwa na CHADEMA. Wameingia kwa kufoji nyaraka

Mkuu Fundi Mchundo, naomba kukiri wewe ni mmoja wa watu ambao you command highly respect kutoka kwangu hivyo criticism kutoka kwako, I take them very serious. Thanks for this.

Asante sana kwa ushauri kuhusu hayo mahojiano, naomba nisiahidi kitu chochote kwa sasa ila...
Nimalize kwa kukushukuru tena.
P
 
Tume ya Uchaguzi NEC imepokea barua ya uteuzi kutoka Chadema, ikawapa uteuzi na kumpelekea Spika majina Spika akatimiza wajibu wake. Anayejua kama barua hiyo ya uteuzi, ni bonafide genuine au ni fake, forgery ni mtu mmoja tuu, Chadema. Kama anajijua hajateua na hajaandika, then this is forgery, it's a police case. Chadema walipaswa kuripoti polisi ili uchunguzi wa kijinai uanze kwanza kwa kuthibitisha hiyo barua ni fake ni forgery, hili lingefanyika kazi ingekuwa imememalizika kitambo.
Ni ajabu sana kwanini Chadema hawataki to do the right thing?!.
P
 
Hili japo sijawahi kulifanyia mahojiano ila nimeliandikia humu na kushauri...
P
 
Nimesoma, katika 'post' zako za nyuma, ukisema Chadema wakalalamike Polisi.
Mimi naona ugumu.
Na naomba ushauri wako, maana nafahamu wewe ni Mwanasheria, na nataka nitoe mfano wa 'ki-laymen'.
"Nikijifanya kuwa 'Paskali' nikamtukana 'fundimchundo' kwa barua, 'Paskali' ambaye jina lake limetumika, atapeleka 'document' gani Polisi kulalamika wakati hana nakala ya hiyo document?
Unless Chadema wawe na 'copy' ya hiyo barua, how can they go to the Police?
And we all know that the National Election Commission will never give them a copy, IF AT ALL THERE IS ONE.
Kwa kuwa hii ni CONSPIRACY, I put it here that Tume ya Uchaguzi ilipeleka majina kwa Spika wa Bunge bila kungojea Fomu zinazojazwa na Chadema.
Ndiyo sababu mimi napenda sana Tume ya Uchaguzi iwekwe kwenye KITIMOTO cha P.
Paskali, sijawahi kuona mahali popote ambapo Tume imeulizwa kuhusu hili.
Tume yetu ya Uchaguzi imekuwa kama Mungu mtu.
Wewe P. na network uliyonayo, unao uwezo wa kulifanya hili kuwa AGENDA na likaanza kuzungumzwa kwenye TV, kwenye electronic media na print media.
Ikitokea hii, inaweza kufikia hatua, Tume ya Uchaguzi ikatoa majibu, au hata ITV wakamuita Mkurugenzi wa Tume kwenye 'Dakika 45'. Tutakuwa tumefaulu.
Paskali, tunakusikiliza.
 
Miaka 2 wanakula mishahara na posho jasho pa waTz kiharamu kabisa.

Kodi za walipakodi zinapotea bure sababu wanaozitumia hawastahili.

Timua hao COVID-19 bungeni ni wezi wa mishahara hao
 
Kwa kuwa Chadema walisema hawajajaza Fomu hata moja ya Viti Maalum, na wakazionyesha hadharani, sasa ifike wakati Tume ya Uchaguzi 'i-come clean' katika hili.
Tume ya Uchaguzi ilikata majina karibu yote ya Wagombea, na Watanzania, kama kawaida yetu, tukakaa kimya.
Hii siyo sawa hata kidogo.
Sasa wamejigeuza kuwa Chadema, wakajitumia majina wao wenyewe, kisha wakayapeleka kwa Spika wa Bunge!
Kwa nini hawaonyeshi hizo Fomu walizopokea kutoka Chadema ili tujue kuwa pengine huu ni mchezo ndani ya Chadema yenyewe?
Tume ya Uchaguzi itoe majibu.
 
Kanuni ya tuhuma dunia kote ni "he who alleges, must prove". Hata ikitokea issue ya mtu kuchapiwa, utakwenda kumuuliza aliyekuchapia kama amekuchapia, au utamuuliza aliyechapwa kama ni kweli amechapwa, baada ya kukuthibitishia amechapwa ndipo unakwenda kwa aliyekuchapia kumdai fidia kwa kukulia mali zako!.
Chadema ndio imefanyiwa forgery, the burden of proof lies with Chadema kuthibitisha hiyo barua ya uteuzi ni fake, forgery.
P
 
Mkuu Pascal. Huyo sio mimi. Huyo anajiita fundimchundo wakati mimi ni Fundi Mchundo. Nashukuru umechukua criticism yake in good spirit.

Amandla...
 
Nadhani hapa unakuwa disingenous. Spika na NEC hawajawahi kusema hadharani kuwa wanazo hizo nyaraka kutoka Chadema. Ki utaratibu barua ya NEC kwenda kwa Spika ikiambatisha barua ya uteuzi ya Chadema ilitakiwa inakiliwe kwa Chadema ili kuonyesha wamefanyia kazi barua yao. Hili hawajafanya. Kwa vile Spika amegoma kuwapa Chadema hizo nyaraka mpaka leo, Chadema hawana ushahidi wowote wa forgery. Ukweli ni kuwa hamna cha barua wala nini, Spika aliamua kuwaapisha na hamna wa kumuuliza. Hivi unaamini Ndugai angekuwa na barua (hata kama ni forged) angesitita kuiweka hadharani ili amuumbue Mbowe na Mnyika?
Mtu wa kufanya the right thing ni Spika na NEC. Hao ndio wanaotakiwa kuweka nyaraka zote walizotumia kufikia uamuzi wa kuwaapisha wakina halima hadharani. Chadema imetimiza wajibu wake kwa kuwaandikia na kudai wapewe nakala za barua hizo. Mpira uko kwa Spika na NEC.

Amandla...
 

Swali ni je!

Mnazitaka zile nafasi au hapana? Kama ni jibu ni yes then why hamkupeleka majina wakati mnatakiwa kupeleka? Kama jibu ni no then kuna shida gani hao covid kuwa huko? Coz hata malipo Yao hayatoki chadema
 

Bossi Kula lunch Kwa bili yangu

Wao wanajua majina ambayo waliyaweka ni majina ya watu gani
 
Polisi Tanzania? Hawa wanaomshikilia Mbowe kwa Ugaidi. Uchunguzi unazani utaisha leo? Au unataka kila wakihoji waambiwe kesi iko polisi inasubiri ushaidi ukamilike ata miaka 10? Na kwenda polisi NI tegemeo la CCM.
 
[emoji871]Kama kina halima waliingia kwa kufoji barua.

[emoji871]Chadema toweni barua yenye majina ya wateule halali.

[emoji871]Acheni ubabaoshaji,kuna clip ambayo ilirekodiwa baada ya majina kutumwa.

[emoji871]Mmojawapo aliyekuwa akiserebuka muziki na kina Mdee alikuwa Msigwa.
 
Ok,kwenye kufanya the right thing!Ni kwanini huhoji Hilo Hilo Kwa tume kwenye kufanya the right thing? Kwanini tume isingepokea malalamiko ya CHADEMA na kuyafanyia kazi na kuangalia kama ni kweli imedanganywa?Vipi kama ni kweli Kuna kughushi nyaraka Kwa hao wanawake 19,tume Ina wajibu gani katika hilo?Unadhani tume ingeamua kushirikiana na CDM Ili kubaini uhalali wa nyaraka Ile ingeshindwa?Sema ni mchongo uliokwisha sukwa na ndio maana suala la kuapishwa likafanywa Siri na mwingine akatolewa gerezani usiku asubuhi akaapishwa!Kwa vyovote vile CDM isingeweza kujua Nusrat ataachiwa lini,Kwa mantiki hiyo wasingeweza kumteua viti maalumu Kwasababu hawakujua hatima yake!
Mchongo ukipangwa,hata CDM wangefanya kila liwezekanalo bado wasingetoboa!
Nikukumbushe Lipumba alivyokuja na maamuzi ya ghafla ya kuwatimua uanachama viti maalumu wa CUF,Ndugai alikuwa India na akapelekwa taarifa Kwa maandishi huko!Kesho yake Spika akamuandikia NEC kuwa nafasi ziko wazi na siku iliyofuata NEC ikatangaza majina ya wabunge viti maalumu kufidia nafasi hizo!
Mchakato ulifanyika ndani ya siku 3 kufukiza na kujaza nafasi za viti maalumu wa CUF!
Hilo liliwezekana kwasababu CCM walikuwa na maslahi na Lipumba na hao viti maalumu walikuwa kikwazo kwenye Hilo kutokana na misimamo Yao!
Hata walipoweka pingamizi mahakamani,haikusaidia chochote!

So tuwe wakweli tu,suala la akina halima ni haramu iliyopangwa na Serikali,NEC na Bunge!
Hapo CDM wanawezaje kuchomoka?Shida ilianzia CDM walivyoonekana kwamba hawana Mpango wa kupeleka viti maalumu!
Nakwambia kama CDM ingekuwa na Nia ya kupeleka viti maalumu basi hao akina Halima wasingechukua round!
Pesa za mabeberu ndio chanzo cha uharamia huu!
Hizo nyingine mnazoleta ni ngonjera tu,ila uhalisia Huo ni mchongo na hakuna namna ya kuuepuka!
 
Wajuzi wa mambo haya tunaomba watusaidie je hawa wabunge wasio na chama ruzuku inayotokana na wabunge hawa inaenda wapi ?
 
Hujui kuwa CDM Ilikuwa haina Mpango wa kupeleka viti maalumu?Kwahiyo hata majina yalikuwa bado hayajateuliwa!
Kuona tutakosa pesa za mabeberu Kwa kukosa uwakilishi wa upinzani bungeni ndio Huo mchongo ukatengenezwa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…