Spika Ndugai aburuzwe Mahakamani kwa kuvunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Spika Ndugai aburuzwe Mahakamani kwa kuvunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mzalendo2015

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2012
Posts
6,710
Reaction score
9,063
Sakata linaloendelea kati ya Spika Ndugai, CHADEMA na wale Wabunge 19 waloapishwa kinyume cha Katiba ni aibu kwa Tanzania.
Ili kukomesha huu upuuxi wa Spika Ndugai CHADEMA lazima ifungue kesi Mahakamani haraka sana ili sheria ichukue mkondo wake.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iko wazi kabisa kuhusu mchakato wa uteuzi wa majina ya Wanawake wa Viti Maalumu toka chama chochote cha siasa chenye usajili halali. Spika Ndugai anajua hili na hata Rais Magufuli anajua hili. Lakini pia CCM, Jaji Mkuu, DPP na IGP wanalijua hili.

Kwamba ili Mbunge aingie Bungeni iwe ni kwa kuchaguliwa, kuteuliwa au Viti Maalum LAZIMA AWE MWANACHAMA WA CHAMA CHA SIASA KILICHOSAJILIWA kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Baada ya kinamama 19 wa CHADEMA kuvunja Katiba ya CHADEMA kwa kukiuka Sheria na Taratibu za Uteuzi wa Viti Maalumu kwa kujipa mamlaka ya kujipendekeza, kujiteua na kuwasilisha majina yao kwa Spika, Kamati Kuu CHADEMA iliwaita kuwahoji lakini wakakataa wito huo na hivo kupelekea KK-CHADEMA kuwatimua uanachama na hivo kupoteza sifa ya kuwa Wabunge wa Viti Maalumu.

Kwa akili za kijinga kabisa Spika ameamua kuwatetea hawa Wanawake 19 aliowaapisha akijificha kwenye kichaka cha kutetea Wanawake. Ndugai amesikika akisema hatakubali kina Mdee wavuliwe Ubunge wao maana ni uonevu Ndugai amehoji swali la kipuuzi kabisa ati Mbowe ni nani Nchi hii

Ndugai anajifanya hajui kuwa Mbowe ni Mwenyekiti wa Chama cha CHADEMA ambacho hao wanawake 19 aliowateua na kuwaapisha wametoka kama haitoshi Spika amemlaumu Mbowe kwa kunyanyasa wanawake haohao ambao waliumizwa kwa kuvunjwa mbavu,mikono na miguu na Polisi kwasababu ya Mbowe. Jeshi la Polisi ya CCM ndiyo walohusika na unyama huo lakini Ndugai anatupa lawama kwa Mbowe.

Bado Ndugai ametoa madai mazito kuwa Mbowe hataki hao Wanawake 19 waingie Bungeni kwa vile siyo vimada au wapenzi wa Mbowe au Mnyika. Huu ni udhalilishaji(defamation) kwa Viongozi wa CHADEMA.

Nawashauri CHADEMA wakiongozwa na Mwenyekiti Mbowe na Makamu wote 2 Tundu Lissu na Salimu Mwalimu wafungue kesi haraka sana Mahakamani kama ifuatavyo:
  • Kupinga uteuzi wa Wanawake 19 kuwa Wabunge Viti Maalumu ilhali sio Wanachama wa CHADEMA.
  • Kumshtaki Spika Ndugai kwa kuvunja Katiba ya nchi akilazimisha kuwatambua Wabunge Viti maalumu wasio wanachama wa CHADEMA.
  • Kuwadhalilisha Viongozi wa CHADEMA kwa kudai kuwa wanajihusisha na Rushwa ya Ngono ndani ya Chama.
  • Mwenyekiti Kaijage na Mkurugenzi NEC kwa kughushi barua na majina ya hao wanawake 19 na kupeleka kwa Spika.
Nawasilisha.
 
Spika anashtakuwaje kama ameletewa majina na tume ya uchaguzi? Kama ni mashtaka wa kushtakiwa ni Tume ya Uchaguzi. Pili, wakati wanateuliwa walikuwa ni wanachama wa CHADEMA hivyo hapo hakuna hoja. Hoja (mashtaka) yako matatu hayana mashiko.
 
Umesahau kuwa sasa Spika ana kinga ya kushtakiwa? Ndio maana yupo huru kufanya anavyojisikia, hakuna wa kumgusa.
 
Spika anashtakuwaje kama ameletewa majina na tume ya uchaguzi? kama ni mashtaka wa kushtakiwa ni Tume ya Uchaguzi. Pili, wakati wanateuliwa walikuwa ni wanachama wa CHADEMA hivyo hapo hakuna hoja. Hoja (mashtaka) yako matatu hayana mashiko.
Acha propaganda wewe.

Ndugai au Spika siyo Roboti kuwa kila anacholetewa anatekeleza bila ya kuchunguza na kutathimini kama Sheria na Taratibu zimezingatiwa.

Nitakuelewa kama utasema katika kesi hii waunganishwa Mwenyekiti Kaijage na Mkurugenzi Mahera wa Tume ya Uchaguzi(NEC).
Spika akiwa mbele ya Pilato ataeleza huo upuuzi wake.
 
Umesahau kuwa sasa Spika ana kinga ya kushtakiwa?Ndio maana yupo huru kufanya anavyojisikia, hakuna wa kumgusa.
Nobody is above the law.
Ndugai atajitetea mbele ya Mahakama kama kweli ana kinga kwa mujibu wa Katiba ya JMT.
 
Acha propaganda wewe.
Ndugai au Spika siyo Roboti kuwa kila anacholetewa anatekeleza bila ya kuchunguza na kutathimini kama Sheria na Taratibu zimezingatiwa.
Nitakuelewa kama utasema katika kesi hii waunganishwa Mwenyekiti Kaijage na Mkurugenzi Mahera wa Tume ya Uchaguzi(NEC).
Spika akiwa mbele ya Pilato ataeleza huo upuuzi wake.
Amini usiamini, SPIKA lazina anavielelezo vilivyowatambulisha wahusika kuwa ni Wabunge; mamlaka ya mchakato wa upatikanaji wao uko chini ya TUME YA UCHAGUZI na siyo SPIKA
 
Spika anashtakuwaje kama ameletewa majina na tume ya uchaguzi? kama ni mashtaka wa kushtakiwa ni Tume ya Uchaguzi. Pili, wakati wanateuliwa walikuwa ni wanachama wa CHADEMA hivyo hapo hakuna hoja. Hoja (mashtaka) yako matatu hayana mashiko.
Leo ndio nimeamini kuna watu wana kichwa bumunda na akili kisoda...yaani eti wakati wanateuliwa walikuwa ni wanachama wa chadema hivyo hapo hakuna hoja...ulisikia wapi mtu anateuliwa akiwa hana chama?
 
Hakuna uharaka huo. CHADEMA wao wafuate utaratibu tu ili muda wa kesi ukifika (kama tutafika huko) kuwe na evidence.

Tamko la kuwatimua wale 19 halitoshi. Utaratibu ni CHAMA kumuandikia barua Msajiri na kumpa taarifa na yeye ataandika barua kwenda kwa ofisi ya Speaker.
 
Leo ndio nimeamini kuna watu wana kichwa bumunda na akili kisoda...yaani eti wakati wanateuliwa walikuwa ni wanachama wa chadema hivyo hapo hakuna hoja...ulisikia wapi mtu anateuliwa akiwa hana chama?
"Kupinga uteuzi wa Wanawake 19 kuwa Wabunge Viti Maalumu ilhali sio Wanachama wa CHADEMA" hili shtaka lina ukweli?
 
Nyerere akukosea kujenga hospital ya milembe dodoma nadhani alifanya study isiyo shaka
 
Sakata linaloendelea kati ya Spika Ndugai, CHADEMA na wale Wabunge 19 waloapishwa kinyume cha Katiba ni aibu kwa Tanzania. Ili kukomesha huu upuuxi wa Spika Ndugai CHADEMA lazima ifungue kesi Mahakamani haraka sana ili sheria ichukue mkondo wake..
Mahakama ipi?
Hii ambayo ipo mfukoni kwa meko?
Time Wasting .

Tatizo sio ccm au chadema.
Tatizo ni Katiba
 
Sakata linaloendelea kati ya Spika Ndugai, CHADEMA na wale Wabunge 19 waloapishwa kinyume cha Katiba ni aibu kwa Tanzania. Ili kukomesha huu upuuxi wa Spika Ndugai CHADEMA lazima ifungue kesi Mahakamani haraka sana ili sheria ichukue mkondo wake...
Ni suala lamuda tu.

Huyu mjinga ndugai wadhifa wa uspika ni mkubwa mno kuliko uwezo wake. Viatu vinampwaya.
 
Leo ndio nimeamini kuna watu wana kichwa bumunda na akili kisoda...yaani eti wakati wanateuliwa walikuwa ni wanachama wa chadema hivyo hapo hakuna hoja...ulisikia wapi mtu anateuliwa akiwa hana chama?
Naomba ufafanue zaidi , unamaana gani?

Je Nyarandu alipojitoa uanachama aliendelea kuwa Mbunge?
 
Mahakama hizi hizi walizozikamata matako?

Mahakama ni hijacked,sio mahakama tena ni tool ya oppression ya hii regime!

Walao hata ile mahakama ya Africa,nayo wamejitoa juzi.....

Hawa jamaa kuwashitaki ni heri ukalime au uwahi ICC tu!

Bunge haliaminiki
Mahakama haziaminiki
Serikali na taasisi zake haziaminiki
Vyombo vya habari haviaminiki


Hakuna serikali wala nchi yenye kueleweka hapo!
Brother ulicho ongea ni sahihi!
Je, Tanzania hatuna Majaji wenye ujasiri kama Jaji Maraga wa Kenya aliyefutilia mbali matokeo ya Uchaguzi Mkuu Kenya?
 
CCM wamejifungia huko wanafanya tathmini ya uchaguzi uliopita na kuanza maandalizi ya uchaguzi ujao. Naona chandimu bado mnajadili kuhusu viti maalum poleni sana
 
Sakata linaloendelea kati ya Spika Ndugai, CHADEMA na wale Wabunge 19 waloapishwa kinyume cha Katiba ni aibu kwa Tanzania. Ili kukomesha huu upuuxi wa Spika Ndugai CHADEMA lazima ifungue kesi Mahakamani haraka sana ili sheria ichukue mkondo wake...
Bro hakuna nchi yenye viongozi wajaa ukatili na laana kama bongo yani apo hakuna cha Katiba wala nini na ao 19 watabaki bungeni maana paka uko Mahakamani wamejaa CCM sa sijui iyo kesi itakuaje mzee!?
 
Back
Top Bottom