Spika Ndugai kuangalia mtu katoka wapi kama kigezo cha ajira ni la kutafakarisha

Spika Ndugai kuangalia mtu katoka wapi kama kigezo cha ajira ni la kutafakarisha

Iruru

JF-Expert Member
Joined
Jan 27, 2014
Posts
1,471
Reaction score
2,891
Nimemsikiliza Ndugai akilalamika juu ya ajira zilizotangazwa na hasa akijikita kwenye ajira za ualimu.

Malalamiko yake yako kwenye kamati yake ya bunge kwamba hawafuatilii hizi ajira na namna zinavyopatikana. Hili la ufuatiliaji wa kamati ya bunge ni sawa kabisa.

Ila alienda mbali zaidi na hili ndilo lilinipa ukakasi. Ndugai anataka ajira zizingatie mgawanyo wa kieneo, yaani kila eneo katika nchi lipate uwakilishi sawa katika ajira.

Alitaja mifano michache ya ajira zilizopita kwamba aliangalia na kuona huyu ametokea kule, yule katokea kule na huyu katokea kule. Hoja yake hapa pamoja na kwamba hakutaja eneo wanalilotoka hao aliowataja ni kwamba kuna eneo la nchi hii lilipata wananchi wengi walioajiriwa.

Hoja yangu hapa ni hii, pamoja na kwamba ni sahihi kwamba kila mtu ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anayo haki ya kuajiriwa, ila utumishi wa umma hautakiwi kuangalia mtu katoka wapi kama kigezo cha ajira.

Ndugai kama spika wa bunge anatakiwa kujua sheria inavyotaka inapotokea suala la kuajiri. Ni lazima uajiri watu kwa merits zao na sio eneo wanakotokea.

Kwa jicho la husda, ni kama Ndugai yeye ajira zinazopitia kwenye himaya yake kuna watu huwa anawaangalia zaidi wapate ajira na wengine wasipate. Hii ni hatari kwa utumishi wa umma na nchi yetu kwa ujumla.

Mawazo ya kina Ndugai yasipothibitiwa, kuna hatari ya kulidodosha taifa hili hapo mbeleni.
 
Kweli mtoa mada hata mimi niliumia sana nilifikiria kama vyuo vinapokea bila kuuliza kabira la mtu, n.k hivo yeye angejikita kuangalia vigezo vinavyotumika kupata watu hao na vigezo hivyo vinapaswa vihainishwe kama wanaajiri kwa GPA au mwaka wa kuhitimu n.k yeye nilimuona kama mtu anayetaka kuleta ukabira ndani ya nchi hii ajue wazi makabira na mikoa inatofautiana katika lever za maendeleo.

Mfano ukienda uchsgani asilimia 85 ya wakazi wa pale utakuta wamesoma wakati ukienda longido au kiteto utakuta ni asilimia kumi tu ya watu walio soma hivo hsta ajira zikitoka unaweza kuta wamasai wawili na wachaga 20 au 30 huo ni mfano tu. Hivo Ndugai ni wakudhibiti mapema kabla ya yote maana kauli zake ni shida.
 
Huyu mkabidhini kwa Sir God kama mlivyomkabidhi Mzee wa Chato hivihivi bila huruma ya Mungu atawachefua tuu.
 
Mwendazake ndio alikuwa na hii tabia ya kujaza watu wa nyumbani kwake serikali

Alaaniwe sana
 
Huyu mkabidhini kwa Sir God kama mlivyomkabidhi Mzee wa Chato hivihivi bila huruma ya Mungu atawachefua tuu.
Ameshakabidhiwa kitambo tu mkuu, tunasubiri wkt sahihi wa Sir God atakapotenda kama itakavyompendeza.
 
Back
Top Bottom