Spika Tulia abebeshwa zigo la kashfa ya kupanda kwa bei ya mafuta ya Petroli Tanzania

Spika Tulia abebeshwa zigo la kashfa ya kupanda kwa bei ya mafuta ya Petroli Tanzania

saidoo25

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2022
Posts
624
Reaction score
1,456
Hali ya mafuta ni mbaya ambapo leo watanzania wenzetu wa Kyerwa Ruberwa Mkoa wa Kagera wanauziwa mafuta ya Petroli kwa Tsh 3,647 kwa lita huku wale wa Ukerewe Mkoa Mwanza wakiuziwa lita moja kwa Tsh 3,619 kwa mujibu wa Tangazo la EWURA.

Mjadala huu umeitikisa nchi tangu bei hiyo mpya itangazwe na EWURA usiku wa kuamkia leo huku watanzania wengi wakimtupia lawama kubwa Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson kwa kitendo cha kuzima hoja hiyo ilipoibuliwa bungeni kwa kile kinachodaiwa kulinda kibarua chake.

Wengi wanamtuhumu Dk. Tulia kwamba ndiye amelitumbukiza Taifa kwenye mgogoro huu mkubwa kutokana na kitendo chake cha kukataa ushauri uliotolewa bungeni na Mbunge wa Sengerema, Hamis Tabasamu kuhusu mchezo mchafu unaofanyika kwenye mfumo wa uagizaji wa mafuta.

"Kuna tatizo kubwa la bei ya mafuta katika nchi hii ambalo linaendelea kwa kasi kubwa na kutokana na hali hiyo ni kwamba mafuta yaliyoagizwa katika tenda za Tarehe 28/3/2022 tenda ile ilichezewa asubuhi ilitoka tenda nyingine, jioni ilitoka tenda nyingine, matokeo yake Mh Spika ni kwamba......" kabla hajamalizia Spika akamzuia kuendelea kusema.



 
Kuna haja ya EWURA na ZURA kuwatolea wananchi ufafanuzi zaidi wa upandaji holela wa bei za mafuta kwa miezi minne mfulilizo. Zaidi watuambie hayo mafuta YANAYOPANDA BEI KWENYE SOKO LA DUNIA wanayatoa kwenye soko la sayari gani?

Hoja yangu ni kwamba kwa mara ya mwisho bei ya mafuta ilipanda tarehe 05/06/2022 ambapo bei ya Brent Crude (soko ambalo ZURA waliwahi kutuambia wananunua mafuta) yalifikia $123.250 kwa pipa moja la mafuta yasiyosafishwa. Kutokea wiki mwezi huo, mafuta yameendelea kushuka bei na hadi naandika andiko hili, yanauzwa kwa wastani wa $99 hadi $103 kwa pipa moja la mafuta yasiyosafishwa.

Mafuta yalishuka hadi $92 katika wiki ya kwanza ya mwezi wa July. Maana yake ni kwamba stock ya mafuta ambayo imenunuliwa mwezi wa July (kwa mategemeo ya kutumika mwezi huu wa August 2022) yangekuwa rahisi zaidi. Cha ajabu yanaendelea kupanda kila mwezi. Kwa nini?

Kwenye soko la fedha, nguvu ya shilingi ya Tanzania dhidi ya dola ya Marekani iko stable kwa thamani ya $1/2315TZS hadi $1/2340TZS kwa kipindi cha miezi hiyo hiyo kuanzia April mwaka 2022. Maana yake ni kwamba shilingi ya Tanzania haijashuka thamani kwa zaidi ya asilimia 0.98%. Kwa hiyo sioni sababu ya kuja kusingizia ushukaji wa thamani wa shilingi ya Tanzania dhidi ya dola ya Marekani kama ni moja ya sababu ya kupandisha bei za mafuta hapa nchini.

Kwa uhalisia wa bei ya mafuta katika soko la dunia ilivyo sasa hivi, tulitarajia bei za July na August kushuka na sio kupanda kama mnavyodai kwamba bei zinaendelea kupanda. Ndio maana nikahoji hayo mafuta mnayoleta hapa nchini mnayatoa kwenye sayari gani? Kwa nini bei inaendelea kupanda na kutupoza kisaikolojia kwa subsidies za Serikali?

Tunasubiri ufafanuzi kwa nini bei zinaendelea kupanda hapa nyumbani. Tujibuni hizi hoja kwa upembuzi yakinifu na sio kauli za kisiasa. Msiumize wananchi out of ignorance ya kwamba wengi wao hawajui kinachoendelea na hawana access ya data ambazo wengine tunaweza kuzipata kwa sababu ya teknolojia.
 
Wao si wanapewa mafuta ya bure sasa kelele za nini bungeni.
 
Kuna haja ya EWURA na ZURA kuwatolea wananchi ufafanuzi zaidi wa upandaji holela wa bei za mafuta kwa miezi minne mfulilizo. Zaidi watuambie hayo mafuta YANAYOPANDA BEI KWENYE SOKO LA DUNIA wanayatoa kwenye soko la sayari gani?

Hoja yangu ni kwamba kwa mara ya mwisho bei ya mafuta ilipanda tarehe 05/06/2022 ambapo bei ya Brent Crude (soko ambalo ZURA waliwahi kutuambia wananunua mafuta) yalifikia $123.250 kwa pipa moja la mafuta yasiyosafishwa. Kutokea wiki mwezi huo, mafuta yameendelea kushuka bei na hadi naandika andiko hili, yanauzwa kwa wastani wa $99 hadi $103 kwa pipa moja la mafuta yasiyosafishwa.

Mafuta yalishuka hadi $92 katika wiki ya kwanza ya mwezi wa July. Maana yake ni kwamba stock ya mafuta ambayo imenunuliwa mwezi wa July (kwa mategemeo ya kutumika mwezi huu wa August 2022) yangekuwa rahisi zaidi. Cha ajabu yanaendelea kupanda kila mwezi. Kwa nini?

Kwenye soko la fedha, nguvu ya shilingi ya Tanzania dhidi ya dola ya Marekani iko stable kwa thamani ya $1/2315TZS hadi $1/2340TZS kwa kipindi cha miezi hiyo hiyo kuanzia April mwaka 2022. Maana yake ni kwamba shilingi ya Tanzania haijashuka thamani kwa zaidi ya asilimia 0.98%. Kwa hiyo sioni sababu ya kuja kusingizia ushukaji wa thamani wa shilingi ya Tanzania dhidi ya dola ya Marekani kama ni moja ya sababu ya kupandisha bei za mafuta hapa nchini.

Kwa uhalisia wa bei ya mafuta katika soko la dunia ilivyo sasa hivi, tulitarajia bei za July na August kushuka na sio kupanda kama mnavyodai kwamba bei zinaendelea kupanda. Ndio maana nikahoji hayo mafuta mnayoleta hapa nchini mnayatoa kwenye sayari gani? Kwa nini bei inaendelea kupanda na kutupoza kisaikolojia kwa subsidies za Serikali?

Tunasubiri ufafanuzi kwa nini bei zinaendelea kupanda hapa nyumbani. Tujibuni hizi hoja kwa upembuzi yakinifu na sio kauli za kisiasa. Msiumize wananchi out of ignorance ya kwamba wengi wao hawajui kinachoendelea na hawana access ya data ambazo wengine tunaweza kuzipata kwa sababu ya teknolojia.
Mkuu , Naona yanapatikana sayari ya mars. Watanzania tunafanywa mazuzu na,serikali yetu kwa kuwa hatuwezi kuhoji lolote tukasilizwa iko siku tutakuwa werevu ngoja kwanza tuendelee kuwa wajinga.
 
Tuna wabunge walopokaji walopokaji sana. Wanaongea bila ushahidi.
 
Huyu PhD fake kutoka dump university hamna kitu zaidi ni kum-https://jamii.app/JFUserGuide off maana ni feckless na wicked leader
 
Si mushukuru yanapatikana angalau?
Kwa mfano yaadimike kabisa itakuweje,
Tuipongeze serikali inafanya kazi kubwa chini ya waziri wa mafuta🤣
Nna hasira mujue ohooo
 
Back
Top Bottom