Spika Tulia Ackson ana "conflict of interest" katika Wizara ya Nishati, mume wake ni bosi wa EWURA

Spika Tulia Ackson ana "conflict of interest" katika Wizara ya Nishati, mume wake ni bosi wa EWURA

Samson Kwayu

Member
Joined
Jun 9, 2022
Posts
19
Reaction score
94
Leo asubuhi tumeshuhudia jinsi spika wa bunge Dokta Tulia akihaha kuhalalisha kuwa kikanuni akidi (idadi) ya wabunge imetimia na mjadala wa bajeti ya wizara ya nishati itaendelea tu japo kuna wabunge zaidi ya 200 wamesusia mjadala wa wizara ya nishati leo asubuhi.

Dr. James Andilile ni mume wa Spika Tulia na picha hii ilipigwa siku moja kabla ya bajeti wakati wizara hii ikifanya bonanza la kugawa mitungi ya gesi ambayo imetafsiriwa kama ni rushwa na Spika akatoa ufafanuzi jana kuwa hiyo siyo rushwa ni jambo la kawaida sana na liko kwenye bajeti ya wizara ya 2022/23. Japo tumetafuta sana fungu hili la kununua mitungi na kuigawa hatujaona kwenye bajeti aliyosema Spika Tulia.

Kwa kuwa mume wa Spika bwana Dr. James Andilile ni Mkurugenzi Mkuu wa EWURA ambapo waziri January Makamba anaisimamia EWURA akiwemo bwana James kwa vyovyote vile simuoni Spika Tulia akijizuia kupendelea na kutetea wizara anayotoka mumewe pale inaposhughulikiwa kwa michango ya wabunge au ukosoaji nje ya bunge.

Hili ni tatizo la kimaadili na kiuadilifu na kwa kutambua hilo nilitegemea Spika Tulia akae pembeni wakati wa mjadala huu ili kuondoa maneno yanayozagaa kuwa amekuwa matari wa mbele kutetea rushwa na uvunjwaji wa kanuni kwa kuwa wizara hii inamhusu mume wake.

View attachment 2642564
 
Hiyo picha iko wapi?

Kama sheria pendekezwa inataka walindwe wao mpaka vitukuu vyao, ajabu ni nini hapo mumewe kutoa TAKRIMA kwa gharama za WADANGANYIKA kisha yeye akakingia kifua?

UKOO WA PANYA huo!
 
Hiyo picha iko wapi?

Kama sheria pendekezwa inataka walindwe wao mpaka vitukuu vyao, ajabu ni nini hapo mumewe kutoa TAKRIMA kwa gharama za WADANGANYIKA kisha yeye akakingia kifua?

UKOO WA PANYA huo!
Hii
20230601_150555.jpg
 
Acha roho ya husda na uzushi wa kipuuzi. Mbunge gani anashindwa kununua mtungi wa gesi? Acha roho ya umaskini. eti wabunge wamesusa, we shwetani mzushi katafute kazi ya kufanya utakufa mapema na hiyo roho chafu.
 
Tanzania hakuna hiyo kitu munaita Conflict of interest mzee, mara ngapi tunashudia Polisi wanafanya umafia lawama zikizidi wanajichunguza wenyewe, hapa ni mbele kwa mbele tu, kwanza mliambiwa muwe na shukrani, kijana anatusaidia sana.
conflict of interest iko wapi, mbona mna akili finyu namna hiyo? Wizara ya nishati ina taasisi ngapi, huyo mume wake ndio waziri? Hata angekuwa waziri spika naweza kupitisha bajeti kwasababu ya mume wake? Acheni ushambenga.
 
Kila mtu ana haki ya maoni yake, nawe mleta mada umeitumia haki yako kikamilifu.

Sasa kazi kwetu, nasi pia tuna maoni yetu.

Maoni yangu binafsi, siioni sababu (motive) ya hiyo rushwa ya mitungi ya gas. Ni kitu ambacho mimi binafsi hakiniingii akilini.

Pia siioni "conflict of interest" ya tulia kwa sababu tu muwewe yupo ewura, ambayo ni idara iliyo chini ya wizara ya nishati.

Ingekuwa mume wa Tulia ni waziri, au naibu waziri au katibu mkuu wa wizara, hapo hata mimi ningesema hapa kuna "conflict of interest", lakini ilivyo, siioni hiyo "conflict of interest".
 
Tanzania tunahitaji sheria itakayoweza kumshtaki kiongozi alie tumia madaraka yake kinyume na kazi yake.

Hii kinga ya kuto shitakiwa ina sababisha uzembe maofisini na kuzorotesha maendeleo nchini.
 
Ni hivi hata uteuzi tu wa Dr. James Andelile tu pale EWURA una mashaka makubwa baada ya utenguzi wa Mhandisi Modestus Lumato. Zipo taarifa za ndani kabisa kuwa kuteuliwa kwa Dr. James kulikuja baada ya Mh. Lumato kukataa takwa la Njanuary la kutaka kupitisha/Kupiga kiasi pesa kupitia EWURA. Ndipo siku chache Njanuary akafanya figisu kwenda kumdanganya Mh. Rais kuwa Lumato anawachelewesha kwenye Utekelezaji wa Miradi ya maendeleo na ndipo akam-propose Dr. James awe DG Ewura na Instantly Mh. Rais kwa Kumwamini Njanuary akafanya hivyo.
 
Ni hivi hata uteuzi tu wa Dr. James Andelile tu pale EWURA una mashaka makubwa baada ya utenguzi wa Mhandisi Modestus Lumato. Zipo taarifa za ndani kabisa kuwa kuteuliwa kwa Dr. James kulikuja baada ya Mh. Lumato kukataa takwa la Njanuary la kutaka kupitisha/Kupiga kiasi pesa kupitia EWURA. Ndipo siku chache Njanuary akafanya figisu kwenda kumdanganya Mh. Rais kuwa Lumato anawachelewesha kwenye Utekelezaji wa Miradi ya maendeleo na ndipo akam-propose Dr. James awe DG Ewura na Instantly Mh. Rais kwa Kumwamini Njanuary akafanya hivyo lakini ukweli ni kwamba Njanuary kumpropose Dr. James ilikuwa ni kweka mtu ambaye atafaa kwa maslahi yake. jambo ambalo halikuwa rahisi kwa Mh. Lumato. So u can see viongozi wazalendo wanaondolewa madarakani kwa manufaa ya majizi na kwa sababu tu wapo na access ya kukutana na Mh. Rais na Kumdanganya kwa kadri wanavyoona inafaa.
Kwanza Waziri ana tuhuma za kuiba mitihani alipokuwa shule,sasa hiyo inatosha kujua tabia mbaya za muhusika!
 
Kila mtu ana haki ya maoni yake, nawe mleta mada umeitumia haki yako kikamilifu.

Sasa kazi kwetu, nasi pia tuna maoni yetu.

Maoni yangu binafsi, siioni sababu (motive) ya hiyo rushws ya mitubgi ya gas. Ni kitu ambacho mimi binafsi hakiniingii akilini.

Pia siioni "conflict of interest" ys tulia kwa sabu muwewe yupo ewura ambayo ni idara iliyo chini ya wizara ya nishati.

Ibgekuwa mume wa Tulia ninwaxiri, au naibu waxiri au katibu mkuu wa wizara, hapo hata mimi ningesema hapa kuna "conflict of interest", lakini ilivyo, siioni hiyo "conflict of interest".
"waxiri" ni kitu gani dada FaizaFoxy !!??
Huko shuleni ulienda kusomea ujinga!?
 
conflict of interest iko wapi, mbona mna akili finyu namna hiyo? Wizara ya nishati ina taasisi ngapi, huyo mume wake ndio waziri? Hata angekuwa waziri spika naweza kupitisha bajeti kwasababu ya mume wake? Acheni ushambenga.
Mbona povu limekujaa mdomoni, hili jukwaa huru chief, ukiendelea kuteseka hivyo utapasuka moyo na presha.
 
Back
Top Bottom