SRC ya Kenya Yaondoa posho za vikao vya Wabunge.

SRC ya Kenya Yaondoa posho za vikao vya Wabunge.

Linguistic

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2021
Posts
3,669
Reaction score
8,268
Wakuu Leo Tume ya mishahara Kenya (The Salaries And Remuneration Commission) imeondoa posho za vikao kwa wabunge 416 ili kuokoa Shs. 7.7 bilioni .
.
Wakati huo leo katika bunge la Tanzania, kuna wabunge 19 wasiokuwa wanachama wa chama siasa wamepokea posho na Per diem.
.
Wakenya Hii ikoje kwenu
 
Katiba Mpya. Tukiwaambia kwamba katiba ni muhimu zaidi ya jambo lolote lingine. Ikifika kwenye masuala yanayohusiana na uongozi na maendeleo. Kwamba ni kichocheo nyeti cha kutimiza maono na kutekeleza ruwaza ya nchi, ya maika na mikaka ijayo. Huwa mnaishia kutuambia kwamba sijui sisi manyang'au tunapenda misifa.

Hiyo SRC ni taasisi huru ya kiserikali, ambayo ilibuniwa na katiba mpya ya Kenya 2010. Majukumu yake sio kupunguza tu mishahara ya wakubwa. Bali ni pamoja pia na kusawazisha mishahara na mapochopocho ya wadogo zao, kwenye ngazi tofauti, kulingana na kazi wanazozifanya. Zaidi ya yote huwa wanatoa mapendekezo ya kupandishwa pia, kwa mishahara ya wafanyakazi kwenye sekta tofauti nchini Kenya.

Viongozi wa taasisi hiyo sio vibaraka wa rais, kwasababu huwa hawachaguliwi moja kwa moja na rais. Ndio maana wana kiburi cha kutekeleza majukumu yao, bila uoga, kisa wanajua kwamba wanalindwa sawasawa na katiba. Hii kwa kimombo ndio huwa wanaita 'checks and balances'. Jambo ambalo ni muhimu sana na huwa linapunguza kwa kiasi kikubwa, kiburi na ulevi wa madaraka wa hawa viongozi. Ambao huwa tunawachagua wenyewe, sisi kina Wanjiku.
 
Mama alisema mkimkuna atawakuna, mkimparua hatakawawia kuwaparua, mnapaswa mumkune taratibu akubali mchakato wa kupata katiba mpya, na ndio itakua suluhu kwenu.

Mimi hapa kama mmojawapo wa wahenga kiaina kwenye nchi yangu niliishi chini ya udhalimu uliosababishwa na katiba mbovu, na nilihusika sana kwenye mapambano hadi tukapata katiba mpya ambayo ilitutoa kimasomaso, nimeshuhudia mafao na manufaa yake, cool kids wengi wa leo hapa Kenya hawayajui hayo maana hawakuwepo enzi tulikua tunapitia magumu ya katiba mbovu kama ilivyo kwa Watanzania kwa leo.
 
Katiba Mpya. Tukiwaambia kwamba katiba ni muhimu zaidi ya jambo lolote lingine. Ikifika kwenye masuala yanayohusiana na uongozi na maendeleo. Kwamba ni kichocheo nyeti cha kutimiza maono na kutekeleza ruwaza ya nchi, ya maika na mikaka ijayo. Huwa mnaishia kutuambia kwamba sijui sisi manyang'au tunapenda misifa.

Hiyo SRC ni taasisi huru ya kiserikali, ambayo ilibuniwa na katiba mpya ya Kenya 2010. Majukumu yake sio kupunguza tu mishahara ya wakubwa. Bali ni pamoja pia na kusawazisha mishahara na mapochopocho ya wadogo zao, kwenye ngazi tofauti, kulingana na kazi wanazozifanya. Zaidi ya yote huwa wanatoa mapendekezo ya kupandishwa pia, kwa mishahara ya wafanyakazi kwenye sekta tofauti nchini Kenya.

Viongozi wa taasisi hiyo sio vibaraka wa rais, kwasababu huwa hawachaguliwi moja kwa moja na rais. Ndio maana wana kiburi cha kutekeleza majukumu yao, bila uoga, kisa wanajua kwamba wanalindwa sawasawa na katiba. Hii kwa kimombo ndio huwa wanaita 'checks and balances'. Jambo ambalo ni muhimu sana na huwa linapunguza kwa kiasi kikubwa, kiburi na ulevi wa madaraka wa hawa viongozi. Ambao huwa tunawachagua wenyewe, sisi kina Wanjiku.
you're talking about a concept Bongolalas can't grasp.

their opposition seems to understand that but the CCM neanderthals, the majority, are ignorant and want to keep the stale constitution.
 
Huu mchezo wa kawaikawaida kuelekea uchaguzi...mbona hawakufanya hivo 4 yrs ago 😭😭
 
Inapendeza kuwashughulikia hao ma-boy child...
 
Back
Top Bottom