Sridevi, Msanii wa Bollywood afariki dunia

Polisi Dubai wamesema ripoti zimeonyesha kuwa kifo cha muigizaji maarufu wa Bollywood (SRIDEVI) kilisababishwa na kuzama katika jakuzi bafuni baada ya kupoteza fahamu. Hapo awali vyombo vya habari vilitangaza kuwa muigizaji huyo alipoteza maisha baadaya kupatwa na mshtuko wa moyo. Lakini baada ya uchunguzi kufanyika imeonekana kuwa sababu hasa ya kifo chake ni kwamba alizama ndani ya jakuzi alipokuwa bafuni hotelini baada ya kupoteza maisha. Sridevi aliyekuwa na umri wa miaka 54 amekuwa katika ulimwengu wa filamu kwa miongo 5. Aliigiza filamu yake ya kwanza akiwa na miaka minne. MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU SRIDEVI MAHALA PEMA PEPONI...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…