St. Joseph Arusha Campus

Querido

Senior Member
Joined
May 12, 2014
Posts
176
Reaction score
109
Habari za wakati wana jamii forrum.............
ST. JOSEPH arusha campus ni moja ya vyuo vikuu. Kiko nje kdg ya jiji la arusha. Chuo kinatoa degree ya education {science]. Kilifunguliwa rasmi 2014.kiko chini ya wahindi
QUALITY OF EDUCATION..Ungozi wa chuo haujui maana na kazi ya curriculum na prospectus...ni baada ya kwenda field mwaka jana february ndipo walimu wengi walipotushangaa kwani kwa uzoefu wao kuna course za msingi ambazo tulitakiwa ziwepo bahati mby hazipo ktk miaka yote mitatu. Tukiwa chuoni tunafundshwa nyimbo za kindergate, vielelezo vya kihindi, kukusanya vizibo vya soda ili kuimprove maths...
LECTURERS... Walimu wa kihindi ni watu wanaoulalamikia uongozi wa chuo kwani unawshurutisha kufundsha vitu ambavyo hawajwai kusomea matokeo yake wanafunzi ndo tunawaelekeza hao walimu. Mbaya zaidi hawajui english....watz lecturers wengi wanaojielewa wamefukuzwa bada ya kukataa kushurutishwa kufundisha matango pori.
MIUNDO MBINU...hali ni mbaya zaidi kwani majengo zamani yalikua kiwanda hivo wamefoji, hamna ventilation, maabara yametengenezwa kama vyumba hamna emergency doors,chemicals,....hatuna dispensari na ukiumwa unambiwa "IS NON OF OUR BUSNESS" ..hamna hostels na mji mdogo wa kisongo umeshndwa kuakomodeti wanafunzi matokeo yke wanalala room moja wanafunzi kumi kwa shift na ndoo 1 ya maji ni 500.....
ADMINISTRATIONS.. kwa zaidi ya mwaka tulidai DEAN OF STUDENTS kwa nguvu waivomleta hana nguvu zozote.. hakuna mkuu [PRINCIPLE] anaedumu hata miezi mitatu wote wanabadilishwa.. hatukua na serikali ya wanafunzi kwa mwaka mzima na bado iliopo haina nguvu yakubeba mawazo ya wanfunzi.
MATATIZO NI MENGI hivo naomba wenye nia njema hatima ya taifa hili mliopo ST. JOSEPH SONGEA, DSM MAKAMBAKO, hata ZAMBIA tupaze sauti zetu kwa pamoja kwani tcu na wizara hawana meno mbele ya wahindi ila tukisimama kwa pamoja WAPO WATZ WENGI WENYE MAONO MEMA WATATUSAIDIA

NB......Niko mwaka wa pili ndo naingia semII ila hali ni tete hatujui nani atakuja tukomboa kwani kuna tetesi nyingi za kufungiwa,kuhamishwa,kufukuzwa,kurudia mwaka,kupewa diploma badala ya degree,...................
 

Umeingia kwa Form 4 au Form Six , Digrii munasoma Miaka mingapi?
 
nasomea edu in chemistry 3yrs degree

ni bada ya kumaliza form six
 
ni miongoni mwa vyuo ambavyo vingefutwa tu kama si kupunguza cumpus maana hawawezi kuvihudumia... yani mi ninapoona elimu ya chuo inafanyiwa mzaha hivyo huwa nakereka sana maana tz bila elimu tutazidi kutawaliwa tu
 
ni miongoni mwa vyuo ambavyo vingefutwa tu kama si kupunguza cumpus maana hawawezi kuvihudumia... yani mi ninapoona elimu ya chuo inafanyiwa mzaha hivyo huwa nakereka sana maana tz bila elimu tutazidi kutawaliwa tu
its true tatizo hakuna chuo ambacho kinaeza kutupokea bcoz education hii ni ya its own type haimatch na chuo chochote tz
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…