Staili mpya ya kupiga mizinga, kutoka kiwandani

Staili mpya ya kupiga mizinga, kutoka kiwandani

Socw

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2016
Posts
1,329
Reaction score
2,644
Wakuu...!

Mimi ni mpenzi mtizamaji kwa muda sasa ila nimeiona hii sina budi kuwasaidia wanaume wasiopenda vibomu. Kuna staili moja matata mno ipo mjini sasa hivi, iko hivi:

Unapata text yenye ujumbe kama huu (mfano), "Honey nipo hapa duka la nguo za kiume hapa, nimekuchukulia t-shirt, jeans na vitu vingine vidogo vidogo. Nilikuwa nataka nikuchukulie na viatu but imepelea elfu 47 sasa my kama unayo tuma sasa hivi maana ni viatu vizuri hope vitakupendeza darling"

Ukishasikia unaletewa viwalo si unasema Mungu anipe nini mie, nimepata mwanamke wa ukweli mimi na unaiachia elf 50 twaaaaa.

Saa kadhaa baadae, "Honey sijui hata nisemeje yaani wakati nakuja nimesahau mizigo kwenye bajaj halafu hata simfahamu, dah my yaani nimechanganyikiwa"

Hapo jua mzinga umefanikiwa kwa kipimo cha 5.7 richa
 
Mleta mada,wewe ni mwanaume au ni mvulana? Maana wanaume huwa hatupigwi mizinga bali huwa tunahonga.
 
Kama ndio umepokwa kwa njia hii basi pole sana....mimi hajanipiga kizinga cha hivyo!....nani kamwambia nahitaji nguo? Kama anataka kunizawadia kwa nini atumie pesa zangu?....hiyo issue ni ya kitoto sana.
 
ha ha ha ha ha nmecheka hapo kwenye richer ya 5.7
 
Mimi mwanmke kunichuna ni rahisi sana, afuate yale yote ninayoyapenda nnampa ela mpaka atachanganyikiwa
 
Yann kwanza mpaka uchomolewe kwa timing kiasi hicho!!!
Mtunze, akikushinda mbinafsisheee.
Wawekezaji tupo na mitaji ya kutosha, tunatafuta maeneo.
 
Back
Top Bottom