Starring ya gari kuwa ngumu kukata kona.

Nenda gereji inayoeleweka gari ifanyiwe uangalizi.
 
Acha ubishi mkuu sio gari zote zinatumia.hydrolic gari nyibgi now zinatumia sterling ya umeme inakuwa na mota. EPS,P/S
 
Mkuu steering power huna hapo nenda kabadili
 
Mkuu uko sawa ila inaitwa PAS pump yaani Powee Assisted Steerring Pump. Ikifa hio steering wheel inakuwa ngumu kama za Isuzu tani 7 za zamani.

Kingine kabla ya kubadili au kuongeza Power Steering Fluid ambayo mara nyingi ni ATF (automatic transmission fluid) inabidi kufanya flashing. Unachomoa pipe moja unajaza fluid unawasha gari na kuzungusha usukani. Ukimaliza ndio unnajaza mpya.

Ukifanya hivi ikiendelea kuwa ngumu ni kwamba pump imekufa.
 
Wanajamvi nini kinasababisha starring ya gari inakuwa ngumu unapokuwa unadrive hususani ktk kupiga kona?
Kwanza, inaitwa "steering" siyo "starring." Tatizo hili husababishwa na mojawapo kati ya haya mambo matatu tu.
(1) Mafuta ya steering yamekwisha. Inabid uongezee kama kweli mafuta yako ya steering yamepungua; kwa magari mengi mafuta haya ni DOT3 ila inabidi uangalie gari lako linahitaji mafuta gani.
(2) Steering box yako imeharibika kiasi kuwa kuna gaskets na oil seals ambazo hazifanyi kazi tena, inabidi ama ubadili steering box, au uifanyie overahaul steering box yako.
(3) Inawezekana belt inayoendesha steering box yako imeshalegea au imekatika kabisa. Hii hutokea sana iwapo injini yako inatumia belt tofauti kati ya Steering na AC na Alternator.
 

Hakuna gari inayotumia hayo mafuta kwenye steering mkuu hayo yanatumika kwenye mfumo wa brake na magari yanayotumia clutch.....Jinsi dot 3,4 yalivyomakali kila siku itakuwa kazi YA kubadili zile pipe yatakuwa yanazikatakata
 
Wanajamvi nini kinasababisha starring ya gari inakuwa ngumu unapokuwa unadrive hususani ktk kupiga kona?

Hilo tatizo lilinikuta wiki hii..

Nilianza kuiona hiyo hali kidogo kidogo lakini baadae ikawa serious. Yani usukani mgumu sana na mngurumo wa ajabu hata sauri ya engine husikii..
Tatizo lilikuwa ni stearing pump ilikufa. Niliponunua nikafunga tatizo limeisha kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…