Stephen Wassira: Nini maana ya uongozi wa kimkakati?

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
February 10, 2020
Dar es Salaam, Tanzania

Mwanasiasa mkongwe Ndugu Stephen Wassira anashusha madini kuhusu Uongozi wa kimkakati akihojiwa na watangazaji Sam Sasali, Hassan Ngoma na Babbie Kabae


Stephen Wassira ambaye zamani alipata kuwa kiongozi ktk nafasi ya uWaziri, mkuu wa mkoa, mbunge na afisa balozi Marekani anatumia uzoefu wake kuangazia wakati wa ukoloni, awamu baada ya uhuru za Nyerere, Mwinyi , Mkapa , Jakaya Kikwete na mikakati ya viongozi hao na hali ya sasa.

Stephen Wassira alibanwa kuhusu suala la Dira ya Taifa kukosa undelevu na kila kiongozi anayeingia madarakani huja na yake. Wassira akakumbushwa nchi kama Marekani dira ya taifa aje Rais mwingine au chama kingine iwe Republican au Democrats, Dira ya Marekani haiyumbi. Lakini kwa Tanzania kila kiongozi anayechukua mamlaka huja na jambo linaloitoa nchi kutoka ktk Dira mfano Kilimo Kwanza tatizo ni nini?

Watangazaji wanauliza kushirikishwa kwa wananchi ktk maamuzi makubwa na nafasi ya kuwepo hoja kizani ndiyo hujenga dira madhubuti itakayozingatiwa kila awamu na haitaathiriwa na mabadiliko ktk uongozi, je hali ya kisiasa na kijamii Tanzania inazingatia hilo?

Mfano Mradi mkubwa wa reli mpya ya SGR unaogharimu ma-Trilioni ya shilingi za kiTanzania unaonekana haupo ktk Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025 iliyozinduliwa miaka 20 iliyopita , na Wassira anakiri haijulikani lini SGR Mpya itakamilika . Mradi huu umeanzishwa na CCM Mpya.

Wassira azungumzia fedha za World Bank za elimu na changamoto za jinsia / gender nini kifanyike mimba zipungue shuleni. Pia nini maana ya uzalendo na utaifa pamoja na misemo iliyozuka awamu hii kulinganisha na awamu zilizopita.

Stephen Wassira mahojiano yake yanajikita ktk taifa kuwa na Dira / Visheni anazungumzia juu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya Tanzania 2025 toka taifa hili linapata uhuru na awamu zote za uongozi zilivyopambana na changamoto za nyakati zao kuhakikisha nchi inavuka na kuwa nchi ya uchumi wa kati ya viwanda na maisha bora zaidi kwa wananchi.

Source: CLOUDSMEDIA

 
Wasira ndiye mtanzania pekee aliyefanya kazi serikalini kwa muda mrefu kuliko wote hapa nchini.
 
February 7, 2020

Washington, Maryland DMV
USA

Mpango mkakati wa Mh. Zitto Kabwe akipewa nafasi ya Urais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mpango mkakati wa Mh. Zitto Kabwe akipewa nafasi ya Urais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati akijibu maswali ya waTanzania diaspora Marekani na wadau mbalimbali wa maendeleo waliotaka kujua Tanzania ya kesho inatambua changamoto gani zitatuliwe kiuchumi, kijamii na kisiasa nchi irudi tena katika reli ya taifa lenye umoja na uchumi imara.


Mh. Zitto Kabwe anaainisha matatizo ya serikali ya CCM Mpya jinsi isivyokuwa na Uongozi Mkakati wala kuongozwa na Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025.

Mfano mradi mkubwa wa SGR reli mpya haukufuata Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025 na kusababisha kutochochea uchumi wa Tanzania. Na reli hii haina muda time frame utaisha lini pamoja yakuwa wahandisi wa reli walikadiria utachukua walau miaka 15 wakati CCM mpya walidhani utakwisha 2019.

Mh. Zitto Kabwe anaainisha umeme toka bwawa la Stiegler's Gorge maarufu kama Bwawa la Umeme la Rufiji mega watt 1 labda itaanza kuzalishwa na kuongozwa ktk gridi ya taifa mwaka 2030 subject to serikali itaweza kuendelea kuwalipa wakandarasi ktk muda muafaka na mikopo ya wadau wa maendeleo kupatikana kwa wakati.

Na miradi mingi mikubwa mingine imeanzishwa kwa matamko na pesa asilimia kubwa kulipwa kwenda nje ya nchi bila mikakati thabiti na kuzidisha kuyumbisha uchumi wa nchi na kipato cha mwananchi mmoja mmoja kiasi cha raia kulia ugumu wa maisha umezidi maradufu na pesa kukosekana mifukoni na mitaani.

Source : Mutwiba
 
Wassira amechoka apumuzike!!!!! Eti ameanza kupanga watu ili agombee tena Ubunge jimboni Bunda!!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…