Stop Foreign Aid to Tanzania Campaign!!

Watoaji misaada wanafaidika sana kwa hiyo hawawezi kuacha.Watanzania ni two bit players tu.
 
Majibu yangu yatarudi huko huko Wamarekani. Nchi yoyote utakayouliza jibu lake ni Wamarekani.

Hihihihihiiiiii...this is funny!! Kweli Wamarekani wana moyo mzuri kweli....

Kwa nini Wamarekani wanasaidia kila nchi?
 
Hihihihihiiiiii...this is funny!! Kweli Wamarekani wana moyo mzuri kweli....

Kwa nini Wamarekani wanasaidia kila nchi?

kwa sababu "wana moyo mzuri kweli"... usiulize kwanini wana moyo mzuri..
 
Kwanini wakisitisha misaada hali iwe "mbaya"? Ina maana pasipo hii misaada Watanzania hawawezi kuishi?

Mkjj nafikiri kampeni isiwe kusitisha misaada, bali iwe " Kuwataka wanaotoa misaada hiyo, waje kusimamia utekelezaji wake wao wenyewe", yaani kama ni kujenga shule wanajenga wao, kama ni barabara wanafanya wao halafu sisi wanatukabidhi kitu ndani ya box tu. Serikali yetu ikigoma maana yake wamekataa misaada. Wasitupe cash watupe vitu, maana sisi hatuwezi kusimamia cash tunapagawa nazo na kusahau wametupa za nini?, mbona nyingi?.

Sisi tumeshindwa kujitawala basi tuwaache watutawale kiutekelezaji, kazi yetu iwe kuwaambia kuwa barabara ile mbovu wao wanatujengea, vyoo vile vimeziba wao wanatumia pesa zao kutuzibulia. Nafikiri tukifanya hivyo Ndani ya miaka mitano nchi itakuwa na mandhali tofauti kabisa.
 

Katika mazingira hayo tunaweza kuomba watuchagulia Rais na wasaidizi wake; Sasa tukiwakaribisha kwa hiari yetu waje watutawale tunaweza kuuita huo ni "ukoloni" au ndiyo "urafiki wa karibu"?
 
Katika mazingira hayo tunaweza kuomba watuchagulia Rais na wasaidizi wake; Sasa tukiwakaribisha kwa hiari yetu waje watutawale tunaweza kuuita huo ni "ukoloni" au ndiyo "urafiki wa karibu"?

Hapana huo hautakuwa ukoloni ni urafiki Mzee Mkjj, ukoloni utakuwa ni pale tu wanapoingia kwa mabavu na kutulazimisha, lakini kama ni kwa hiari yetu hiyo itakuwa ni heshima kubwa kwetu, kwani wanaweza hata kutusaidia ku-identify watu faithful na makini wasio na tamaa ya kujulimbikizia mali, kwani hilo sisi tumeshindwa kulitatua kwa mtazamo wetu finyu.

Tena kutakuwa hakuna kuogopana kwani ukitenda kosa ukifikishwa mahakamani hata kama wewe Rais mstaafu hutaweza kuwalaumu watanzania wenzako na hasa chama chako, kwani tutasema ni mabwana wakubwa ndiyo walioamua ufungwe.

Baada ya sisi wote kuwa na mitazamo tofauti kwa nchi yetu na kuweka uwajibikaji na masilahi ya wengi na Taifa mbele hapo ndipo, tunaweza anzisha kampeni ingine ya kuwataka wawe watazamaji zaidi badala ya wachezaji. Ila kwa sasa suluhisho ni hilo.

Tunajiona tuna uhuru pasipokuwa huru, watu tunaogopana kwa ranks na uwezo wa fedha, wahalifu wapo katika madaraja kuna VIP na sogea twende, Ukiiba kidogo unashughulikiwa ila ukiiba kingi unalindwa, kwa hawa mabwana wakubwa haya hayapo.

Solution ni kuwaita tena watufanyie mambo wanayotaka sisi tufanye badala ya kutupa blank cheques.
 
Mzee mwanakijiji, Misaada hii tuliyokwisha pewa toka tumepata uhuru kama ingelikuwa na maana basi tungelikuwa mbali sana. Tena tungelikuwa tunawazidi ulaya yenyewe kwa maendeleo!
Lakini misaada hii hawa wenzetu hawatupi kwa kuwa wanatupenda sana, hapana, bali hiki ni chanbo tu ili wajisogeze kwetu na kuja kubeba rasilimali zetu.
Na viongozi wetu ni majuha sana maana utawasikia wanajisifia sana kwa wapiga kura kwamba wamefanikiwa kuwashawishi wafadhili kuendelea kutufadhili (Sio tumeomba kama Matonya ila tumomba ufadhili ) na kwa mtaji huo nasi wapiga kura tuwape uongozi ili waendelee kuwa omba omba. Ajabu sana kwa mtaji huo huo majuha wenzao wanawapatia.
Nitashangaa watu wakisema tupewe na waje kusimamia wenyewe. Sasa hapo tumejitoa kuwa koloni?
Hakuna jingine.
 
Kulikuwa na kampeni ya kusitisha madeni iliyoongozwa na Jubilee 2000, madeni mengi yakasamehewa; lakini inflow ya foreign aid haikuwa lengo hasa matokeo yake, baada ya madeni kusamehewa mataifa yaliyokuwa Highly Indebted Poor Countries yakajikuta na zaidi ya mabilioni ya dola; hapa ndipo ufisadi ukaanza kujitokeza kwa nguvu sana (kuanzia mwaka 2000 hivi).

Tukiweza kuziba mtiririko huu wa fedha za dezo, tutaweza kusababisha utawala unaojua kuweka kipaumbele kweli.
 

Ngongo nakubaliana na maoni yako mazito...Nakubaliana kuwa misaada isimamishwe.
Hivi tukiangalia kiundani nani anamsaidia nani?
I mean honestly...Wanachochukuwa na wanacholeta kipi kina thamani kubwa zaidi ya kingine?
Mimi nadhani sisi ndio tunatowa misaada na malipo yao nadhani ni kidogo na hivyo ni budi kuyasimamisha.
Ila hatuwezi kufanya hivyo ni hadi uongozi huu wa bora liende uondolewe...I mean mapinduzi ni lazima otherwise hatuendi mahali na hii ni guaranteed.
Saa nyingine ni bora kuvunja na kujenga upya badala ya kurepea tu.
Ufa tulionao ni mkubwa sana and so we need a new direction in whatever means neccessary.
Kwani tumeshajiuliza kuwa nini hasa mikakati ya muda mrefu ya misaada hiyo ambayo tumekuwa tukipokea mara baada ya uhuru wa bendera?

Ama misaada ndiyo imekuwa utamaduni na biashara?
No wonder NGO zimekuwa deal na wasomi wanazianzisha tu huku wakisubiri kuzikinga pesa za misaada ya UKIMWI,malaria,homeless kids etc.

Tujifunze sasa watanzania na tuelewe na kuzisoma jamii nyingine zinazotunzunguka na tunazo interract nazo...Je ni kweli watu hao wana nia ya kusadia ama ni mtandao wa kifisadi duniani kote kati ya mafisadi dhidi ya raia masikini?

Hatuhitaji misaada tunahitaji viongozi wapya wenye fikra mpya za kimapinduzi za kutupeleka in a different direction ....Tunachohitaji ni Positive ideas,better techology,Fair trade na baada ya hapo mambo safi.

Tukipewa share yetu fair kwenye biashara na kuwapatia wananchi kazi basi tutatumia pesa zetu kununuwa hayo madawa,neti na kondom kwa pesa zetu waache kutuyeyusha hao wakoloni na manyapara wao mafisadi.
Time is over.
 
Kuna mtu kaniambia leo ingekuwa inawezekana tubadilishane na wazungu-yaani wazungu waende kwetu Africa na sisi tuhamie kwao. Akasema baada ya miaka miwili tungeanza kujipanga kuomba visa kwenda Tanzania na nchi zingine za Africa tena! Inawezekana hii ni kweli hee??
 

Hii mbona ya zamani sana.....where have you been...under a rock?
 

Ngabu, nimeipenda sana post yako. Great. ngoja nisake moja niliyowahi andika hapo kitambo inayofanana..
 
as usual attention seeking at its best

Unasema tukatiwe misaada kwa saabu you are not on the dround

last time nilipokuwa kijijini kwetu nilikuwa miradi ya donors kibao inasaidia watu

Naona boksi hapo D town linakuhemea sana

kama unashida ya pesa kwa nini usiongee na tuu watu wakakusaidia?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…