Stori kamili na picha juu ya P-Funk kufunga ndoa ya siri

Money Stunna

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2011
Posts
13,053
Reaction score
6,304

Baada ya kuishi maisha ya kisela kwa muda mrefu, hatimaye mtayarishaji nguli wa muziki Bongo, Paul Mathyasse ‘P Funk’ ameoa kwa siri.
Mtayarishaji nguli wa muziki Bongo, Paul Mathyasse ‘P Funk’ wakati wa harusi yake. Taarifa kutoka kwa chanzo makini kilichoshuhudia tukio hilo, lilichukua nafasi jijini Arusha mwishoni mwa wiki iliyopita kwa usiri mkubwa. Imeelezwa kuwa, P Funk aliamua kumuoa rasmi mzazi mwenzake, Samira baada ya kuishi naye kwa miaka kadhaa kama mke na mume lakini haikujulikana mara moja sababu za kuweka usiri katika tukio hilo la kheri.
Maharusi wakipongezwa na ndugu na jamaa zao baada ya ndoa. “Jamaa (P Funk) amevuta jiko rasmi kwa siri kubwa lakini ameamua kufanya siri hata sijui ni kwa nini, tukio limechukua nafasi huku Arusha na watu kadhaa walialikwa lakini mastaa siyo wengi. “Sherehe imefana, watu wamekula, wamekunywa kwelikweli maana misosi ilikuwepo ya kumwaga,” kilisema chanzo hicho. Chanzo hicho kilizidi kumwaga data kuwa, katika harusi hiyo, kulikuwepo na ulinzi mkali wa watu kuzuiwa kupiga picha hivyo matukio mengi kushindwa kusambaa mtandaoni. “Daah! Ilikuwa ngumu sana, watu hawakuruhusiwa kupiga picha, hata simu zilizotumika zilikuwa zaidi ni za bwana na bibi harusi na ndugu wa karibu,” kilisema chanzo.
 
Afadhali,maana ushakula ujana vya kutosha
 
P Funk yupo ki hip hop hana mbwembweeer kama kina fulanii,
 
Je kabadili dini au ndoa imefungwa dini gani maana naona samira na paulo
 
Je kabadili dini au ndoa imefungwa dini gani maana naona samira na paulo

Ndiyo nashangaa, huyu bwana long time kitambo wakati tunacheza basketball oysterbay kwa kina Master J alikuwa anaitwa Khalfan ila jina la PFunk lilikuwepo Sasa hili jina la Paul. Ndiyo nakuna kichwa.
 
sasa hapo khalfan kafanya siri gani, wakati watu wamealikwa.....?
 
Je kabadili dini au ndoa imefungwa dini gani maana naona samira na paulo

Baba yake mkristo,mama ya muislam....ila hajawai kugusa church wala masjid...sijui tuseme alikuwa dini gani
 
Ndiyo nashangaa, huyu bwana long time kitambo wakati tunacheza basketball oysterbay kwa kina Master J alikuwa anaitwa Khalfan ila jina la PFunk lilikuwepo Sasa hili jina la Paul. Ndiyo nakuna kichwa.

Paul na Khalfan yote ni majina yake. I guess la Paul alipewa upande wa Baba yake na Khalfan upande wa Mama yake kwani upande huo ni Waislamu.
 
Huyu bi Dada anaitwa samira au hidaya?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…