Story hii ya ombaomba inaonesha jinsi watu wanavyochukulia wema wako kama haki yao

Story hii ya ombaomba inaonesha jinsi watu wanavyochukulia wema wako kama haki yao

Ugwanzee

Senior Member
Joined
Mar 7, 2024
Posts
137
Reaction score
225
Mwanaume mmoja alikuwa akimpa ombaomba $1000 kila mwezi. Alifanya hivyo kwa muda fulani bila kukosa. Siku moja, alimpa ombaomba $750 pekee. Ombaomba alishangaa, lakini akajiambia, "$750 ni bora kuliko kutopata chochote," kisha akaondoka.

Baada ya mwezi mmoja, mwanaume alimpa ombaomba $500 pekee. Ombaomba alishangaa zaidi na kumuuliza, “Ulikuwa unanipa $1000, kisha ikapungua na kuwa $750. Sasa ni $500. Kwa nini? Naweza kujua sababu?”

Mwanaume akamjibu, “Hapo awali, watoto wangu wote walikuwa wadogo na hali yangu ya kifedha ilikuwa nzuri, ndiyo maana nilikuwa nakupa $1000 kila mwezi. Baadaye, binti yangu alikua na akaingia chuo kikuu, na gharama za chuo ziliongezeka, hivyo nikaanza kukupa $750. Sasa, mwanangu wa pili amejiunga na chuo kikuu, gharama zimeongezeka zaidi, ndiyo maana nimekupa $500.”

Ombaomba akamuuliza, “Una watoto wangapi?”

Mwanaume akajibu, “Wanne.”

Ombaomba akamuangalia kisha akasema, “Na unataka niwasomeshe wote kwa pesa zangu?!”

Mara nyingine, watu huchukulia wema na ukarimu kama haki yao badala ya kuona ni fadhila kutoka kwako.
 
Il
Mwanaume mmoja alikuwa akimpa ombaomba $1000 kila mwezi. Mwanaume huyo aliendelea na hali hiyo kwa kipindi fulani. Siku moja, alimpa ombaomba $750 pekee. Ombaomba alishangaa, lakini akajiambia, "$750 ni bora kuliko kutopata chochote." Kisha akaondoka.
Baada ya mwezi mmoja, mwanaume alimpa ombaomba $500 pekee. Ombaomba akashangaa sana! Akamuuliza yule mwanaume, “Ulikuwa unanipa $1000, kisha ikapungua na kuwa $750. Sasa $500, kwa nini? Naweza kujua sababu?”
Mwanaume akamjibu, “Hapo awali, watoto wangu wote walikuwa wadogo na hali yangu ya kifedha ilikuwa nzuri, hivyo nilikuwa nakupa $1000. Baadaye, binti yangu alikua na akaingia chuo kikuu, na gharama za chuo zilikuwa kubwa, kwa hiyo nikaanza kukupa $750. Sasa, mwanangu wa pili amejiunga na chuo kikuu, na gharama zimeongezeka zaidi, hivyo nimekupa $500.”
Ombaomba akamuuliza, “Una watoto wangapi?”
Mwanaume akajibu, “Wanne.”
Ombaomba akamuuliza, “Na unataka niwasomeshe wote kwa pesa zangu?!”
Mara nyingine, watu huchukulia wema na ukarimu kama haki yao badala ya kuona ni fadhila kutoka kwako.
Ila huyo ombaomba kazidi yaani, maana nikikadiria kulingana na story, huyo ombaomba alikuwa anaomba Toka watoto wa uyo jamaa anae msaidia wapo wadogo mpaka wamekuwa wapo chuo kikuu Bado anaomba duuuh, Kwaiyo ombaomba yupo katika kazi yake ya kuomba sii chini ya miaka 15.
 
Il

Ila huyo ombaomba kazidi yaani, maana nikikadiria kulingana na story, huyo ombaomba alikuwa anaomba Toka watoto wa uyo jamaa anae msaidia wapo wadogo mpaka wamekuwa wapo chuo kikuu Bado anaomba duuuh, Kwaiyo ombaomba yupo katika kazi yake ya kuomba sii chini ya miaka 15.
Kuna mama alihojiwa ITV ni ombaomba
Ana nyumba 2 na watoto anawasomesha alisema kajenga kwa kazi ya kuomba.
 
Kuna mama alihojiwa ITV ni ombaomba
Ana nyumba 2 na watoto anawasomesha alisema kajenga kwa kazi ya kuomba.
Yupo mmoja kariakoo nilimchangia mia mbili mchana nikakuta anakula biriani y ngamia na juisi ya matunda ya buku jumla elfu saba mchana tu. Nikagoma mpaka leo kuwasaidia. Naskia anapelekwa kwake kimara na pikipiki wakati waliomsaidia wanapanda mwendo kasi
 
Nishaachaga kuwapa hela ombaomba wanaokaa barabarani.
 
Mwanaume mmoja alikuwa akimpa ombaomba $1000 kila mwezi. Alifanya hivyo kwa muda fulani bila kukosa. Siku moja, alimpa ombaomba $750 pekee. Ombaomba alishangaa, lakini akajiambia, "$750 ni bora kuliko kutopata chochote," kisha akaondoka.

Baada ya mwezi mmoja, mwanaume alimpa ombaomba $500 pekee. Ombaomba alishangaa zaidi na kumuuliza, “Ulikuwa unanipa $1000, kisha ikapungua na kuwa $750. Sasa ni $500. Kwa nini? Naweza kujua sababu?”

Mwanaume akamjibu, “Hapo awali, watoto wangu wote walikuwa wadogo na hali yangu ya kifedha ilikuwa nzuri, ndiyo maana nilikuwa nakupa $1000 kila mwezi. Baadaye, binti yangu alikua na akaingia chuo kikuu, na gharama za chuo ziliongezeka, hivyo nikaanza kukupa $750. Sasa, mwanangu wa pili amejiunga na chuo kikuu, gharama zimeongezeka zaidi, ndiyo maana nimekupa $500.”

Ombaomba akamuuliza, “Una watoto wangapi?”

Mwanaume akajibu, “Wanne.”

Ombaomba akamuangalia kisha akasema, “Na unataka niwasomeshe wote kwa pesa zangu?!”

Mara nyingine, watu huchukulia wema na ukarimu kama haki yao badala ya kuona ni fadhila kutoka kwako.
Huyo ''tajiri'' naye ana sehemu ya lawama. Alimzoesha sana na kumlemaza. BTW hata mimi ninapoenda kijijini nilikozaliwa huwa nina ukarimu wa kuwapa wazee ninaowafahamu ''fedha za ugoro''. Hata vijana wa jirani fedha za soda huwa nawapa. Ikitokea siku nikaenda likizo hali ikiwa tight usimpompa mtu chochote anakasirika na wako wanaotukana kabisa.
 
Pitia hili andiko utajifunza zaidi.

 
Kuna mmoja nilimpa sabuni akaksirika akasema "acha upumbavu unanipa sabuni ya nini" ,, Mimi hao watu siwapagi chochote kile
 
Yupo mmoja kariakoo nilimchangia mia mbili mchana nikakuta anakula biriani y ngamia na juisi ya matunda ya buku jumla elfu saba mchana tu. Nikagoma mpaka leo kuwasaidia. Naskia anapelekwa kwake kimara na pikipiki wakati waliomsaidia wanapanda mwendo kasi
Hao ni CCM.
Wana maisha mazuri kuliko raia walipa kodi wa marekani.


Ombaomba mwenyewe ni Tanzania kupitia ccm....hujasikia wanavyomfokea Trump kwa kukata misaada? Walishachukulia hizo hela za walipa kodi wa America ni za kwao 😁
 
Kumbe mkuu hii ya marekani nayo watu macho yaliwatoka?
Hao ni CCM.
Wana maisha mazuri kuliko raia walipa kodi wa marekani.


Ombaomba mwenyewe ni Tanzania kupitia ccm....hujasikia wanavyomfokea Trump kwa kukata misaada? Walishachukulia hizo hela za walipa kodi wa America ni za kwao 😁
 
Hili swala limenigusa sana, ndio uhalisia wa dunia.

Ninaye mtu ambaye nliamini nikimsaidia naye atanibeba, kusaidia kazi zangu ziende, mambo kwangu yamekuwa magumu kidogo sasa kageukia watu ambao wapo tayari nisifanikiwe.

Lawama ni kila siku.
 
Kariakoo kuna vituko. Alikuja mzee mmoja dukani akiomba vitendea kazi tu (nyundo, msumeno, nk), hataki pesa. Maneno mengiii. Nikampatia. Muda nikahama fremu. Siku akaja tena kasahau alishaomba vifaa dukani. Nikamwambia wewe si ulishakuja pale? Alishituka sana na kuona aibu akaondoka haraka.

Mwingine (kipofu) nikamwona duka moja la plumbing anafanya manunuzi ya maana na maneno mengi. Baada ya muda namuona maeneo ya gerezani, anaombaomba madukani. Mpolee

Mwingine huwa anajifanya akitembea mwili unakakamaa. Anajitupatupa kama mwendawazimu akiwa anaendelea kuomba. Mara utamkuta maeneo mengine anapita utadhani "kapona". Mzima hatetemeki wala kukakamaa
 
Mwanaume mmoja alikuwa akimpa ombaomba $1000 kila mwezi. Alifanya hivyo kwa muda fulani bila kukosa. Siku moja, alimpa ombaomba $750 pekee. Ombaomba alishangaa, lakini akajiambia, "$750 ni bora kuliko kutopata chochote," kisha akaondoka.

Baada ya mwezi mmoja, mwanaume alimpa ombaomba $500 pekee. Ombaomba alishangaa zaidi na kumuuliza, “Ulikuwa unanipa $1000, kisha ikapungua na kuwa $750. Sasa ni $500. Kwa nini? Naweza kujua sababu?”

Mwanaume akamjibu, “Hapo awali, watoto wangu wote walikuwa wadogo na hali yangu ya kifedha ilikuwa nzuri, ndiyo maana nilikuwa nakupa $1000 kila mwezi. Baadaye, binti yangu alikua na akaingia chuo kikuu, na gharama za chuo ziliongezeka, hivyo nikaanza kukupa $750. Sasa, mwanangu wa pili amejiunga na chuo kikuu, gharama zimeongezeka zaidi, ndiyo maana nimekupa $500.”

Ombaomba akamuuliza, “Una watoto wangapi?”

Mwanaume akajibu, “Wanne.”

Ombaomba akamuangalia kisha akasema, “Na unataka niwasomeshe wote kwa pesa zangu?!”

Mara nyingine, watu huchukulia wema na ukarimu kama haki yao badala ya kuona ni fadhila kutoka kwako.
1738924095797.jpg
 
Back
Top Bottom