Strategies for Tanzania's Economic Development


Mkanadara:

Mpaka hapa sina amabacho nigeongezea kwenye maelezo uliyotoa kwa hoja inayoedelea. Nimekuna kichwa nikajiuliza ni mimi sijui maana ya hili azimio la arusha au tunapishana wapi na wengine.

Nimemuelewa Mtanzania, nikisoma post za Kichuguu nazielewa... Zinanipa moyo kuwa kama kimsingi hawa wanaona kama ninavyona may be bado ninalijua Azimio la Arusha ni nini!

Uzuri wa JF tofauti na hizi yingine nilizozipitia kwa kipindihiki cha "mahangaiko ya Mapolisi" ni kuwa michango ni mingi na wakati mwingine ina vina kwelikweli. Ninafurahia JF kwa hilo.

Nafikiri nijipe muda kuangalia na kujifunza kwa undani wachangiaji wengine, nione mitizamo yao, niangalie kwa makini kabisa wanafikiri Azimio la Arusha ni nini. Bahati mbaya kabisa mimi sio mwansiasa kabisa. Na sikumbuki kufindishwa maana ya Azimio la Arusha mahali popote shuleni. Kama walifundisha basi sikuwa msikivu. Labda niliona ni kitu kisichonihusu..na kukiondolea mbali!!

Lakini hivi karibuni imebidi na imetokea nikaamua kufuatia kwa kina na mapana. Nikafikiri nimelielewa. ndio maana nikaona mtizamo inayofanana na ya baadhi ya post hapa, Nikaiona ni ok, Nikajisemea, kama ninawaelewa maoni ya badhi ya wenzangu ..nafikiri niko njiani..lakini nikaona pia kuwa kwa kutoelewa maoni mengine...nijibidiishe kujifunza Azimio la Arusha. Najipa muda!!!

Moyoni ninajua kabisa Kuna jambo ndani ya hili Azimio la Arusha. Na ninafikiri litaibuka wazi hadharani!!!
Sitegemei liwe photocopy ya lile cha 1967.... lakini kwa kuwa huu ni mfumo wa maisha ulio na structure, value na character it can come in any shape and form kutoa majibu muhimu ya ustawi wa maisha.

Na inawezekana maneno haya Azimio la Arusha yanapotosha ..kwani the tool and its system inaweza kuweko kwa ubatizo tofauti tu!! Lakini ikihudumia jamii kwa ufanisi mkubwa. Ni kama neno UMEME lisivyo husiana na KITU CHENYEWE. Na kulibadili neno umeme kwa maneno mengi kwenye nyakati tofauti na hali tofauti isivyo adhiri KITU CHENYEWE! Tutafute kitu chenyewe!
 
Koba,
sasa tunaenda mbele with free market Economy AKA capitalism...low taxes + less regulations + small government = innovations,freedom and prosperity
...

Sielewi haya ulozungumza yanahusiana vipi na hoja hii ya Azimio la Arusha. Zipo nchi za kibepari zenye serikali kubwa (tukianza na Tanzania yenyewe), tax kubwa (Canada), na regulation kibao kwa sababu hawahitaji wawekeshaji toka nje...Tanzania ya leo regulation kibao ndani ya nchi lakini sio kwa wageni...Hii yote ni katika kuhakikisha ng'ombe wote wanaliwa..i

Swala mkuu wangu tuna ngombe wawili, tufanye nini ikiwa leo hii mpango ni kula wote tunaomba msaada kesho. Kupiga madongo Azimio la Arusha hali huna Azimio kabisa ni sawa na Maskini anayelala msikitini akisubiri sala ya Asubuhi...Hayupo hapo kusubiri sala isipokuwa target yake kubwa ni kuomba msaada kwa waumini watakao jitokeza.

Sasa unapozungumzia Capitalism hali huna Azimio la kile unachotaka kujenga na utafanya nini kabla/baada ya hata kukipata ni uchuro mtupu...tutaitana wachawi hadi Kiyama...Ubepari hautafutwi hivyo mkuu, wenzetu wote walianza na Maazimio kama yetu kabla hawajafika hapa walipo. Ujenzi wa nyumba hii Capitalism haukuanza kwa kujenga paa, na tunayoyaona leo na kuyafurahia ktk Ubepari ni matunda ya Maaziomio mazito na kazi ngumu waliyoipitia hawa jamaa zetu...Kumbuka walianza na kodi za vichwa na kushika makoloni zaidi (vita) kuchangia kodi zao kukuza uchumi wa nchi zao...

Leo hii hawa watu wapo zaidi ya millioni 250 na mauzo ya mwaka kwa trillioni ya dollar unataka kulinganisha asilimia ya makusanyo ya kodi zake na Tanzania ati kwa kutumia Capitalism...Mkuu siku zote utajipima koti kwa umbo lako na sio kuiga uwezo wa tembo ktk kushusha kipudu...Utapasuka msamba!

Mkuu wangu hata sisi wengine hapa tulikuwa na mashamba yetu na hayakuchukuliwa hata moja ila yamekuja chukuliwa wakati wa Mkapa walidai upanuzi wa mji na barabara. Hizo habari za wananchi kuchukuliwa mashamba yao nimezisikia hivi karibuni kuliko wakati wowote ule na nakuhakikishia kuwa Azimio la Arusha liliweka msisitizo zaidi ktk kilimo. Kila nyumba (familia) wakati huo walikuwa na shamba somewhere, na hata wafanya kazi serikalini na mashirka ya Umma walilazimika kuwa na mashamba yao binafsi.


Mashamba yaliyochukuliwa na serikali yalikuwa mashamba ya walowezi tena bidhaa za mauzo (cash crops)..Kwa kutazam picha ya mafanikio kwa uchache tu naweza kwambia kuwa pamoja na kidogo walichoweza pata ktk kilimo hicho kila mzazi wetu aliweza jenga nyumba, hata kiwe kibanda. Leo hii nambie mnafanya kazi Benki tena Ofisa lakini huwezi kununua hata kiwanja Kimara juu..sii swala la kukosekana viwanja, hawana uwezo, Lowassa na wenzake wana ma hekalu bila kuzalisha kitu wala kutoka jasho!

Kwa hiyo hizi shutama zako hazina sura kabisa mkuu wangu, labda huko ulikotoka wewe.
 

Mkandara:

Nadhani mada ni mikakati ya maendeleo. Toka tumepata uhuru mikakati ilikuwepo na mingi ilikuwa inapangwa na viongozi na sisi wananchi tulilamishwa kufuata. Na moja ya hayo ni Azimio la Arusha.

Mtu mmoja anakaa mezani na kuandika jinsi nchi itakavyokuwa bila mjadala na bila kuangalia matatizo yatakayotokea iwapo kile anachoandika kitashindwa.

Kuhusu mfano wako wa ng'ombe hauniingii akilini. Je ukila ng'ombe wote na kupata nguvu ya kwenda kuiba ng'ombe wengine kumi kutakuwa na matatizo gani?
 

Bin Maryam,

Ukisoma Azimio, limitation ziko kwenye viongozi ambao walikuwa na upper hand kwa madaraka. There is no where in Azimio ambapo lilizuia ushindani katika jamii zaidi ya Viongozi.

Ndio ni kusadikika kujenga jamii iliyo sawa. Lakini mandhari ya Tanzania wakati tunatangaza Azimio hata leo hii, kuna haja ya kutoa nafasi sawa ili kujenga Taifa imara. Ziwe jitihada binafsi kuwa na nyongeza katika uzalishaji mali.

Mchaga na Mhaya wao walilima mpaka ziada na kuuza kwa majirani. Mgogo na Mzaramo wao walilima kwa kuhemea, kilimo cha kula leo, kesha ajua Mola!

So Azimio was not prohibitive to competition, it was restrictive to the leaders from exploiting the mass. In turn, these leaders decided to use articles meant to them to suppress everyone and this is where Nyerere failed short by allowing viongozi to mis-intepret the Azimio and suppress Juhudi na Maarifa kwa wananchi na kuwa washindani!
 

Hivyo basi si azimio au sera za ujamaa zilikuwa ni mbovu, bali ni watu na tabia zao (tamaduni) kama ulivyosema hapo juu, kukimbilia ujima badala ya kukabili hali halisi na kuchangia gharama.

Nakumbuka jinsi Serikali ilipoleta mambo ya wananchi kuchangia elimu na afya, kila mtu hata wale wenye uwezo walilalamika kuwa hawawezi kulipia na kukimbilia ujima.

Tunahitaji mfumo wa kulazimisha watu wawe wanajenga jitihada na ikiwezekana basi extreme measures zitumike mfano kuacha wadorore na kuteketea!
 

Koba,

Lets say we stop asking for Azimio, what economic policies and strategies do you think will make Tanzania improve economically and financially? Do the FME policies you are advocating working for us? if they do how? if they are not how and what are the alternatives?

What are the social policies that are currently pushing and unifying Wananchi to be more productive and innovative if we keep Azimio on back burner?

Let us for a minute stop criticising Azimio as failure and cause of complete collapse of Uzalishaji mali and hear from you opponents of Azimio your Social Economical programs and mechanism that can revamp Uchumi and start fighting Umasikini.
 

Bin Maryam,

Okay you are right on this one. What do you propose? what is your plan? i think it is time that we hear from you solutions and plans rather than constant criticism on Azimio and Nyerere failures!
 
introducing a policy like China where by no foreign company can own a business in China, companies must form a joint venture with a local company if they want to do business there, the can own no more than 50% of any shares in a company. Kama hawataki basi yaache madini na maliasili zetu zibaki huko ardhini. We have something they need and now its about time Tanzanians to use that as a bargaining chip. (no more excuses of sijui oooh kulikuwa na ukame ....in order to get us in these shady business deals)
 
Jaribuni kufanya bishara TZ ndio mtagundua ninachoongea kuhusu hizo regulations & taxes ambazo ni product ya siasa zetu.

Nakuhakikishia bila dirty tricks & corruptions utafunga biashara the next day, na kumbe kitu gani msichoelewa kuhusu small government huku nyie ndio wapiga kelele wakubwa wa baraza la Jk la mawaziri 60 wengi wao hawana akili na VXs zaidi ya 10000 za serikali...wewe tupatie low taxes + less stupid regulations then utaona jinsi watu watakavyofanya kazi kwa bidii.

Na wewe Mkandara hizo nchi zinazochukua Tax kubwa at least hiyo Tax inaonekana inaenda wapi,Germany wanachukua 40% lakini Elimu bure mpaka University, health care is almost free na infrastructure ziko tight, wabongo wanachukua wanaenda kuongeza VX za serikali sasa hapo wapi na wapi.
 

Mkuu sana Invincible,
Kabla ya kusoma mchango wako, nilikuwa najiandaa kuandika mkakati ambao mie ningeupendekeza. Lakini baada ya kusoma wako imekuwa kama umesoma wazo langu kuu siku zote.

NAKUUNGA MKONO KWA 100%
 
Mkandara:

Kuhusu mfano wako wa ng'ombe hauniingii akilini. Je ukila ng'ombe wote na kupata nguvu ya kwenda kuiba ng'ombe wengine kumi kutakuwa na matatizo gani?

Bin Maryam;

Mfano ulikuwa unasiamia kuonyesha two aspects za development. Kuwa; Unahitaji kitu cha kwanza cha kuanzia "starter" kama hatua ya kwanza na hatua ya pili ni “jasho”, jitihada, maarifa na good manegement kufanya the stater kuwa expected product.

Kuwa na mental set up inayo kuelekeza kwa makusudi ku extinguish starter.... na kuwala Ngombe wawili... Kwa kuwa Utawaiba wengine ni tatizo la kiutu. Pili wizi huo si chelei kuuita ni kukiukwa kwa moral values.

Hatuwezi kutafuta maendeleo kwa udi na uvumba yaani hata ikibidi kuvunja maadili na haki za kibinaadamu.

Set up ya azimio la arusha ilikuwa imetake care all those measures. Yaani maadii ya utu na hatimaye ya uongozi katika kujenga uchumi. Usingekaa na kufikiri kula mavuno yote ya msimu huu simply ulikuwa na uwezo wa Kuiba mbegu za mahindi kwa jirani. Au tuseme kwa kuwa unauwezo wa kuiba ng’ombe wengine.

Mitizamo kama hiyo ikiachiwa ndio inatupelekea hapa tulipo. Kila kiongozi anaona ni rahisi na sawa tu kuiba ili kukuza mtaji wake. Miiko ya maadili na usawa katika utu amabayo ni nguzo kuu ya azimio la Arusha vilihakikisha hilo halitokei katika harakati za kujenga maendeleo ya jamii. Na leo jamii inadai maadili hayo kwa kasi ya ajabu. Hata bunge lililokuwa limelala sasa limepata pa kuibukia.

You know what?

"Mind set ya maadili na utu" vilivyokuwa vinajengwa kwenye azimio la arusha kwa kumfunza mtu uvumilivu na subira ya kutokula ”Ngombe” wawili wa mwisho, pamoja na maumivu na kuhitaji kujitolea kwa dhati ili kuyaweza..lakini ndio msingi wa kumtofautisha binadamu na mnyama. Na imegundulika kuwa are the same “social forces” zinazodaiwa na ugonjwa wa ukimwi ili kupunguza maambukizi na kurefusha maisha ya mgonjwa.

Ukimwi kama natural social force inamdai mwanadamu utu, ubinadamu, uwezo wa kujinyima, kuvumilia, subira etc ili kunusuru taifa kuteketea. Cha ajabu? Hizo ndizo nguvu ndani ya azimio la Arusha ambazo zinakimbiwa na wengi. But tutakimbiaje ukimwi/Magonjwa yanayodai traits za azimio la Arusha kama social remedy? Ni kupitia uchumi na mtindo wa maisha uliosimamia maadili ya utu na uliotandaa kwa kila familia utakaoweza kuzuia sehemu ya maambukizo mapya. Nani haoni hilo? Na hapa kwetu njia iliyotandaa kwenye kila familia ambayo unaweza kujegea uchumi wa aina hiyo ni “KILIMO” kama ilivyoainishwa kwnye Azimio la Arusha.


Hatuwezi kuua utu na maadali yake ili kujenga uchumi maana tukifika angaza kabla ya kupewa dawa za kurefusha maisha wanatudai tujifunze kutokuiba mali au “watu”, tuwe na utu tusiambukize wenzetu, tudumishe maadili ya kifamlia, maadili ya kazi, uongozi na maadii katika kujenga uchumi. Kwa hiyo leo dawa zinatudai utu ili zifanye kazi yake. Sasa itakuwaje Uchumi usiojali, usawa na utu kwanza? Wenye nacho siwatawaambukiza wasio kuwa nacho na kutekeketeza Taifa?

Kama una "jicho" sahihi ona Angaza wanacho advocate. Ni basic traits au componets mihumu ndani ya azimio la Arusha.
 
..Maoni ya Jenerali Ulimwengu kuhusu yaliyojiri wakati wa Azimio la Arusha na siasa za Ujamaa.

 
I believe in Education nothing else,
Maana strategies must be configured in hierarchical model with full of protocals.
kama huna wasomi hizo protocal hawatazielewa wala kuzifuata na hatima yake the failure of whole system.
Mkamap, education bila uzalendo wa hao wasomi hauna maana yoyote.... academicians na wengineo mbalimbali tulionao ndani ya Taifa letu wangetosha kabisa kulisukuma Taifa letu a 2 step ahead. Tunachokosa kwa wasomi wetu ni uzalendo.
 
Game Theory,

Naomba maoni yako kuhusu nguvu na tofauti kati y Cash economy na Credit economy.
 
Hivi tukibadilisha mfumo wa malipo ya mishahara Tanzania mathalani kuwa lipa watu mara mbili kwa mwezi badala ya mara mmoja kunaweza kutusaidia kuongeza ufanisi na kupunguza rushwa?
 
Rev. Kishoka,
haya matatizo ya Marekani kama yangekuwa Bongo tunaweza kutoka kweli?....
Duh, sijui Koba atasema nini kuhusiana na Ubepari maanake uliubebea bango bila kufahamu kwamba Ubepari nao una nyufa mbaya sana ambazo nchi kama Tanzania ikija shikwa na matatizo kama hayo ndio kitakuwa kifo cha nyani!...

Bin Mayram,
Mkuu hivi kweli unafikiria kula ng'ombe wako ili upate nguvu ya kwenda kuiba ng'ombe wa mtu mwingine... mtu mwenyewe unayemkusudia kumwibia nani?... Mmasai na pinde zake!
 
Hivi tukibadilisha mfumo wa malipo ya mishahara Tanzania mathalani kuwa lipa watu mara mbili kwa mwezi badala ya mara mmoja kunaweza kutusaidia kuongeza ufanisi na kupunguza rushwa?

Rev., tukifanikisha hilo katika sekta binafsi basi hata mfumo wa malipo kwa saa nao utawezekana. Isitoshe, takwimu zinaonesha kuwa sekta binafsi tanzania ndiyo mwajiri mkubwa kuliko zote (sorry no ref.)
 
well, Steve unajua umeileta hii thread nilishaisahau

anyway nitarudi kuchangia baada ya muda
 
nadhani kabla ya yote tunahitaji institution reforms.

hayo mengine yanafuata hapo
 
Mkamap, education bila uzalendo wa hao wasomi hauna maana yoyote.... academicians na wengineo mbalimbali tulionao ndani ya Taifa letu wangetosha kabisa kulisukuma Taifa letu a 2 step ahead. Tunachokosa kwa wasomi wetu ni uzalendo.

Wasomi wetu wana uzalendo mkubwa sana! Kama wasingekuwa Wazalendo, wasingeshinda ndani ya JF wakijadili mustakabali wa taifa letu!

Tatizo kubwa ni wanasiasa wetu ambao wengi wao, nachelea kusema kwamba, si wasomi! Siasa zetu zimejaa watu wababaishaji huku wasomi wengi wakijiengua kutoka kwenye siasa na kufanya kazi zao zingine za kitalaamu zaidi, ndani na nje ya nchi!

Siasa zimeachiwa watu ambao wanafanya kazi kwa kujipendekeza kwa wakubwa, baadhi yao ni washirikina wakubwa, na hivyo kuwatisha watu wengine ambao wana njia za kujikimu na kuendesha familia zao pasipo mambo yanayofanana na hayo!

Hebu niambie, uzalendo gani unahitajika kumhudumia mgonjwa pale Muhimbili huku ukiwa huna gloves, wala vitendea kazi vingine, wakati misafara ya viongozi wa nchi inaandamana na kuchoma mafuta ya serikali kila siku bila sababu za msingi?

Ni nani atakuwa mzalendo wa kujitoa kufundisha wanafunzi 400 ndani ya madarasa mawili, halafu mshahara wake unacheleweshwa kwa miezi zaidi ya 7?

Ni askari gani ambaye anaweza kuwa mzalendo kiasi cha kutosha kulinda usalama wa raia wakati mshahara wake ni mdogo, na anaishi kwenye nyumba ya mabati kuanzia chini mpala juu!!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…