Suala la Mbunge Mpina kuthibitisha tuhuma za ukiukwaji wa uagizaji Sukari nje ya nchi, limethibitisha udhaifu wa Bunge letu

Suala la Mbunge Mpina kuthibitisha tuhuma za ukiukwaji wa uagizaji Sukari nje ya nchi, limethibitisha udhaifu wa Bunge letu

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
luhaga-mpinaa-jpg.3017557
Mbunge Luhaga Mpina amethibitisha mbele ya waandishi wa. habari kuwa kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa sheria katika uagizaji Sukari nje ya nchi, wakati Taifa letu lilipokumbwa na uhaba mkubwa wa Sukari, miezi michache iliyopita.

Akiongea mbele ya waandishi wa habari, alisema kuwa ana uthibitisho kuwa hata mmiliki wa stationery, alipewa kibali Cha kuagiza Sukari nje ya nchi!

Hata hivyo kitu Cha ajabu sana ni hiki kilichotokea Bungeni Jana, Kwa Spika wa Bunge, Tulia Ackson kuamuru Mbunge huyo, Luhaga Mpina, aburuzwe Kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, eti Kwa kumdharau yeye Spika wa Bunge, Kwa kutomletea yeye ushahidi huo na badala yake kuupeleka Kwenye vyombo vya habari!

Tunafahamu kuwa vyombo vya habari ni mhimili wa 4 wa Dola, ambao unapaswa kufichua uovu wote unaofanyika hapa nchini.

Wananchi wote wa nchi hii, tunapaswa kusimama na Mbunge Luhaga. Mpina, Kwa kuwa inaonekana dhahori kuwa huyu Spika Tulia Ackson, anataka kuligeuza Bunge letu, kuws ni sehemu ya kuwalinda wale wanaovunja sheria za nchi hii.

Hivi kosa la Mbunge Luhaga Mpina, ni lipi hasa, hadi aburuzwe Kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge??

Hili Bunge letu, limezidi kuthibitisha udhaifu wake, ambao sisi wananchi tumekuwa tunauona Kwa kipindi kirefu sasa.

Pia soma:
 
Ajabu zaidi ni kwamba Mpina alisema […] nimempelekea mheshimiwa speaker ushadihidi huu…
Na ndipo akaanza kusoma alichowasilisha…
Kwa maana Nyingine, mahakama ikisema siku fulani ni siku ya kuleta nyaraka au ushahidi na wewe ukatangaza utakacho au ulicho washirisha tayari ni kumkosea Adabu hakimu… ?
Ndio maana huwa napenda sana kujua waalimu wa wanasheria wetu ni Nani walikuwa mwalimu wao? Ni taabu tupu huko kichwani Kwa wanafunzi wao Kama Mh. Speaker…

Kwa kumpeleka Mpina huko maadili, wabunge wanaelekea kujisahau kwamba ni wa wabanchi, lakini wao wanahangaika kujionyesha ni wa serikali…
Mpina anaibana serikali ili ijieleze Kwa wananchi Kama alivyotumwa na wananchi walio mtuma pale.
Bado serikali haijatoa majibu, Mara paap tunasikia… umenikosea adabu mimi…
Hivi wabunge ni watoto wa speaker na mama speaker lazima aheshimiwe kwanza?
Huyu speaker ni muwakilishi wa wananchi au serikali?
Wabunge na speaker - acheni sarakasi- wananchi tunawaona mnacho mtendea huyo mpina kupitia speaker wa serikali…
Tunataka kuona mkifanya kazi ya wananchi, sio serikali…
 
Ajabu zaidi ni kwamba Mpina alisema […] nimempelekea mheshimiwa speaker ushadihidi huu…
Na ndipo akaanza kusoma alichowasilisha…
Kwa maana Nyingine, mahakama ikisema siku fulani ni siku ya kuleta nyaraka au ushahidi na wewe ukatangaza utakacho au ulicho washirisha tayari ni kumkosea Adabu hakimu… ?
Ndio maana huwa napenda sana kujua waalimu wa wanasheria wetu ni Nani walikuwa mwalimu wao? Ni taabu tupu huko kichwani Kwa wanafunzi wao Kama Mh. Speaker…

Kwa kumpeleka Mpina huko maadili, wabunge wanaelekea kujisahau kwamba ni wa wabanchi, lakini wao wanahangaika kujionyesha ni wa serikali…
Mpina anaibana serikali ili ijieleze Kwa wananchi Kama alivyotumwa na wananchi walio mtuma pale.
Bado serikali haijatoa majibu, Mara paap tunasikia… umenikosea adabu mimi…
Hivi wabunge ni watoto wa speaker na mama speaker lazima aheshimiwe kwanza?
Huyu speaker ni muwakilishi wa wananchi au serikali?
Wabunge na speaker - acheni sarakasi- wananchi tunawaona mnacho mtendea huyo mpina kupitia speaker wa serikali…
Tunataka kuona mkifanya kazi ya wananchi, sio serikali…
Ni ajabu na kweli!

Mbunge anafichua maovu nchini, Spika wa Bunge anadai kuwa amepuuzwa, Kwa hiyo anatakiwa apelekwe Kwenye Kamati ya Haki, Maadoli na madaraka ya Bunge, Ili awajibishwe!
 
Ni ajabu na kweli!

Mbunge anafichua maovu nchini, Spika wa Bunge anadai kuwa amepuuzwa, Kwa hiyo anatakiwa apelekwe Kwenye Kamati ya Haki, Maadoli na madaraka ya Bunge, Ili awajibishwe!
Speaker huyu ametoa maamuzi beyond the scope of her authority. Mambo ya nje ya Bunge yana sheria zake na alichosema Mpina, hakukisema ndani ya Bunge. Yafaa sasa huyu Raisi ya Mabunge duniani ajiuzuru maana anatutia aibu sana kwa uelewa wake wa sheria. Ya bungeni, ushahidi tayari katoa. Ya nje ya bunge, yale ni maoni yake binafsi kama raia wengine humu mtandaoni. Speaker ajisahihishe na aachane na Mpina kwa sasa. Joho limempwaya tayari
 
Speaker huyu ametoa maamuzi beyond the scope of her authority. Mambo ya nje ya Bunge yana sheria zake na alichosema Mpina, hakukisema ndani ya Bunge. Yafaa sasa huyu Raisi ya Mabunge duniani ajiuzuru maana anatutia aibu sana kwa uelewa wake wa sheria. Ya bungeni, ushahidi tayari katoa. Ya nje ya bunge, yale ni maoni yake binafsi kama raia wengine humu mtandaoni. Speaker ajisahihishe na aachane na Mpina kwa sasa. Joho limempwaya tayari
Huyu Spika Tulia Ackson, Kwa uwezo wake, hastahili kuwa hata Mwenyekiti wa serikali ya mtaa!😎
 
Back
Top Bottom