Suala la mtaala ulioboreshwa lisifanyiwe mzaha

Suala la mtaala ulioboreshwa lisifanyiwe mzaha

Luhungu

JF-Expert Member
Joined
Sep 5, 2013
Posts
817
Reaction score
237
Shule zimefunguliwa takribani siku Nne Hadi Sasa na kwa uhakika wanafunzi wa Kidato Cha kwanza Wana miminika mashuleni.

Uhakika uliopo ni kuwa wote wanakuja kuanza mtaala ulioboresha (alimaarufu mtaala mpay)

Pasipo kupinga mtaala ulioboreshwa umelenga kupunguza changamoto za mwanafunzi kuhitimu akiwa hana cha kuonyesha katika uhalisia huko mtaani katika maisha ya kawaida. Serikali naipongeza.

Changamoto yangu ni namna maandalizi yalivyo na namna uwazi na utekelezaji wake unavyo kwenda kuwa.

Ukitazama kwa umakini utangundua hata walimu watakao tekeleza mtaala huu, wengi wao ni Kama wanasubri nani afanye, maana hata wao hawaamini Kama ndo mtaala umeeanza.

1. Hakuna mafunzo stahiki
2. Ushirikishwaji ni mdogo na ama haupo kwa baadhi ya maeneo na
3. Utayari wa Walimu ni kama hawako tayari japo kwao tamko ni agizo.

Nashauri namna Bora na ya haraka ifanyike ikiwemo,
1. Uzalishaji/usambazaji wa vitabu na vitendea kazi stahiki
2. Semina wezeshi hasa katika kuliendea na utekelezaji wa jambo hili.
3. Vipindi elekezi vya radio, tv na namna nyingine ambayo itawapa Wazazi uelewa wa mapema dhidi ya kile Watoto wao wanacho kiendea.

Mwisho, Elimu ni Silaha, isitumiwe vibaya maana Taifa litaangamia.
 
Screenshot_20250112-141523_1.jpg
 
Sio tu sekondari, hata primary school walimu wanatumia simu( Notes za online) Hakuna vitabu, hasa darasa la nne.. wiki la kwanza linaisha.
 
Sio tu sekondari, hata primary school walimu wanatumia simu( Notes za online) Hakuna vitabu, hasa darasa la nne.. wiki la kwanza linaisha.
Wenzetu Kenya, wameongeza darasa, kutoka madarasa nane shule ya msingi, sasa ni tisa shule ya msingi, nahuu mwaka hakuna kidato Cha kwanza, mpaka mwa ujao
 
Kama mmerushiwa contents online shida nini..
Wakati mnasubiri hard copies tumieni mliyonayo ktk cm zenu
 
Wenzetu Kenya, wameongeza darasa, kutoka madarasa nane shule ya msingi, sasa ni tisa shule ya msingi, nahuu mwaka hakuna kidato Cha kwanza, mpaka mwa ujao
Ni sahihi, ila mtaala wetu ulioboreshwa ni mzuri sana mkuu, unawaandaa vijana kujitegemea baada ya kuhitimu.
Shida ni moja tu hapa Tz , utekelezaji utakuwa wa kisiasa..
 
Shule zimefunguliwa takribani siku Nne Hadi Sasa na kwa uhakika wanafunzi wa Kidato Cha kwanza Wana miminika mashuleni.

Uhakika uliopo ni kuwa wote wanakuja kuanza mtaala ulioboresha (alimaarufu mtaala mpay)

Pasipo kupinga mtaala ulioboreshwa umelenga kupunguza changamoto za mwanafunzi kuhitimu akiwa hana cha kuonyesha katika uhalisia huko mtaani katika maisha ya kawaida. Serikali naipongeza.

Changamoto yangu ni namna maandalizi yalivyo na namna uwazi na utekelezaji wake unavyo kwenda kuwa.

Ukitazama kwa umakini utangundua hata walimu watakao tekeleza mtaala huu, wengi wao ni Kama wanasubri nani afanye, maana hata wao hawaamini Kama ndo mtaala umeeanza.

1. Hakuna mafunzo stahiki
2. Ushirikishwaji ni mdogo na ama haupo kwa baadhi ya maeneo na
3. Utayari wa Walimu ni kama hawako tayari japo kwao tamko ni agizo.

Nashauri namna Bora na ya haraka ifanyike ikiwemo,
1. Uzalishaji/usambazaji wa vitabu na vitendea kazi stahiki
2. Semina wezeshi hasa katika kuliendea na utekelezaji wa jambo hili.
3. Vipindi elekezi vya radio, tv na namna nyingine ambayo itawapa Wazazi uelewa wa mapema dhidi ya kile Watoto wao wanacho kiendea.

Mwisho, Elimu ni Silaha, isitumiwe vibaya maana Taifa litaangamia.
Mtaala ulioboresha kwani una wahusu na hao wa sekondari sio kuanza la nne wanaoishia la Sita
 
Back
Top Bottom