OLS
JF-Expert Member
- Oct 12, 2019
- 426
- 685
Kwa kipindi sasa raia wamekuwa wakilalamikia bei ya sukari kupaa na utetezi mbalimbali ukittoka kuhusu sababu ya kupaa kwa bei hiyo. Sababu ikitolewa kuwa ni mwezi wa ramadhani au kufungwa kwa viwanda. Vyovyote vile lakini imeshaonekana kuwa tunahitaji sukari kwa kipindi hiki na hivyo tunapaswa kuingiza sukari kutoka nje.
Serikali ilisema imeagiza tani 40,000 za sukari na ilishanza kupakuliwa, na ingeweza kuingia mitaani tangu Aprili 17 kwa ripoti za mamlaka zilizotolewa mwanzo. Nahisi kuna changamoto kwenye namna sukari hiyo inawafikia walaji, ndio sababu bado bei elekezi inalalamikiwa kutofuatwa maeneo mengi.
Nguvu ya soko ina maajabu yake, na ukitumia nguvu za kimamlaka kudhibiti nguvu ya soko, biashara haramu ‘black market; huwa ni matokeo. Kama baadhi ya watu waliolalama kuuziwa sukari na watu wanaowajua tu. Kuwakamata au kuwafutia leseni wafanyabiashara bado hakutashusha bei.
Ipo haja ya kuona kuwa kwa kipindi hiki tatizo la sukari lipo kwenye uzalishaji wake ‘Supply’, ambayo hii inaweza kuongezwa kwa kuruhusu sukari kutoka nje kwa kuangalia upya masharti ya uagizaji wa sukari. Upande wa uhitaji ni huwa unadhibitiwa zaidi na bei.
Hivyo basi ipo haja ya kuona sukari inaingia kwa wingi nchini na bei itashuka. Sukari isiingie kwa namba tu, bali iingie kwa uhakika, maana ni swala la kufikirika kuwa na tani 40,000 za sukari halafu bado sukari adimu.
Wala tusidhani kuwa kuna watu wanaficha sukari ndani mwao, na hata kama wanaficha sukari ikiwa nyingi hiyo wanayoificha itawadodea, kibiashara ufichaji wa bidhaa unaweza kufanyika iwapo bidhaa inaanza kuwa adimu, Bidhaa ikipatikana kwa wingi ni ngumu mtu kuihodhi.
Signed
OEDIPUS
Serikali ilisema imeagiza tani 40,000 za sukari na ilishanza kupakuliwa, na ingeweza kuingia mitaani tangu Aprili 17 kwa ripoti za mamlaka zilizotolewa mwanzo. Nahisi kuna changamoto kwenye namna sukari hiyo inawafikia walaji, ndio sababu bado bei elekezi inalalamikiwa kutofuatwa maeneo mengi.
Nguvu ya soko ina maajabu yake, na ukitumia nguvu za kimamlaka kudhibiti nguvu ya soko, biashara haramu ‘black market; huwa ni matokeo. Kama baadhi ya watu waliolalama kuuziwa sukari na watu wanaowajua tu. Kuwakamata au kuwafutia leseni wafanyabiashara bado hakutashusha bei.
Ipo haja ya kuona kuwa kwa kipindi hiki tatizo la sukari lipo kwenye uzalishaji wake ‘Supply’, ambayo hii inaweza kuongezwa kwa kuruhusu sukari kutoka nje kwa kuangalia upya masharti ya uagizaji wa sukari. Upande wa uhitaji ni huwa unadhibitiwa zaidi na bei.
Hivyo basi ipo haja ya kuona sukari inaingia kwa wingi nchini na bei itashuka. Sukari isiingie kwa namba tu, bali iingie kwa uhakika, maana ni swala la kufikirika kuwa na tani 40,000 za sukari halafu bado sukari adimu.
Wala tusidhani kuwa kuna watu wanaficha sukari ndani mwao, na hata kama wanaficha sukari ikiwa nyingi hiyo wanayoificha itawadodea, kibiashara ufichaji wa bidhaa unaweza kufanyika iwapo bidhaa inaanza kuwa adimu, Bidhaa ikipatikana kwa wingi ni ngumu mtu kuihodhi.
Signed
OEDIPUS