Suluhisho la wamachinga halina wala halijawahi kuwa na uhalisia hapa nchini! Tuache kujidanganya

Suluhisho la wamachinga halina wala halijawahi kuwa na uhalisia hapa nchini! Tuache kujidanganya

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
1,968
Reaction score
2,957
Kundi la vijana wasio na ajira rasmi linaongezeka kwa kasi kubwa sana, kila kukicha wanakuwa wengi leo kuliko jana.

Mzee kikwete alikuja na ufumbuzi eti wa kujenga machinga complex ambayo matokeo yake haijapunguza tatizo hata tone moja.

Namuona rais wa sasa anajaribu kupitia njia ileile eti kujenga soko, ukweli ni kwamba hata ungejenga soko la kuchukua machinga milioni moja sioni kama unaweza kumaliza changamoto ya machinga.

Badala ya kuhangaika na machinga huku mitaani nakushauri serikali kama ipo serious na swala la machinga basi wawekeze nguvu nyingi sana huko wanakotokea hawa vijana. Yaani wawekeze zaidi kwenye kilimo ili kivutie vijana lakini pia wabadili elimu ili ilenge kuzalisha wazalishaji!
 
Ukiboresha kilimo viwanda vitaongezeka ajira zitaongezeka machinga na bodaboda mijini watapungua.

Ongezeko la machinga na bodaboda mijini ni kushindwa kwa serikali ya CCM kuhusu uchumi na ajira nchini yaani imeshindwa kuzitumia fursa za raslimali tele zilizojaa zizalishe ajira.

Raslimali zinaoza hazitumiki ni asilimia 20 tu ndo zinatumika,zingetumika angalau asilimia 70 tu Hakuna mtu asingekuwa na ajira ya kufanya nchini.
 
Nani kakwambia machinga anataka ghorofa case study machinga complex ghorofa ni kwa ajili ya hostel hawa ndo wanataka ghorofa.

Machinga complex ingegeuzwa hostel ingerudisha pesa kitambo.

Machinga anaendana na stand.

Tatizo kubwa la watunga sera wa nchi hii awawashirikishi wahusika sisi walipa kodi tunaletewa sera zilizotungwa na wakaa ofisi kwenye viyoyozi thus sera zao zikingia field zinabuma.

Hata vipaumbele vya nchi walipa kodi wangeshirikishwa tusingekuwa masikini.

Machinga na ghorofa wapi na wapi.

Ni bora stand zote ziboreshwe na waweke sehemu za machinga.Hayo masoko ya ghorofa yatajaa chini labda na ghorofa ya kwanza tu.

Tija ni kuboresha kilimo jenga vyuo vya ujuzi kila kata na sio kurundika vyuo vikuu vingi visivyo tija sasa mtu unasoma hadi masters then unaenda kuwa machinga au bodaboda hio miaka 20 uliyoipoteza shuleni vipi kama ungeifanya Kazi hio miaka 20 iliyopita si ungekuwa mbali.

Kuwa na vyuo vikuu vingi katika nchi ni kuongeza idadi ya masikini nchini huku kodi zetu zikipotea maana mikopo waliyopewa Ili kusoma ndo ishapotea eti hadi mtu apate ajira ndo alipe asipopata imepotea hio.
 
Ukiboresha kilimo viwanda vitaongezeka ajira zitaongezeka machinga na bodaboda mijini watapungua.

Ongezeko la machinga na bodaboda mijini ni kushindwa kwa serikali ya CCM kuhusu uchumi na ajira nchini yaani imeshindwa kuzitumia fursa za raslimali tele zilizojaa zizalishe ajira.

Raslimali zinaoza hazitumiki ni asilimia 20 tu ndo zinatumika,zingetumika angalau asilimia 70 tu Hakuna mtu asingekuwa na ajira ya kufanya nchini.
Pesa iliotumiwa na Magufuli na inayotumiwa na Samia kupambana na upinzani inatosha kujenga mashule, mahospitali, vituo vya afya na kuajiri vijana wengi na tatizo la machinga lingepungua kwa kiasi kikubwa. Tunachoshudia ni mihemko, si mipango ya kutatua matatizo na kuleta maendeleo.
 
Nani kakwambia machinga anataka ghorofa case study machinga complex ghorofa ni kwa ajili ya hostel hawa ndo wanataka ghorofa.

Machinga complex ingegeuzwa hostel ingerudisha pesa kitambo.

Machinga anaendana na stand.

Tatizo kubwa la watunga sera wa nchi hii awawashirikishi wahusika sisi walipa kodi tunaletewa sera zilizotungwa na wakaa ofisi kwenye viyoyozi thus sera zao zikingia field zinabuma.

Hata vipaumbele vya nchi walipa kodi wangeshirikishwa tusingekuwa masikini.

Machinga na ghorofa wapi na wapi.

Ni bora stand zote ziboreshwe na waweke sehemu za machinga.Hayo masoko ya ghorofa yatajaa chini labda na ghorofa ya kwanza tu.

Tija ni kuboresha kilimo jenga vyuo vya ujuzi kila kata na sio kurundika vyuo vikuu vingi visivyo tija sasa mtu unasoma hadi masters then unaenda kuwa machinga au bodaboda hio miaka 20 uliyoipoteza shuleni vipi kama ungeifanya Kazi hio miaka 20 iliyopita si ungekuwa mbali.

Kuwa na vyuo vikuu vingi katika nchi ni kuongeza idadi ya masikini nchini huku kodi zetu zikipotea maana mikopo waliyopewa Ili kusoma ndo ishapotea eti hadi mtu apate ajira ndo alipe asipopata imepotea hio.
Ni ukweli kwamba nchi hii ina mambo mengine yanatia uchungu sana, kilimo kimekua mhimili wa uchumi wa nchi yetu kwa namna kama tatu hivi kinaongoza kuajiri watu wetu, ni chanzo muhimu cha fedha za kigeni, ndio chanzo cha cha kula karibia chote tunachokula hapa nchini, kinatuzalishia malighafi za viwanda, kinautambulisha nchi na kuiletea fedha za kigeni.
Kutokana na ukweli huo nilidhani kwa makusudi kabisa serikali ingewekeza sana kwenye elimu na teknolojia ya kilimo!!
 
Nani kakwambia machinga anataka ghorofa case study machinga complex ghorofa ni kwa ajili ya hostel hawa ndo wanataka ghorofa.

Machinga complex ingegeuzwa hostel ingerudisha pesa kitambo.

Machinga anaendana na stand.

Tatizo kubwa la watunga sera wa nchi hii awawashirikishi wahusika sisi walipa kodi tunaletewa sera zilizotungwa na wakaa ofisi kwenye viyoyozi thus sera zao zikingia field zinabuma.

Hata vipaumbele vya nchi walipa kodi wangeshirikishwa tusingekuwa masikini.

Machinga na ghorofa wapi na wapi.

Ni bora stand zote ziboreshwe na waweke sehemu za machinga.Hayo masoko ya ghorofa yatajaa chini labda na ghorofa ya kwanza tu.

Tija ni kuboresha kilimo jenga vyuo vya ujuzi kila kata na sio kurundika vyuo vikuu vingi visivyo tija sasa mtu unasoma hadi masters then unaenda kuwa machinga au bodaboda hio miaka 20 uliyoipoteza shuleni vipi kama ungeifanya Kazi hio miaka 20 iliyopita si ungekuwa mbali.

Kuwa na vyuo vikuu vingi katika nchi ni kuongeza idadi ya masikini nchini huku kodi zetu zikipotea maana mikopo waliyopewa Ili kusoma ndo ishapotea eti hadi mtu apate ajira ndo alipe asipopata imepotea hio.
Hahahah hata mimi huwa nashangaa yani eti soko lina floor 7 kama benki? Hamnaga huo uphala! Huko floor ya 7 nani atakaa? Nani atapanda kufata nyanya floor ya 7 wakati zipo floor ya kwanza!

Ghorofa lililofanikiwa ni Mobile Plaza tu ile iliokuwa ikiitwa china plaza awali!
 
Hahahah hata mimi huwa nashangaa yani eti soko lina floor 7 kama benki? Hamnaga huo uphala! Huko floor ya 7 nani atakaa? Nani atapanda kufata nyanya floor ya 7 wakati zipo floor ya kwanza!

Ghorofa lililofanikiwa ni Mobile Plaza tu ile iliokuwa ikiitwa china plaza awali!
Yaani iko haja ya kuitisha mijadala mahususi kuhusiana na huu utani na mzaha ambao watu tuliowapa dhamana wanatufanyia Hawa wanaamua kuhujumu maisha yetu kwa makusudi maana takwimu ziliwahi kusema zamani kila mwaka vijana takribani laki 8 wanaingia kwenye soko la ajira na mifumo yetu yote ya ajira rasmi inaajiri watu wasiozidi laki 2 kwa nini usitake kuumiza kichwa kwaajili ya Hawa laki 6,7,8, Hadi 9 wanaoingia mitaani kila mwaka!?.
Na kwa kuwa Mungu katupendelea ardhi bahari misitu maziwa mito nk ni kwa nini serikali haiwekezi fedha za kutosha huko ili hayo maeneo yaajiri walau nusu ya vijana wetu!!
 
Kama Taifa tunasafari ndefu isiyo na matumaini kusimama na kuwa imara ,inasikitisha sana wasomi wetu ndio watungaji wa hizi sera na mikakati inayo tudidimiza na iliyo tufikisha hapa tulipo.
 
MACHINGA NI KAMA WAMELAZIMISHWA KWENDA LIKIZO.....night duty....
 
Kama Taifa tunasafari ndefu isiyo na matumaini kusimama na kuwa imara ,inasikitisha sana wasomi wetu ndio watungaji wa hizi sera na mikakati inayo tudidimiza na iliyo tufikisha hapa tulipo.
Ukweli inaumiza sana kwa sababu Hali iko wazi wala si ya kificho lakini inavyoonekana watu wanatafuta majibu mepesi kwa maswali magumu ila nitoe tu angalizo kwamba kama serikali haitabadili chochote kwa huu mwenendo wa sasa basi tutarajie misukosuko mikubwa sana huko mbele
 
Hahahah hata mimi huwa nashangaa yani eti soko lina floor 7 kama benki? Hamnaga huo uphala! Huko floor ya 7 nani atakaa? Nani atapanda kufata nyanya floor ya 7 wakati zipo floor ya kwanza!

Ghorofa lililofanikiwa ni Mobile Plaza tu ile iliokuwa ikiitwa china plaza awali!
Machinga na stand ni sawa na kuku na yai.Serikali ibomoe nyumba za nyuma ya stand zote ipate open space kwa ajili ya masoko ya machinga na open market,kisha machinga wapangwe walipe elf 50 kwa mwaka jumla ya machinga milioni 5 wote itapata tilioni 2.5 kwa mwaka kama kodi.Hizi pesa zipelekwe kujenga miundombinu ya umwagaliaji ili kupunguza idadi ya machinga na bodaboda mijini waende wakazalishe mashambani tuuze mazao China na sio kuwaacha machinga na bodaboda kuwa madalali wa kuuza bidhaa za China ili kukuza uchumi wa China.
 
Ni ukweli kwamba nchi hii ina mambo mengine yanatia uchungu sana, kilimo kimekua mhimili wa uchumi wa nchi yetu kwa namna kama tatu hivi kinaongoza kuajiri watu wetu, ni chanzo muhimu cha fedha za kigeni, ndio chanzo cha cha kula karibia chote tunachokula hapa nchini, kinatuzalishia malighafi za viwanda, kinautambulisha nchi na kuiletea fedha za kigeni.
Kutokana na ukweli huo nilidhani kwa makusudi kabisa serikali ingewekeza sana kwenye elimu na teknolojia ya kilimo!!
Kilimo kinaweza ajili vijana wote nchini wasio na kazi.Soko tu la China hata KILA mtza akilima bado hatuwezi lijaza achilia masoko ya ulaya.Ni aibu sana kuagiza nje mafuta ya kula huku tuna ardhi ya bure na maji tele
 
Kilimo kinaweza ajili vijana wote nchini wasio na kazi.Soko tu la China hata KILA mtza akilima bado hatuwezi lijaza achilia masoko ya ulaya.Ni aibu sana kuagiza nje mafuta ya kula huku tuna ardhi ya bure na maji tele
Uko sahihi sana na sio mafuta tuu yaani nchi hii tunaaibishana sana tunaagiza bidhaa nyingi toka nje zinazozalishwa na wakulima wa mataifa ya wenzetu vitu kama sukari, ngano, maepo nk badala ya kuumiza vichwa ili tubaki na zero import ya bidhaa zinazozalishwa mashambani badala yake tunaumiza vichwa kuvunja vibanda vya machinga!!
 
Uko sahihi sana na sio mafuta tuu yaani nchi hii tunaaibishana sana tunaagiza bidhaa nyingi toka nje zinazozalishwa na wakulima wa mataifa ya wenzetu vitu kama sukari, ngano, maepo nk badala ya kuumiza vichwa ili tubaki na zero import ya bidhaa zinazozalishwa mashambani badala yake tunaumiza vichwa kuvunja vibanda vya machinga!!
Hio ilitakiwa iwe Kazi ya TISS na ya sio ya kuiba kura.Bakhresa anawafaidisha Sana wakulima wa ngano wa Canada wanampa meli za ngano then akiuza unga, mikate,maandazi anawapa pesa zao sababu tu hakuna uzalishaji nchini iliyopo haimtoshi,mashamba yanaota visiki tu Mbulu,Mbeya,Iringa,klm hizo pesa anazowapa wacanada ilifaa wapewe wakulima wetu.Hawa wanachojua kwa bidii ni kupambana na upinzani tu badala ya kupambana na umasikini.
 
Dawa ya machinga ni virungu na sheria kali kama zilivyo sheria za Rwanda...Rwanda huwezi mkuta mtu na beseni Wala toroli pale kigali..haya mengine ni kubembeleza a tu...etu kuwatafutia sehemu ya biashara..that's impractical..ajira tu serikali imeshindwa kutoa ajirakwa wahitimu iweje iweze kuwatafutia maeneo ya biashara machinga wote.its impossible
 
Dawa ya machinga ni virungu na sheria kali kama zilivyo sheria za Rwanda...Rwanda huwezi mkuta mtu na beseni Wala toroli pale kigali..haya mengine ni kubembeleza a tu...etu kuwatafutia sehemu ya biashara..that's impractical..ajira tu serikali imeshindwa kutoa ajirakwa wahitimu iweje iweze kuwatafutia maeneo ya biashara machinga wote.its impossible
Ndugu trubarg hii suluhisho yako kuhusu machinga hauoni kama itazalisha tatizo kubwa sana!?
 
Back
Top Bottom