Suluhisho la yanayotokea Mtwara ni Sera ya Majimbo, Katiba Mpya ilitazame hili

Suluhisho la yanayotokea Mtwara ni Sera ya Majimbo, Katiba Mpya ilitazame hili

Mtanke

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2011
Posts
743
Reaction score
1,839
Nimefuatilia yanayoendelea Lindi na Mtwara na hoja za Serikali pamoja na wadau mbalimbali nikagundua serikali inataka kupingana na ukweli tu bila sababu. Nimeshindwa kuelewa maana ya kauli ya serikali kwamba mali zinazogundulika sehemu yoyote ya nchi hii ni mali za Watanzania wote. Hao Watanzania wote maana yake nini na ni akina nani hao Watanzania wote!!?? Maana sijaona namna madini, misitu, pembe za ndovu zilivyotunufaisha hasa mimi binafsi zaidi ya kila siku kusikia tuhuma za ujangili, ufisadi, mikataba mibovu n.k na ubaya wanaotajwa katika tuhuma na kashfa zote hizi ni kikundi kilekile cha watu au hicho ndio kinakula halafu Watanzania wote tunashiba??. Sera ya Majimbo ndio suluhisho. Natamani Wasukuma, Wachaga, Watu wa nyanda za juu kusini, Kanda ya ziwa, Arusha na wote ambao rasilimali zao zinavunwa na hiki kikundi kinachojiita Watanzania wote tuamke na kuwashika mkono na ikibidi tuipake mikono yao kwenye mchanga ili wasiendelee kula tena la sivyo wtamaliza kila kitu maana hawashibi. Hawa ni madalali wan chi yetu na ndio maana wanapeana tu vyeo kwenye Chama na Serikali ili wawe na kinga na kujihakikishia usalama. Tuamke Watanzania. Wanapoonewa wa Mtwara tuwaunge mkono maana kesho itakuwa zamu ya watu wa Bahi, na Watanzania wengine kwa niaba ya Watanzania wote.
 
Ni wazo Zuri ila Ndg zetu wa kanda ya Kati Dodoma labda Watafaidi jengo la Bunge ambalo si Kitega Uchumi...Ebu katiba Itusaidie hili lakini Pia ndio Utakuwa Mwanzo wa Kusimika Bendera hasa huku Mara itakuwa Nchi huru, si Mnakumbuka enzi zile??. Tena Msijaribu Tutajitenga na Migodi yetu.
 
Utengano huo hautawaacha salama. Utazalisha aina ingine ya ubaguzi hadi kuisambaratisha jamii nzima.
 
hao wanaotaka sera ya majimbo ndio wanaochochea vurugu mtwara
 
mkuu haya mambo unayosema ni kuandaa nchi ya kibaguzi na yenye mwenye nacho kinakuwa chake,pengine kama unavyofahamu kunachama kimojawapo ambacho kinasimamia sera hii pengine unakipigia debe hicho chama.
 
Nimefuatilia yanayoendelea Lindi na Mtwara na hoja za Serikali pamoja na wadau mbalimbali nikagundua serikali inataka kupingana na ukweli tu bila sababu. Nimeshindwa kuelewa maana ya kauli ya serikali kwamba mali zinazogundulika sehemu yoyote ya nchi hii ni mali za Watanzania wote. Hao Watanzania wote maana yake nini na ni akina nani hao Watanzania wote!!?? Maana sijaona namna madini, misitu, pembe za ndovu zilivyotunufaisha hasa mimi binafsi zaidi ya kila siku kusikia tuhuma za ujangili, ufisadi, mikataba mibovu n.k na ubaya wanaotajwa katika tuhuma na kashfa zote hizi ni kikundi kilekile cha watu au hicho ndio kinakula halafu Watanzania wote tunashiba??. Sera ya Majimbo ndio suluhisho. Natamani Wasukuma, Wachaga, Watu wa nyanda za juu kusini, Kanda ya ziwa, Arusha na wote ambao rasilimali zao zinavunwa na hiki kikundi kinachojiita Watanzania wote tuamke na kuwashika mkono na ikibidi tuipake mikono yao kwenye mchanga ili wasiendelee kula tena la sivyo wtamaliza kila kitu maana hawashibi. Hawa ni madalali wan chi yetu na ndio maana wanapeana tu vyeo kwenye Chama na Serikali ili wawe na kinga na kujihakikishia usalama. Tuamke Watanzania. Wanapoonewa wa Mtwara tuwaunge mkono maana kesho itakuwa zamu ya watu wa Bahi, na Watanzania wengine kwa niaba ya Watanzania wote.

kwa post kama hii bado anatafutwa mchawi wa vurugu za MTWARA? Serikali iokoeni nchi kuingia katika machafuko , mkamateni mwenyekiti wa CHADEMA kwani ni wzi kabisa kwamba wao ndiyo wako nyuma ya vurugu za hizi.
 
Nimefuatilia yanayoendelea Lindi na Mtwara na hoja za Serikali pamoja na wadau mbalimbali nikagundua serikali inataka kupingana na ukweli tu bila sababu. Nimeshindwa kuelewa maana ya kauli ya serikali kwamba mali zinazogundulika sehemu yoyote ya nchi hii ni mali za Watanzania wote. Hao Watanzania wote maana yake nini na ni akina nani hao Watanzania wote!!?? Maana sijaona namna madini, misitu, pembe za ndovu zilivyotunufaisha hasa mimi binafsi zaidi ya kila siku kusikia tuhuma za ujangili, ufisadi, mikataba mibovu n.k na ubaya wanaotajwa katika tuhuma na kashfa zote hizi ni kikundi kilekile cha watu au hicho ndio kinakula halafu Watanzania wote tunashiba??. Sera ya Majimbo ndio suluhisho. Natamani Wasukuma, Wachaga, Watu wa nyanda za juu kusini, Kanda ya ziwa, Arusha na wote ambao rasilimali zao zinavunwa na hiki kikundi kinachojiita Watanzania wote tuamke na kuwashika mkono na ikibidi tuipake mikono yao kwenye mchanga ili wasiendelee kula tena la sivyo wtamaliza kila kitu maana hawashibi. Hawa ni madalali wan chi yetu na ndio maana wanapeana tu vyeo kwenye Chama na Serikali ili wawe na kinga na kujihakikishia usalama. Tuamke Watanzania. Wanapoonewa wa Mtwara tuwaunge mkono maana kesho itakuwa zamu ya watu wa Bahi, na Watanzania wengine kwa niaba ya Watanzania wote.

mkuu ningekuwatayari kuunga mkono hoja yako kama ungebainisha faida na hasara lakini umeandika kilaghai tu kwa lengo la kutetea chama fulani chenye hiyo sera.
 
mkuu haya mambo unayosema ni kuandaa nchi ya kibaguzi na yenye mwenye nacho kinakuwa chake,pengine kama unavyofahamu kunachama kimojawapo ambacho kinasimamia sera hii pengine unakipigia debe hicho chama.
mkuu unajua muasi akishaamua kuasi hata aibu humtoka, hivi kwa mtu mwenyekili anaweza kuleta mada kama hii? hawa CHADEMA kweli hata aibu ya kibaguzi sasa imeshawatoka wanaamua kujianika hadharani.
 
Ni wazo Zuri ila Ndg zetu wa kanda ya Kati Dodoma labda Watafaidi jengo la Bunge ambalo si Kitega Uchumi...Ebu katiba Itusaidie hili lakini Pia ndio Utakuwa Mwanzo wa Kusimika Bendera hasa huku Mara itakuwa Nchi huru, si Mnakumbuka enzi zile??. Tena Msijaribu Tutajitenga na Migodi yetu.

teh teh teh , umeona mkuu, yaani sera hii sera ya Majimbo ni ya kipuuzi kweli
 
mkuu ningekuwatayari kuunga mkono hoja yako kama ungebainisha faida na hasara lakini umeandika kilaghai tu kwa lengo la kutetea chama fulani chenye hiyo sera.
Hawa CHADEMA hata aibu sasa hawana.
 
hello, tz. acheni kupandikizana chuki miongoni mwetu, maliasili tulizonazo nizakwetu sote watanzania. Tuwe na aibu katika jamii yetu.
 
Back
Top Bottom