Suluhu ya div zero kidatu cha nne

Umutimbaru

Member
Joined
Jul 22, 2011
Posts
91
Reaction score
5
Matokeo mabaya ya kidatu cha nne yangelipunguzwa kama ile sera ya mitihani ya kidatu cha pili ingeiiimarishwa na kuzingatiwa. Mtihani wa kidato cha pili unawafanya watoto kujiandaa vyema kuvuka daraja la maandalizi ya kufanya mtihani wa kidato cha nne.
Mtihani huo ukizingatiwa kiasi kwamba wale ambao hawajafaulu wasivuke kwenda kidato cha tatu matikeo ya kidatu cha nne yatakuwa na uafadhali.
Kama utaratibu huu uliopo wa kujaza madarasa bila kuzingatia sifa utaendelea, matokeo ya kuwa na zero nyingi mwisho wa mwaka utakuepo TU
Sera ya mitihani ya kidato cha pili ingawa imerudi, iboreshwe ili wavukao kwenda kidato cha tatu wawe wazuri, hivyo hivyo kwa mtihani darasa la nne.
 
Matokeo mabaya ya kidatu cha nne yangelipunguzwa kama ile sera ya mitihani ya kidatu cha pili ingeiiimarishwa na kuzingatiwa. Mtihani wa kidato cha pili unawafanya watoto kujiandaa vyema kuvuka daraja la maandalizi ya kufanya mtihani wa kidato cha nne.
Mtihani huo ukizingatiwa kiasi kwamba wale ambao hawajafaulu wasivuke kwenda kidato cha tatu matikeo ya kidatu cha nne yatakuwa na uafadhali.
Kama utaratibu huu uliopo wa kujaza madarasa bila kuzingatia sifa utaendelea, matokeo ya kuwa na zero nyingi mwisho wa mwaka utakuepo TU
Sera ya mitihani ya kidato cha pili ingawa imerudi, iboreshwe ili wavukao kwenda kidato cha tatu wawe wazuri, hivyo hivyo kwa mtihani darasa la nne.
 
Unachosema ni kweli kimechangia matokea mabaya; ukiangalia waliomaliza form IV mwaka jana, hawakuchujwa wakati wakiwa form II. Ndio wakati nadhani JK alisema mtihani wa form II uwe wa kujipima tu na si wa kuzuia mwanafunzi kupanda darasa.
Kuhusu wanaoingia form I, ebu wizara itupatie marks za waliomaliza darasa la 7 mwaka jana ili tuone waliostahili kuingia kidato cha kwanza ni akina nani na ni akina nani wamepelekwa tu kujaza nafasi. Mchujo mzuri wa kuingia form I unaweza kuonyesha kuwa si kila kata inapaswa kuwa na sekondari. Ikitokea hivyo basi shule ziunganishwe na badala ya kutawanya nguvu kwa kila kata tunaziunganisha.
Tayari matokeo ya kidato cha pili mwaka jana yameonyesha uwezekano huo; kama shule moja imebaki na wanafunzi 16 kidato cha tatu na nyingine 40, kama ziko jirani kwanini zisiunganishwe?. Yawezekana kama wangechuja vizuri darasa la 7 wangepata darasa moja tu la wanafunzi 70 kwa kata zote mbili.
 
Ni kweli ugonjwa uliopo wa kujaza shule bila sifa kwaajili ya ufahari wa kisiasa utatupeleka pa baya kielimu.
Shule nyingi zimejengwa na wananchi kwa ahadi ya kuongeza idadi ya watoto kujiunga na kidatu. cha kwanza na kuletewa walimu, lakini baada ya kumalizika wanafunzi wanajazwa bila kujali sifa kwa kukwepa lawama.
Utaratibu huu niwakuwaragai wananchi wengi ambao wanapenda watoto wao wasome. Pia nikuwapotezea muda watoto wawakulima. Bora kusema ukweli mapungufu yaliopo ili mzazi awe na uamuzi juu ya hatima ya mwanae.
Nashauri tusiangalie wingi bila kujali ubora. Tujali ubora.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…