Sumaye: Tusifurahie Bunge la chama kimoja

Sumaye: Tusifurahie Bunge la chama kimoja

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Baada ya Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuonyesha 'madudu' ya ubadhirifu wa fedha kwenye maeneo mbalimbali, Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, ameibuka akisema Bunge linapaswa kuwa kali katika kuisimamia na kuishauri Serikali.

Sumaye aliyekuwa Waziri Mkuu kwa muongo mmoja kuanzia mwaka 1995 hadi 2005 katika utawala wa Awamu ya Tatu amesema kwa kawaida hakuna Serikali ya demokrasia inayokataa ushauri wa Bunge.

"Haya mambo yanapojitokeza mara kwa mara lazima tukubali kuna tatizo mahali fulani, kubwa kabisa ni Serikali lakini Bunge nalo halifuatili," alisema.

Sumaye anatoa kauli hiyo ikiwa ni takribani wiki mbili zimepita tangu Ripo-ti za CAG Charles Kichere kwa mwaka 2021/22 zilizowasilishwa bungeni jijini Dodoma.

Katika mahojiano kati ya Sumaye na televisheni ya mtandaoni ya Dar 24, yalijikita katika masuala mbalimbali yanayomhusu Sumaye na ripoti za CAG, alisema;

"Bunge lina kazi kubwa na linatakiwa liwe na ukali zaidi, ndiyo maana tunapenda Bunge lenye vyama mbalimbali kwa sababu ni afya kwa nchi.

"Hiki kitu watu hawakielewi, watu wanafikiri ukiwa na Bunge la chama kimoja, ndio njema, hapana. Ukiwa na Bunge la chama kimoja ndani ya mfumo wa vyama vingi ni tatizo," alisema.

Ripoti za CAG alizokuwa anajadili Sumaye zimeonyesha ubadhirifu kati-ka taasisi na mamlaka za Serikali, hali ambayo imewaibua wadau wakitaka hatua kali zichukuliwe dhidi ya wahusika.

Tayari Rais Samia Suluhu Hassan, amekwishaanza kuchukua hatua kwa kutengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) na kuivunja Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Mbali na hilo, Rais Samia ametoa maagizo kwa Katibu Mkuu Kiongozi.

DK Moses Kusiluka kuhakikisha makatibu wakuu na watendaji wakuu wote wa taasisi za Serikali wanapitia kwa kina taarifa ya CAG, wajibu na kuzifanyia kazi kwa haraka hoja zote.

Bunge la sasa ambalo lilitokana na uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020, lina wabunge wengi wa chama tawala- Chama Cha Mapinduzi (CCM), zaidi ya asilimia 90 huku upinzani wakiwa wachache tofauti na mabunge yaliyopita na wengine hawatambuliwi na vyama vyao.

Aprili 12 mwaka huu, Spika Tulia Ack-son alisema wabunge wanaruhusiwa kuijadili ripoti hiyo kwa namna wanavyoona inafaa lakini watambue kuwa Serikali haitalazimika kujibu kwa kuwa Kamati za Bunge Mashirika ya Umma (PAC) na ile ya Serikali za mitaa (LAAC) itapitia taarifa hiyo na itawasilishwa bungeni.
 
Ila Kipindi cha mwendazake alikaa kimyaa kama maji ya mtungi. Sasa hivi ndio anakumbuka Bunge la Chama kimoja.

Wasichoeleza kwa undani ni kwamba bunge la chama kimoja ni matokeo ya tume mbovu ya uchaguzi na katiba yenye Mrengo wa urais wa kifalme.
 
Ndiyo maana anaitwa mr ziro.

Hajui kwamba wabunge hawajipeleki bungeni wanapelekwa na wananchi.

Huwezi kuwalazimisha wananchi wachague chama wasichokitaka.
 
Ndiyo maana anaitwa mr ziro.

Hajui kwamba wabunge hawajipeleki bungeni wanapelekwa na wananchi.

Huwezi kuwalazimisha wananchi wachague chama wasichokitaka.
Ni lini wananchi walipewq uhuru huo? Au wewe ndio Ziro.

Yule Mwendawazimu alibebana na washkaj wake kama hii nchi ni ya familia yake akawajaza bungeni na matokeo yake ni haya unayoyaona...
 
Kati ya ushetani mkubwa uliowahi kufanywa na awamu ya 5, ukiacha mauaji, ni kupora uchaguzi. Madhara yake tunaendelea kuyashuhudia.

Tukazanie katiba mpya. La sivyo, kuna siku tutapata tena kichaa mwingine anayeweza kuwa mharibifu zaidi.
 
Ndiyo maana anaitwa mr ziro.

Hajui kwamba wabunge hawajipeleki bungeni wanapelekwa na wananchi.

Huwezi kuwalazimisha wananchi wachague chama wasichokitaka.
Wananchi hawachagui chama, wanachagua wagpombea wanaofaa bila kujali wanatoka chama gani cha siasa. Huu utapeli ulitokana na uhuni wa awamu ya Ile ya kupitishwa wahuni bila kupingwa pamoja na kuunga juhudi feki.
 
Huyu mzee sijamwelewa! Wakati tunaunda bunge la chama kimoja mwaka 2020 si alikuwepo? Mbona hatukumsikia akikemea jambo hilo?
 
Baada ya Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuonyesha 'madudu' ya ubadhirifu wa fedha kwenye maeneo mbalimbali, Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, ameibuka akisema Bunge linapaswa kuwa kali katika kuisimamia na kuishauri Serikali.

Sumaye aliyekuwa Waziri Mkuu kwa muongo mmoja kuanzia mwaka 1995 hadi 2005 katika utawala wa Awamu ya Tatu amesema kwa kawaida hakuna Serikali ya demokrasia inayokataa ushauri wa Bunge.

"Haya mambo yanapojitokeza mara kwa mara lazima tukubali kuna tatizo mahali fulani, kubwa kabisa ni Serikali lakini Bunge nalo halifuatili," alisema.

Sumaye anatoa kauli hiyo ikiwa ni takribani wiki mbili zimepita tangu Ripo-ti za CAG Charles Kichere kwa mwaka 2021/22 zilizowasilishwa bungeni jijini Dodoma.

Katika mahojiano kati ya Sumaye na televisheni ya mtandaoni ya Dar 24, yalijikita katika masuala mbalimbali yanayomhusu Sumaye na ripoti za CAG, alisema;

"Bunge lina kazi kubwa na linatakiwa liwe na ukali zaidi, ndiyo maana tunapenda Bunge lenye vyama mbalimbali kwa sababu ni afya kwa nchi.

"Hiki kitu watu hawakielewi, watu wanafikiri ukiwa na Bunge la chama kimoja, ndio njema, hapana. Ukiwa na Bunge la chama kimoja ndani ya mfumo wa vyama vingi ni tatizo," alisema.

Ripoti za CAG alizokuwa anajadili Sumaye zimeonyesha ubadhirifu kati-ka taasisi na mamlaka za Serikali, hali ambayo imewaibua wadau wakitaka hatua kali zichukuliwe dhidi ya wahusika.

Tayari Rais Samia Suluhu Hassan, amekwishaanza kuchukua hatua kwa kutengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) na kuivunja Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Mbali na hilo, Rais Samia ametoa maagizo kwa Katibu Mkuu Kiongozi.

DK Moses Kusiluka kuhakikisha makatibu wakuu na watendaji wakuu wote wa taasisi za Serikali wanapitia kwa kina taarifa ya CAG, wajibu na kuzifanyia kazi kwa haraka hoja zote.

Bunge la sasa ambalo lilitokana na uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020, lina wabunge wengi wa chama tawala- Chama Cha Mapinduzi (CCM), zaidi ya asilimia 90 huku upinzani wakiwa wachache tofauti na mabunge yaliyopita na wengine hawatambuliwi na vyama vyao.

Aprili 12 mwaka huu, Spika Tulia Ack-son alisema wabunge wanaruhusiwa kuijadili ripoti hiyo kwa namna wanavyoona inafaa lakini watambue kuwa Serikali haitalazimika kujibu kwa kuwa Kamati za Bunge Mashirika ya Umma (PAC) na ile ya Serikali za mitaa (LAAC) itapitia taarifa hiyo na itawasilishwa bungeni.
Hapa ndipo Magufuli alikosea kushiriki Hadi watu wa ajabu kuingiaa Bungeni kwa mbeleko

Japo nchi hii hatuna upinzani ila angalau Hawa wapinzani mamluki wangesaidia kidogo kuiamsha serikali

Sent from my CPH2217 using JamiiForums mobile app
 
Baada ya Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuonyesha 'madudu' ya ubadhirifu wa fedha kwenye maeneo mbalimbali, Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, ameibuka akisema Bunge linapaswa kuwa kali katika kuisimamia na kuishauri Serikali.

Sumaye aliyekuwa Waziri Mkuu kwa muongo mmoja kuanzia mwaka 1995 hadi 2005 katika utawala wa Awamu ya Tatu amesema kwa kawaida hakuna Serikali ya demokrasia inayokataa ushauri wa Bunge.

"Haya mambo yanapojitokeza mara kwa mara lazima tukubali kuna tatizo mahali fulani, kubwa kabisa ni Serikali lakini Bunge nalo halifuatili," alisema.

Sumaye anatoa kauli hiyo ikiwa ni takribani wiki mbili zimepita tangu Ripo-ti za CAG Charles Kichere kwa mwaka 2021/22 zilizowasilishwa bungeni jijini Dodoma.

Katika mahojiano kati ya Sumaye na televisheni ya mtandaoni ya Dar 24, yalijikita katika masuala mbalimbali yanayomhusu Sumaye na ripoti za CAG, alisema;

"Bunge lina kazi kubwa na linatakiwa liwe na ukali zaidi, ndiyo maana tunapenda Bunge lenye vyama mbalimbali kwa sababu ni afya kwa nchi.

"Hiki kitu watu hawakielewi, watu wanafikiri ukiwa na Bunge la chama kimoja, ndio njema, hapana. Ukiwa na Bunge la chama kimoja ndani ya mfumo wa vyama vingi ni tatizo," alisema.

Ripoti za CAG alizokuwa anajadili Sumaye zimeonyesha ubadhirifu kati-ka taasisi na mamlaka za Serikali, hali ambayo imewaibua wadau wakitaka hatua kali zichukuliwe dhidi ya wahusika.

Tayari Rais Samia Suluhu Hassan, amekwishaanza kuchukua hatua kwa kutengua uteuzi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA) na kuivunja Bodi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC).

Mbali na hilo, Rais Samia ametoa maagizo kwa Katibu Mkuu Kiongozi.

DK Moses Kusiluka kuhakikisha makatibu wakuu na watendaji wakuu wote wa taasisi za Serikali wanapitia kwa kina taarifa ya CAG, wajibu na kuzifanyia kazi kwa haraka hoja zote.

Bunge la sasa ambalo lilitokana na uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020, lina wabunge wengi wa chama tawala- Chama Cha Mapinduzi (CCM), zaidi ya asilimia 90 huku upinzani wakiwa wachache tofauti na mabunge yaliyopita na wengine hawatambuliwi na vyama vyao.

Aprili 12 mwaka huu, Spika Tulia Ack-son alisema wabunge wanaruhusiwa kuijadili ripoti hiyo kwa namna wanavyoona inafaa lakini watambue kuwa Serikali haitalazimika kujibu kwa kuwa Kamati za Bunge Mashirika ya Umma (PAC) na ile ya Serikali za mitaa (LAAC) itapitia taarifa hiyo na itawasilishwa bungeni.
Mzee sumaye anawakosoa walinda legacy walipoamua kua na bunge la chama kimoja? Inamaana hajui kua walinda legacy ndio wazalendo wa kweli ambao waliamini katika chama kimoja bungeni? Mzee sumaye nakwambia ngoja walinda legacy waje....
 
Back
Top Bottom