DOKEZO Sumbawanga MANISPAA madereva bajaji wamekaa kikao na kupandisha gharama za usafiri hususani bajaji kutoka Tshs 600 hadi 800 mpaka elfu 1000

DOKEZO Sumbawanga MANISPAA madereva bajaji wamekaa kikao na kupandisha gharama za usafiri hususani bajaji kutoka Tshs 600 hadi 800 mpaka elfu 1000

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

JET SALLI

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2014
Posts
2,392
Reaction score
1,578
Ndugu zangu tunapata taarifa nyingi toka kila pande ya nchi yetu pendwa ya Tanzania,Leo nimepata taarifa kuwa huko Sumbawanga MANISPAA madereva bajaji wamekaa kikao na kupandisha gharama za usafiri hususani bajaji kutoka Tshs 600 hadi 800 mpaka elfu 1000 kwa baadhi ya maeneo,ilhali gharama za mafuta zinashuka kila siku.

Nimejaribu kutafakari hivi chombo rasmi kinachopanga nauli za usafiri wa umma kinafanya kazi gani hadi madereva BAJAJI na viongozi wao wanachukua mamlaka mikononi na kupandisha gharama kiholela kabisa na kuongeza ukali wa maisha ya watanzania wa MANISPAA ya sumbawanga na Tanzania kwa ujumla.Mkoa una viongozi na mkuu wa mkoa ni mtoto wa Baba wa Taifa Mwl.Julius kambarage Nyerere ndugu yetu Makongoro Nyerere yawezekana hana taarifa hizi za kikundi cha wahuni waliokaa na kujigeuza SUMATRA.

Nchi hii inaongozwa kwa mujibu wa Sheria ninaomba mamlaka husika fuatilieni huko Sumbawanga MANISPAA mtaigundua hiyo Sumatra mpya iliyozuka naamini mtachukua hatua stahiki kwa mujibu wa Sheria,Tukumbuke gharama za mafuta zinaposhuka watanzania hawapaswi kuendelea kuteseka bila sababu zozote za msingi.Mamlaka husika fuatilia.
 
Kama wahun wachache wanakaa na kuanza kuumiza wananch na serk ipo bas tuko katika hatar kubwa sn

Mkuu wa mkoa yupo,mkuu wa wilaya yupo pamoja na mkurugenzi lkn hakuna hata mtu mmoja alieonesha kutoa walau kauli kwa uuni wa watu wachache

Tunaomba mamalaka inayohusika na utetez wa wanach katika suala la nauli iingilie kati uuni huu mana kamwe hauwez vumiliwa hasa katika mazingira magumu tulionayo
 
Hii ni balaa mpaka tumalize na huyu mama yenu sijui na hv huwa hajali chochote.kazi ipo.
 
Kama huna 800 au buku tembea kwa mguu. Au nunua Yako uwabebe kwa jero
 
Mkuu wa mkoa makongolo Nyerere anatakiwa kuchukua hatua haraka maana gharama za nishati ya mafuta ziko chini.
 
Na leo tarehe jumatano EWURA imetangaza bei mpya bado ziko chini ila sasa ninyi EWURA hakikisheni na udhibiti wa nauli pia yaani mifumo yenu isomane vzr.
 
Bajaji na Bodaboda hazisimamiwi na Latra kwa maana Latra hawatoi ruti rasmi wala kupanga nauli ya kituo hadi kituo kwa hivyo vyombo kwahiyo wanajiongeza tu wenyewe kama walivyojiongeza kwa kujichagulia ruti.
Hivyo vyombo kimsingi vinatakiwa kupaki kituoni kwa ajili ya kukodiwa ndiyo maana mara nyingi huko mikoani wanakuwa na migogoro ya mara kwa mara na madereva na makondakta wa daladala kwa kuingilia ruti za daladala.
 
Back
Top Bottom