Swali fikirishi: Barafu ya mlima Kilimanjaro ikiyeyuka yote, je hifadhi ya mlima Kilimanjaro itaendelea kupata watalii wengi?

Swali fikirishi: Barafu ya mlima Kilimanjaro ikiyeyuka yote, je hifadhi ya mlima Kilimanjaro itaendelea kupata watalii wengi?

Balqior

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2021
Posts
2,406
Reaction score
8,039
Habarini,

Kama sikosei takwimu zinasema hifadhi ya mlima Kilimanjaro ndo inayoongoza kwa kuingiza fedha nyingi zaidi za kigeni hapa nchini kuliko hifadhi zingine. Najiuliza hivi zile barafu pale juu zikiisha, ile hifadhi itaendelea kuvutia watalii kweli🤔

Ninaposema barafu, namaanisha glaciers yenye muundo wa magorofa marefu yaliyoenda hewani, yenye muonekano kama huu hapa chini, na sio theluji, ile ilivyo kama machicha ya nazi, inayonyesha leo, kesho inayeyuka, hii picha hapa chini ni muonekano wa glaciers za mlima Kilimanjaro ukizisogelea kwa karibu

Rebmann-Glacier-for-web.png


Nimekuwa nikifuatilia muonekano wa mlima Kilimanjaro kwa miaka zaidi ya 20, nimegundua glaciers zinayeyuka kwa kasi ya ajabu miaka ya 2002 mlima Kilimanjaro glaciers zake, ukisimama kwa mbali zilikuwa na muonekano huu hapa chini
Screenshot_20240917-192907.jpg


Sahivi mwaka 2024 glaciers unazoziona hapo, ukiangalia through Google maps, zimeyeyuka na kubaki kama chenga chenga tu, kama ilivyo hapa chini
Screenshot_20240917-192646.jpg


Nawaza tu future of tourism for this mountain, miaka 20 inayokuja mlima Kilimanjaro utakuwa kama mlima meru tu. No snow, no glaciers, na vizazi vyetu vijavyo havita-enjoy beautiful view of an ice covered mountain, kama sisi tulivo-enjoy.
 
Back
Top Bottom