Swali kwa madaktari wa kinywa

Swali kwa madaktari wa kinywa

San Opa

New Member
Joined
Oct 12, 2016
Posts
3
Reaction score
1
Habari za muda huu.... Kuna tatizo limenipata wakati wa kutafuna kuna upande wa mwisho wa mdono kuna kanyama nakang'ata hivyo inanifanya nishindwe kutafuna vizur nilipokwenda uospital walinambia kuwa fizi zinavimba na kupelekea kunga'ata nyama ya mashavuni wakanpa amxiln na panaldo imemaliza week sion tofauti anaejua tiba au ni ugonjwa wa aina gani naomba anijuze asanten
 
km walivyokuambia sio ugonjwa ni nyama ya fizi imejitokeza inawezakana kuna jino linatokeza.usihofu sana
 
Habari za muda huu.... Kuna tatizo limenipata wakati wa kutafuna kuna upande wa mwisho wa mdono kuna kanyama nakang'ata hivyo inanifanya nishindwe kutafuna vizur nilipokwenda uospital walinambia kuwa fizi zinavimba na kupelekea kunga'ata nyama ya mashavuni wakanpa amxiln na panaldo imemaliza week sion tofauti anaejua tiba au ni ugonjwa wa aina gani naomba anijuze asanten

Kwanza kabisa pole kwa hilo tatizo Mkuu na najua ' maumivu ' unayoyapata kwani hata Mimi huko nyuma nilikuwa na tatizo kama lako ila nilipata tiba zifuatazo ambazo naomba nawe nikuambie ili uweze kuzijaribu na kupona.
  1. Kwanza usipende kutumia Mswaki mmoja kwa muda mrefu.
  2. Jitahidi sana kupiga mswaki mara kwa mara.
  3. Hakikisha mswaki wako siyo wenye nyuzi ngumu kule mbele siyo mnene sana kwani yawezekana wakati unauweka mdomoni huathiri zile gums zako kule katika ' magego ' yako na hatimaye kukutengenezea kidonda.
  4. Hakikisha kila mara unasukutua na dawa iitwayo ' Haydrogen ' kwani kinachokusumbua yawezekana ikawa ni ' bacteria ' waliopo katika ' gums ' zako na hayo maumivu unayoyasikia ni kwamba hao ' wadudu ' wanashambulia hiyo sehemu.
  5. Tafuta ' Karafuu ' ambazo zinapatikana mno madukani kisha chukua kidogo iweke ile sehemu inayokuuma halafu ibane pale na meno kama vile unaikamua ili yale maji yake yasambae kwenye kidonda au sehemu ya maumivu kisha unatema. Fanya hivyo kwa siku tatu tu mfululizo Mkuu na utapona kabisa.
Ni hayo tu Mkuu na nimekujibu haya kutokana na uzoefu wangu wa tatizo kama lako ambalo nilikuwa nalo ILA humu JF kuna Madaktari wa Meno wengi na tena ni ' Nguli ' kabisa hivyo naamini na Wao kuna watakayokuambia kwani Mimi siyo Daktari isipokuwa nimekupa tu uzoefu wangu. Pole sana Mkuu ila hopefully utapona na kuwa safi. Akhsante.
 
Kwanza kabisa pole kwa hilo tatizo Mkuu na najua ' maumivu ' unayoyapata kwani hata Mimi huko nyuma nilikuwa na tatizo kama lako ila nilipata tiba zifuatazo ambazo naomba nawe nikuambie ili uweze kuzijaribu na kupona.
  1. Kwanza usipende kutumia Mswaki mmoja kwa muda mrefu.
  2. Jitahidi sana kupiga mswaki mara kwa mara.
  3. Hakikisha mswaki wako siyo wenye nyuzi ngumu kule mbele siyo mnene sana kwani yawezekana wakati unauweka mdomoni huathiri zile gums zako kule katika ' magego ' yako na hatimaye kukutengenezea kidonda.
  4. Hakikisha kila mara unasukutua na dawa iitwayo ' Haydrogen ' kwani kinachokusumbua yawezekana ikawa ni ' bacteria ' waliopo katika ' gums ' zako na hayo maumivu unayoyasikia ni kwamba hao ' wadudu ' wanashambulia hiyo sehemu.
  5. Tafuta ' Karafuu ' ambazo zinapatikana mno madukani kisha chukua kidogo iweke ile sehemu inayokuuma halafu ibane pale na meno kama vile unaikamua ili yale maji yake yasambae kwenye kidonda au sehemu ya maumivu kisha unatema. Fanya hivyo kwa siku tatu tu mfululizo Mkuu na utapona kabisa.
Ni hayo tu Mkuu na nimekujibu haya kutokana na uzoefu wangu wa tatizo kama lako ambalo nilikuwa nalo ILA humu JF kuna Madaktari wa Meno wengi na tena ni ' Nguli ' kabisa hivyo naamini na Wao kuna watakayokuambia kwani Mimi siyo Daktari isipokuwa nimekupa tu uzoefu wangu. Pole sana Mkuu ila hopefully utapona na kuwa safi. Akhsante.
Asante sana mkuu nashukuru sana kwa ushauri wako naanza ufanyia kazi sasa na nitakupa mrejesho
 
Back
Top Bottom