ukweli mchungu......
samatta hapo alipo ndio keshafika kwenye kilele cha mafanikio yake, hawezi kutoboa zaidi ya hapo. tena awe makini mkataba ukiisha pale genk hawezi kupewa mwingine na ataishia kwenda kuchezea moroko, egypt, south africa na kwingineko.
kamwe hawezi kwenda kuchezea ligi kubwa kama french, germany, spain , england n.k. yaani kwa uwezo wa samatta, sio tu kuchezea ligi kuu, hawezi hata kuchezea timu za daraja la kwanza mfano championship.
sababu.
1. nafasi anayocheza(pure stricker) inamgharimu sana, anatakiwa afunge magoli mengi sana ili timu kubwa zimuone zimchukue, sina takwimu sahihi lakini huu ni mwaka wa tatu belgium sidhani kama ameshafunga goli 50.
2. umri unakimbia. yes umri, pasport yake inasoma 24/25 lakini ni uongo, jamaa ni mkubwa zaidi ya hapo. i bet miaka yake inaanzia 28-32.
katokea african lyon akaenda simba akacheza mwaka mmoja, akaenda congo akacheza miaka sita, now yupo belgium mwaka wa tatu. hata kama tukiongopa aliondoka simba na miaka 18 bado hawezi kuwa na huo umri ambao uppo kwenye makaratasi.
hata haya majeruhi ya mara kwa mara ni kiashiria tosha umri unasogea.
jamaa yupo na spirit ya hali ya juu, angekuwa anacheza nafasi nyingine kama midfild, beki au kipa pengine now angekuwa sehemu nyingine. ila yote kwa yote kapeperusha bendera yetu vyema, pengine watatokea wengine wafike mbali kuliko alipofika yeye.....
[HASHTAG]#hainakufeli[/HASHTAG]