Swali kwa TRA

Swali kwa TRA

ze farmer

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2016
Posts
922
Reaction score
1,804
Sifa moja ya kodi ni kuwa comprehensive kwa maana ya inatakiwa kucover eneo kubwa na sio kuwapa burden watu wachache walipe kodi.
Sasa.
Kuna hawa jamaa wenye nyumba za kupanga inshort wanapokea bilions of money every month na hakuna kodi wanachajiwa ukitoa ile 10,000 ambayo hata nyumba za kawaida tu tunatoa.
TRA vipi mmelala au hamtumii taaluma zenu mmebaki kushinda kumnafukuzana na mama ntilie.
 
TRA yatangaza kukusanya kodi za nyumba za kupanga
3 years ago Comments Offon TRA yatangaza kukusanya kodi za nyumba za kupanga

Mamlaka ya Mapato Tanzannia (TRA) imetangaza mpango wa kuanza kukusanya kodi kwenye nyumba za kupangisha ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kupata fedha ambazo Serikali ilikuwa haipati kutoka kwenye vyanzo vyake.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo aliwaambia waandsihi wa habari jana jijini Dar es Salaam kuwa Mamkala hiyo itafanya uhakiki wa nyumba za kupanga na kubaini gharama za kodi.
Aliwataka wananchi wanaopanga katika nyumba hizo kuhakikisha wanashirikiana na TRA kueleza bei ya nyumba na kuepuka kufanya udanganyifu ili wasikumbwe na mkono wa sheria.

“Natoa wito kwa wapangaji na wapangishaji kujiepusha na aina yoyote ya udanganyifu katika suala zima la kodi halisi ya pango kwa kuwa inaweza kuwasababishia kushtakiwa endapo udanganyifu huo utabainika,” alisema Kayombo.
Kayombo alieleza kuwa lengo la Mamlaka hiyo ni kuhakikisha Serikali inapata kodi yote ambayo imekuwa ikikosa kutoka kwa vyanzo mbalimbali ikiwa ni pamoja na nyumba.

Kayombo alieleza kuwa mwezi Julai, Mamlaka hiyo ilikusanya kiasi cha shilingi trilioni 1.055 ambazo ni sawa na asilimia 95.6 ya lengo walilopangiwa na Serikali kwa mwezi huo, ambazo ni shilingi trilioni 1.103.
 
Sifa moja ya kodi ni kuwa comprehensive kwa maana ya inatakiwa kucover eneo kubwa na sio kuwapa burden watu wachache walipe kodi.
Sasa.
Kuna hawa jamaa wenye nyumba za kupanga inshort wanapokea bilions of money every month na hakuna kodi wanachajiwa ukitoa ile 10,000 ambayo hata nyumba za kawaida tu tunatoa.
TRA vipi mmelala au hamtumii taaluma zenu mmebaki kushinda kumnafukuzana na mama ntilie.
Pesa iliyojenga hizo nyumba ilishalipiwa kodi tayari; anachopata kwa kukupangishia wewe ni sawa na riba anayopewa mtu aliwekeza pesa yake kwenye akiba maalumu benki au aliyewekeza kwenye hisa kule DSE
 
Pesa iliyojenga hizo nyumba ilishalipiwa kodi tayari; anachopata kwa kukupangishia wewe ni sawa na riba anayopewa mtu aliwekeza pesa yake kwenye akiba maalumu benki au aliyewekeza kwenye hisa kule DSE
Ukiweka pesa kwny fixed a/c riba unayopewa tra wanakata kodi ya 10%.

Dividend ukipokea huko kwny hisa Tra wanakata kodi ya 5% kama ni co. iko registered hapo DSE na kama haiko registered wanakata 10%(kama nakumbuka vzr).

So mifano yako ni irrelevant mzee baba.
 
Ukiweka pesa kwny fixed a/c riba unayopewa tra wanakata kodi ya 10%.

Dividend ukipokea huko kwny hisa Tra wanakata kodi ya 5% kama ni co. iko registered hapo DSE na kama haiko registered wanakata 10%(kama nakumbuka vzr).

So mifano yako ni irrelevant mzee baba.
Ahsante sana kwa majibu yako; hayo nayajua ila sasa nikuulize kwanini kipato kinachotokana na pango la nyumba (rent) tulipe kodi ya 30% na siyo 10% kama mtu aliyewekeza kwenye kampuni au Fixed Deposit?

Kamama wewe ni mdau mkianza mchakato wa bajeti ya 2020/2021 hilo mliweke kwenye mapendekeze kodi ya mapato ya kupangisha nyumba iwe 10% tutajitokeza kwa hiari kulipa
 
Ahsante sana kwa majibu yako; hayo nayajua ila sasa nikuulize kwanini kipato kinachotokana na pango la nyumba (rent) tulipe kodi ya 30% na siyo 10% kama mtu aliyewekeza kwenye kampuni au Fixed Deposit?

Kamama wewe ni mdau mkianza mchakato wa bajeti ya 2020/2021 hilo mliweke kwenye mapendekeze kodi ya mapato ya kupangisha nyumba iwe 10% tutajitokeza kwa hiari kulipa
Kucharge corporte tax(30%) huo ni ukichaa mkuu lkn huku kwny ma frame tuna withhold 10% ndio inaenda TRA.
 
Kucharge corporte tax(30%) huo ni ukichaa mkuu lkn huku kwny ma frame tuna withhold 10% ndio inaenda TRA.
Ni hivi hiyo 10% kwa mwenye nyumba ni advance; anatakiwa apeleke return yake aonyeshe mapato yote akokotoe kodi ya 30%, apunguze mliomkata nyie wapangaji 10% alipe hiyo tofauti ambayo ni 20%
 
Bado kuna inefficiency kubwa sana kwenye suala la kodi za nyumba za kupanga. Mimi nalipa 500,000 kila mwezi halafu hailipiwi kodi hata kidogo. Kumbukeni hata wenye viwanda waliwekeza hela suala la kuwa alijenga kwa gharama kubwa halina mantiki kabisa
 
Back
Top Bottom