swali kwa wadada na wakaka

Unajua hata familia tunazoishi ni kama nchi kila moja na utawala wake na sheria zake.

Kuleta mwanamke au mwanaume nyumbani, si tu kwa kaka/dada hata baba mwenye familia mwenyewe haruhusiwi kuleta mwanamke nyumbani na kulala naye hata kama ni mjane. Apige mechi za mchangani aje nyumbani mwepesi. Kama atamleta huyo mwenzi wake aje kama mgeni lakini si kupiga mechi nyumbani vinginevyo amuoe na familia imkubali kama member mpya wa familia. The same applies kwa mama mwenye nyumba.

Sasa hawa karumekenge wengine, hata kama hakuna wazazi na mnaishi kisela na kila mtu anajitegemea na ana maisha yake binafsi kuja kupigia mechi home, mimi nachukulia like abormination to familyhood. Haijalishi waliopo ni wadogo au wakubwa wala jinsia.Tena kwa mtu above 30 na ana kazi kama hapendi kulala gesti basi asifanye kabisa maana kupanga ni kuchagua.
Ataruhusiwa kuja kulala nyumbani na mkewe au mumewe tu.

Kama familia yenu wenyewe mtaidharau na kuifanya danguro nani ataiheshimu? Afu mzae watoto wawe vicheche kuanzia vidudu mtasingizia TEHAMA?

Its a big NO kwa member yeyote kupigia mechi nyumbani na mtu ambaye si mkewe wala mumewe. Naona ikifikia point hiyo mtakuwa mmekaribia na kuuza nyumba mgawane urithi.
 

Kami ni mimi,najiandaa kuhama hiyo nyumba!Belivdat
 
mmhh...mimi kaka/wadogo zangu walikuwa wakiingia chumbani na gf zao, yaani natunga safari ya ghafla ili tu nisiwe nyumbani. i couldn't stand it kwa kweli. binafsi bf wangu hakujua hata chumba changu chafananaje.........
 
Boss mara nyingi inategemea relationship iliyopo katika ya hao ndugu wawili kuna wengine hiuwa unakuta hawana time kabisa wala hawataki kufuatilia leo sister kaja na nani au michongo yake ikoje but mara nyingi sana huwa inakuwa mbinde pale sister akija na kidume the truth of the matter ni wachache sana wanaoweza kuvumilia na kuchukulia kawaida kuwa dada yao nae ana mahitaji kama ya kwao, vidume vingine lazima patifuke:lol:
 
Ni kweli kama alivyosema mdau hapo juu. Familia zenye heshima na maadili ya kiafrika, si dada wala kaka anaruhusiwa kula mzigo ndani ya nyumba ya familia. Kutembelewa na boyfriend au girlfriend ni ruksa ila mambo yenu fanyeni guest; nyumba ni mahali pa heshima. Imagine umekaa sebuleni na rafiki zako unasikia miguno chumbani kwa kakako/dadako; utajisikiaje??? Hiyo ni nyumba, gheto au dangulo???

Wapo wanaofanya sikatai hila ndo zile nyumba zinaitwa za wahuni.
 
Simply haivumiliki hata kidogo for both side...Mi yaaaan sister awe aniniletea vidume daily tena tofauti tofauti lazima tuelezene ukweli hapa home anapachukuliaje maaana itafika kipindi hata rafiki zake au washikaji zangu wanakuja kugongea room wakiwa na viburudisho vyao...its shame
 
Mkataba wa awali ungekuwa "hakuna yoyote kuleta watu kwa uzinifu wake ndani. Kila mmoja balaa lake amalizane nalo nje" ahsante
 
wewe unaonaje?ni sawa au sio sawa kwa mdada kuwa huru
kubadili vidume home?

BOSS mimi kwa maoni yangu inabidi wote waheshimiane na kuzuia kabisa tabia ya kubadilisha wanaume/wanawake kila siku au kila baada ya siku chache. Vinginevyo heshima kati ya dada na kaka inapungua sana na hata majirani pia heshima mnazostahili kutoka kwao zitashuka kwa kiwango cha kutisha.
 
This is a tough one Boss. But if it comes down to it I think either way it is a no-no. Out of respect for the family home it is better to do whatever it is that you do somewhere else.
 
Mkataba wa awali ungekuwa "hakuna yoyote kuleta watu kwa uzinifu wake ndani. Kila mmoja balaa lake amalizane nalo nje" ahsante

Asante! Nami huo ndo ungekuwa msimamo na mtazamo wangu.
 
Mkuu Boss, wote walitakiwa wasilete mizigo home. Wakaka wakileta basi dada nae alete. It's a fair game!
Cha kujiuliza kwanza wote wanang'ang'ania nini kukaa na wazazi huku wakiwa over 25 ama over 30?
Walitakiwa wawe wameshaondoka makwao wakaanze maisha ya kujitegemea wenyewe.
 
Kama nyinyi ni wakaka...mnaishi na dada yenu mwenye ajira yake
wote ni above 25 au hata above 30
lakini mnaishi nyumba ya familia bila wazazi.....

Mkuu Boss, wote walitakiwa wasilete mizigo home. Wakaka wakileta basi dada nae alete. It's a fair game!

Right on! What's good for the goose is good for the gander.

Cha kujiuliza kwanza wote wanang'ang'ania nini kukaa na wazazi huku wakiwa over 25 ama over 30?

Hawakai na wazazi. Cheki hapo pekundu nilipomnukuu Boss.
 
Right on! What's good for the goose is good for the gander.



Hawakai na wazazi. Cheki hapo pekundu nilipomnukuu Boss.

Hata kama hawakai na wazazi walitakiwa wamwache dada yao na wao watimue wakaanze maisha kivyao na wawe na makwao. Mtoto wa kiume tena uko over 30 unangojea nini nyumbani hata kama wazazi hawapo?
 
Naongelea tamaduni za kiafrika, mwanaume anatakiwa akatafute kwa ajili ya familia, mwanamke anakaa kusubiri kuolewa.
Ndio maana akina baba wengi zamani wasipopata mtoto wa kiume ilionekana kama hana mtu wa kuendeleza ukoo wake.

Kwa nini yeye asiwaache na akaanze maisha kivyake?
 
:tongue::tongue::tongue: Hii ni issue ambayo nadhani kwa dunia ya wenzetu majuu inawezekana bali kwa maadili ya watanzania na Afrika kiujumla, ni cha kushangaza. Muhimu hata wakaka wanahitaji kuwa na staa na dada yao. Wamuheshimu naye awaheshimu. My opinion
 
Boss huo ni ukosefu wa maadili, vijana waliolelewa vyema hawafanyi upuuzi huo, Huwa wanajiheshimu, wanajilinda na maovu na huwalinda wengine.

Mahusiano yoyote ya kingono ama nyumbani ama nje ya nyumbani yakiwa nje ya ndoa ni ukosefu wa maadili.
 
Unamwacha aishi maisha yake....haitakiwi kukusumbua unless una mipango mingine na dada yako huyo!!
 
....Dahhhhh,
kwa post kama hizi ndipo ninapomshukuru mungu kutokuwa na
wadada mapepe aiseee,....'wazimu' wetu huko huko nje....nyumbani heshima na adabu!
 
mi naonaa sio busaraa,kwa kama mnakaa na dada yenu yumbaa ya familia,kuingiza wasichana tofauti tofauti au msichana ambae huna malengo nae kwa baadae,usichopenda wewee jua na wezako hawapendi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…