Swali kwa wanajanvi wanaofahamu hili.

Ikengya

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2013
Posts
614
Reaction score
178
Habarini za wakati huu wadau wa ili jukwaa?

Hivi kwaninini kila waziri anayechuku wizara ya elimu lazima aje na kitu chake cha kushangaza jamii? Je, hii inatokana na kukosekana kwa dira madhubuti ya Elimu?

Kuna baadhi ya matukio ya kushangaza yaliyowahi kufanywa na hiyo wizara chini ya mawaziri tofauti na haya ndo naweza kumbuka.

1: Kufutwa kwa mtihani wa taifa wa form II
2: 1993 Wanafunzi walipanda Form III kwa ufaulu wa wastani wa 14 badala 21
3: Kuacha kutoa vyeti darasa la saba na baaadae kuvirudisha
4: Kufutwa kwa mtihani wa kidato cha II na kuurudisha tena
5: Kufuta mtihani wa darasa la nne na kuurudisha tena
6: Kuunganisha baadhi ya vipindi katika shule za msingi na sekondari eg Physics na Chemistry, History na Geography
7: Kumurundikia mtoto wa darasa la kwanza vipindi lukuki mpaka kushindwa kutimiza matakwa ya KKK (3R)
8: Watu kusomea ualimu wiki tatu.
10: Kuondoa michezo mashule na baadae kuirudisha
Mengine mtaongezea

Hapa tunakosa nini mpaka watu wanavurugavuruga hivi hii elimu ya nchi yetu?
 
Mulugo kuwa waziri wa elimu nalo ni tukio mkuu.
 
Hivi majanga ndo hayo tu
 
Tatizo viongozi wetu vihiyo na wamefika hapo kwa rushwa. Elimu yao ya kuungaunga wategemea efficiency hapo? Hawapo seriuos na wachosumbuka nacho ni vyama vya upinzani na kufisidi nchi tu, masuala nyeti kama elimu na afya tutajiju! Isitoshe, Mr. President sina uhakika kama anafuatilia uwezo wa anayemteua kuwa waziri. Au akipelekewa jina yeye ni kujibu 'pass' tuuu? Inasikitisha sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…