Swali kwa Wanaotaka Kura za Siri: Na hili mtataka liwe siri?

Swali kwa Wanaotaka Kura za Siri: Na hili mtataka liwe siri?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Swali kwa Wanaotaka Kura ya Siri: Hoja kubwa inayotolewa na wale wanaotaka kura ya siri kwenye Bunge la Katiba ni kuwa hawataki watu wajioneshe wanapigia kura wapi kwa sababu inawapa shinikizo kufuata maelekezo ya kichama na pia inaweza ikaleta uhasama dhidi yao. Wanasema kura ya wazi siyo ya kidemokrasia na kuwa watu wataogopa kupiga kura kwani wataonekana kura yao imepigwa vipi; ni bora wapige kura ya siri ili tuone matokeo tu.

Inawezekana vipi kutaka kura za siri lakini wakati huo huo kutaka mijadala ya wazi hata ile ambayo ni ya Kamati?

Sasa swali langu ni je wanaotaka kura ya siri wako tayari pia kukubali baadhi ya vikao vya Bunge la Katiba kuwa vya siri kwa sababu hizo hizo? Ili kwamba wabunge wawe huru kujadiliana na kuchukua maamuzi mbalimbali bila kujionesha mbele ya wapiga kura? Kwamba baadhi ya vikao vya kamati vifanyike kwa siri ili kulinda uhuru wa wachangiaji wake?
 
Hili bunge la Katiba ni Comedy tupuu Wanakula POSHO za bure tu..

EWE MUNGU SAIDIA HII NCHI
 
Mijadala ni lazima iwe ya wazi iliwafuatiliaji wajue kile kinachojiri. Tatizo la kura za siri ni unafiki wa mwanadamu. Mwanadamu wa asili ana unafiki ndani yake. Hilo la kwanza. Lakini la pili ni kwamba kuna watu wanafikiria nafsi zao bafala ya taifa na kwa sababu hiyo wanataka kuwashinikiza wati wengine wakubaliane nao. Kama ingekuwapo demokrasianya kweli kura za wazi isingekuwa tatizo. Lakini shida inakujakwa kuwankuna shinikizo. Kama wakubwa wanasema mtu akipiga kura kinyume na matakwa yao atanyang'anywa kadi ya chama chake ni wazi kuwa huyu mtu hana maamuzi yake. Lakini kura kama ni ya siri mtu atakuwa na uhuru wa kuamua kilr anachokiona ni sahihi.
 
Swali kwa Wanaotaka Kura ya Siri: Hoja kubwa inayotolewa na wale wanaotaka kura ya siri kwenye Bunge la Katiba ni kuwa hawataki watu wajioneshe wanapigia kura wapi kwa sababu inawapa shinikizo kufuata maelekezo ya kichama na pia inaweza ikaleta uhasama dhidi yao. Wanasema kura ya wazi siyo ya kidemokrasia na kuwa watu wataogopa kupiga kura kwani wataonekana kura yao imepigwa vipi; ni bora wapige kura ya siri ili tuone matokeo tu.

Inawezekana vipi kutaka kura za siri lakini wakati huo huo kutaka mijadala ya wazi hata ile ambayo ni ya Kamati?

Sasa swali langu ni je wanaotaka kura ya siri wako tayari pia kukubali baadhi ya vikao vya Bunge la Katiba kuwa vya siri kwa sababu hizo hizo? Ili kwamba wabunge wawe huru kujadiliana na kuchukua maamuzi mbalimbali bila kujionesha mbele ya wapiga kura? Kwamba baadhi ya vikao vya kamati vifanyike kwa siri ili kulinda uhuru wa wachangiaji wake?

Hao wabunge wako pale kama wawakilishi kwa hiyo ni lazima wanachokizungumza wananchi wakifahamu na ndipo watakapoweza kujua jinsi ya kupiga wakati wao ukifika. Ili wasibughudhiwe nao wapige kura za siri. Kumbuka huwezi kuandika minutes za kikao ambacho hukuhudhuria.
 
Wanaoshinikiza kura ya siri ni wale wanaotaka kupiga kura kwa Miongozo yao binafsi badala ya Taasisi wanazowakilisha.

Kila Mjumbe aliepo Bungeni ni Mwakilishi wa ama Chama au Taasisi au kundi fulani, iweje hutaki unaowawakilisha wajue kama umewakilisha kama walivokutuma? Iweje uwakilishe Wafugaji kwenye Bunge la Katiba halafu kwenye upigaji kura upige kwa kificho as if unajiwakilisha mwenyewe au familia yako?
 
babu wa shamba, hizo kura iwe za siri au za wazi ni mradi wa watu kujineemesha and coz watz wengi ni bendera fuata upepo(remember issue ya dowans tulivyoishabikia na sasa inavyokula kwetu) ndio maana tunaona vurugu zote hizi. ccm wanajua kuwa ikipitishwa kura ya siri bajeti yao itabidi iongezeke coz wanafiki watakuwa wanajipangia dau tu ili wawasapoti kwenye misimamo yao tofauti na ikiwa kura ya wazi ndio hivyo kutishana utanyang'anywa kadi ya uanachama ukipingana nao.hata hao wapinzani wananunulika tu mbele ya pesa, kitakachomatter ni dau kiasi gani ccm wanatoa. hiyo itakuwa determined na ushawishi wako au ubishi wako lakini tusijidanganye kuwa kura ya siri ndio itageuza mioyo ya wanafiki kusimama upande wa wananchi. me kinachonikera kwenye hii proces yote ya katiba mpya its like tunatengeneza mfumo wa muungano tu na vitu vingine si hoja za msingi.kama tungetaka kutengeneza muundo wa muungano isingepaswa kutmia mabilioni ya shilingi ilikuwa ni kuitisha kura ya maoni kuwauliza wananchi ni mfumo gani wa muungano wanautaka then yakaisha.coz nachoona hapo kinachogombaniwa kwenye hiyo kura ya siri au wazi ni kura kwenye mfumo wa muungano.
 
Katika mijadala watu hutoa mawazo yao ambayo yanaweza kuwa tofauti na vile wanavyosema baada ya watu wengine kutoa hoja zao na kuwaconvince kuwa yale mawazo waliyokuwa nayo awali sio sahihi na hiyo ndio itakayompa uhuru wa mjumbe kupiga kura kufuatana na kile anachoamini baada ya mijadala!!!! Kura ya siri inampa mhusika amani kwa kile anachokiamini bila shinikizo la mtu.
 
kura ya siri itapunguza wanafiki.

Hakuna chochote bali ni wizi mtupu. Kuna habari zimezagaa hapa Dodoma kuwa kuna wabunge wengi wana maelekezo kutoka kwa watu waliowapa hela ndefu tu kuwa waunge mkono hoja ya kura za siri na watalindwa. Kura ya wazi inawapa shida NGOs ambazo zimepewa hela nyingi kwa ajili ya kushawishi matakwa ya wafadhili hao yaingizwe kwenye Katiba mpya kama vile Gays and Lesbians societies na the like. Ni matarajio yao kuwa with money every thing is possible but ikiwa kura zitakuwa ni za siri. Kwa wasiojua au wanaojifanya kutokujua wakalaghe bhaho.
 
Back
Top Bottom