Kawe Alumni
JF-Expert Member
- Mar 20, 2019
- 8,685
- 12,000
Mkuu, namba hazina chama, ingependeza uje na takwimu kuthibitisha ulichosema.
Wala usidhani mimi nimekuja na hizi namba kwa minajili ya kuponda...
Umenipa uhalisia upi huo usiokuwa na fact?Mimi sinufaiki na chochote ila nimekupa uhalisia
Maana zile sifa sifa za tumbua tumbua ulikuwa mchezo wa kutafuta sifa za kijinga toka kwa wasojielewaHuu ni muendelezo wa kutoa habari kuhusu utafiti wangu wa kitaalamu huhusu namba za serikali ambazo zinapatikana wizara ya fedha, kwenye report ya serikali ya kila mwaka.
Ni muunganiko wa nyuzi ambazo nimekuwa nikizotoa na kuzipa jina 'Namba zinanuka'
. ‘Namba zinanuka’ – Serikali imechangia kudumaza mifuko ya Hifadhi ya Jamii
. ‘Namba zinanuka’ – kwanini nasema bado uchumi wetu upo kwenye mkwamo...
Ona majibu ya Pimbi.
Itakuwa hata tengua teua ni sababuMaana zile sifa sifa za tumbua tumbua ulikuwa mchezo wa kutafuta sifa za kijinga toka kwa wasojielewa
Gharama za mshahara zinapanda Kwasababu kila mwaka kuna ajira mpya
Unajuwa mara ya mwisho kuajili ni lini?Gharama za mshahara zinapanda Kwasababu kila mwaka kuna ajira mpya
You might have a point... lakini kumbuka hayaJust adding on your point ... .... .. Pamoja na ajira mpya wafanyakazi wengi wanapanda madaraja ooops (grades) hivyo lazima gharama zinaongezeka. Ingekuwa bora ukatuwekea idadi ya wafanyakazi wakati wa zoezi la wafanyakazi hewa na idadi yao hivi sasa. Bila kusahau ajira mpya kwenye sehemu mbalimbalia ambazo hazikuwepo.
Unajuwa mara ya mwisho kuajili ni lini?
Unazungumzia hizi ajira za kutangaza karibu na uchahguzi..!!? Uwe mkweli ndugu..!!! Intake za kutosha toka vyuo mbalimbali hawajaajiriwa muda sasa...Mkuu tembelea wavuti wa utumishi kila siku ajira zinatangazwa na watu wanaajiriwa tatito nyie mkinunua bando mnakimbilia Instagram
Labda anamaanisha ajira za nyuma ya pazia,kuhusu takwimu tunalazimika kumpa muda ili atuletee zinazoeleweka.Hili jibu lako ni fact ama opinion?
Hebu njoo na takwimu ambazo zina justify ulichokisema. Vinginevyo labda unatufurahisha.
Halafu labda tunaishi Tanzania tofauti sana, unavosema suala la ajira mpya kwenye huu utawala.
KabisaGharama za mshahara zinapanda Kwasababu kila mwaka kuna ajira mpya
Kabisa
Na pia kuna watumishi wa kada tofauti wamepandishwa madaraja kwa kipindi hiki cha miaka4,
kumekua na uboreshaji wa utendaji uliopelekea kuboresha au kuanzishwa vitengo na idara mpya serikalini ambazo zimeongeza waajiriwa pia
Na kuna ulipwaji wa stahiki za watumishi ikiwa ni pamoja na likizo, malimbikizo, uhamisho na kadhalika.
Ukiwauliza wizara husika watakupa majibu sahihi
You might have a point... lakini kumbuka haya
1. Ajira ilisimamishwa
2. Madaraja yalisimamishwa
HIYO EFFECT YA WAFANYAKAZI HEWA NA WA VYETI FEKI, UMEIONA KWEYE GRAPH? Kwa maelezo uliyoyatoa, nilitegemea graph ipande, ifike mwaka wa kuondolewa wafanyakazi hewa na wa vyeti feki, at least kuwe na significant drop ya gharama, then ipande kwa uliyoyasema...
Ulivyoongea ni as if baada ya kutoka walioondoka, wakaajiriwa wapya wa ghara ile ile kama walioondolewa na siku hiyo hiyo walioondolewa...
Kumbuka hili..
Wale wakurugenzi 8 waliotumbuliwa, watano walikuwa replaced emadiately wakati kesi bado inaunguruma... Kwa hiyo, waliotumbuliwa wakawa wanaendelea kulipwa mishahara.. Hii maana yake, kwa nafasi zile 5, mishara miwili ilikuwa inalipwa kwa nafasi moja... aliyetumbuliwa na mpya... THIS WENT ON FOR A YEAR.. na watumbuliwa wakaja lipwa..!!! UFAHAMU TU KWAMBA PARTLY, MISHAHARA ILIPANDA KWA SABABU YA MAAMUZI YASIYOFUATA TARATIBU TULIZOJIWEKEA
Mataga ya uvccm yakikujibu unambie.Huu ni muendelezo wa kutoa habari kuhusu utafiti wangu wa kitaalamu huhusu namba za serikali ambazo zinapatikana wizara ya fedha, kwenye report ya serikali ya kila mwaka.
Ni muunganiko wa nyuzi ambazo nimekuwa nikizotoa na kuzipa jina 'Namba zinanuka'
. ‘Namba zinanuka’ – Serikali imechangia kudumaza mifuko ya Hifadhi ya Jamii
. ‘Namba zinanuka’ – kwanini nasema bado uchumi wetu upo kwenye mkwamo?
Leo ntauliza tu swali la kichokozi baada ya kupitia wage bill ya serikali kuanzi mwaka wa fedha 2016 mpaka 2019.
Nilichogundua ni kwamba, wage bill inakuwa kubwa siku hadi siku, haiakisi kitendo cha serikali kutimua wafanyakazi hewa maelfu na kitendo cha kutokuongeza mishaara kwa watumishi wa umma.
Ki nadharia, kitendo cha kuondoa wafanyakazi hewa na wenye vyeti feki, pamoja na kutoongeza mishaara kungetosha kabisa kuwa kunapunguza wage bill ya serikali. Sasa tunavyoona serikali imefanya hayo yote na bado tunaona wage bill inaongezeka, lazima tuhoji, Je, nini kinasababisha hii wage bill kupanda mwaka hadi mwaka?
View attachment 1490972
Year 2016 2017 2018 2019Wages, salaries, and employee benefits in Tzs '000 8,783,734,521 8,652,125,857 10,129,046,518 10,927,828,010 % change N/A -1.50% 17.07% 7.89%
Ukiangalia kwa makini hiyo chart hapo juu, utagundua kwamba, kutoka mwaka wa fedha wa 2018 mpaka 2019, wage bill ime shoot kwa takribani asilimia 24.96% (Kutoka Trillioni 8.6 mwaka wa fedha 2017, mpaka Trillioni 10.9 mwaka wa fedha 2019)
Unakaa ukijiuliza, je sababu haswa ya serikali kutokuongeza watumishi mishahara ilikuwa ni ipi, kama bado wage bill inaendelea kupanda mwaka hadi mwaka?
Kwa nnavyoona inawezekana kuna mismanagement fulani ambayo mimi na wewe hatuijui, labda serikali siku moja watoke kidedea kutujibu hili swali la ni kwanini pamoja na hatua zote za 1) Kuondoa wafanyakazi hewa, 2) Kutumbua wenye vyeti feki, 3) Kustopisha kuajiri kwa miaka zaidi ya mitatu, 4) Kustisha ongezeko la mishaara kwa watumishi wa serikali, lakini bado wameshindwa kudhibiti ongezeko kubwa la wage bill ambalo linaonekana wazi kwenye namba za serikali na kwenye report za kibajeti.
Kuna nini haswa kinaendelea????? Au ndo ule usemi wa wataisoma namba unatimia?
Uzi Tayar.
N. Mushi
Ni kweli lakini hata yule mbunge wenu alisema mmetoa ajira elfu 42 na laki nane kwa hesabu zenu za kuzimuGharama za mshahara zinapanda Kwasababu kila mwaka kuna ajira mpya
Huyu jamaa sijawahi kumuelewa hata siku moja,anapost kitoto Sana, amesahau jf ni home of great thinkersBora wewe umeuliza, maana na mimi nlikuwa nahisi hivo hivo.. jamaa amejaa ushabiki sana, kila kitu anadhani ni siasa. Anasahau namba hazina chama
Akikujibu niite.. serikali walistopisha kuajiri kwa miaka kama mitatu, hizi ajra zilizotolewa mwaka mmoja na nuzu kuelekea uchaguzi, ni ajira za kuombea kura.Unajuwa mara ya mwisho kuajili ni lini?
Tanzania ipi unaizungumzia mkuu? Tuanzie hapo kwanza maana inawezekana tunaishi nchi mbili tofauti.Kabisa
Na pia kuna watumishi wa kada tofauti wamepandishwa madaraja kwa kipindi hiki cha miaka4,
kumekua na uboreshaji wa utendaji uliopelekea kuboresha au kuanzishwa vitengo na idara mpya serikalini ambazo zimeongeza waajiriwa pia
Na kuna ulipwaji wa stahiki za watumishi ikiwa ni pamoja na likizo, malimbikizo, uhamisho na kadhalika.
Ukiwauliza wizara husika watakupa majibu sahihi