Swali la Ugomvi: Mawaziri na Vikao vya Bunge la Katiba - Itakuwakuwaje?

Swali la Ugomvi: Mawaziri na Vikao vya Bunge la Katiba - Itakuwakuwaje?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Huu mchakato nilishadokeza kuwa ni mchakato mbovu; hapa najaribu kuonesha jambo jingine. Mawaziri Wote na Manaibu Wao ni Wabunge wa Bunge la Katiba. Hapa nazungumzia Mawaziri wa Serikali ya Muungano na wale wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar! Tofauti na Bunge la Kawaida, hawa hawaingii kama wasemaji wa serikali na hawatosimama kuulizwa maswali na wabunge na watoe majibu. Kwenye Bunge hili wanaingia kama wajumbe wengine tu na wakiwa na sauti kama wabunge wengine.

a. Pamoja na Mishahara yao ya Mawaziri na Ubunge (sijui kama wanalipwa yote) watalipwa pia posho za Bunge hili (kama Rais atakuwa ameridhia). Sawa?

b. Kwa sababu Bunge hili litakuwa na vikao karibu vya miezi mitatu (sijui litakuwa linakutana kwa mfumo upi tusubiri) lakini vyovyote ilivyo Mawaziri na Manaibu Waziri itabidi na wao wajitahidi kuhudhuria vikao hivi kwani ukijumlisha utaona kuwa peke yao ni karibu 1/6 ya bunge la Katiba!

c. Vikao vya Baraza la Mawaziri itabidi vipangwe kuzingatia Bunge la Katiba au vikao vya Bunge la Katiba itabidi viaccommodate vikao vya Baraza la Mawaziri (ambavyo kwa kawaida hufanyika kila wiki). Na kwa vile Bunge linafanyika Dodoma, Mawaziri nao watakuwa wanakutana vipi na Marais wao; kumbuka kuwa hata Waziri Mkuu ni mjumbe wa Bunge la Katiba!

Hapa inabidi kujiuliza mfumo wa utendaji kazi wa serikali zetu utakukuwa vipi wakati wa Bunge hili la Katiba? Au kutakuwa na 'excuses' nyingi za hawa kutohudhuria lakini watakuja siku ya kupiga kura?

Mweh "magenius wetu" hawa...
 
Mmh, haijakaa vizuri. Waziri wamekua na sura nyingi mno.

Lakini pia, kama kuna jambo la maana haitazuia wako kukutana hasa baraza la mawaziri, si kuna saa huwa linafanyika hadi usiku?

Ila sema kwa miezi yote hiyo 3, wizara zitakuwa hazina watendaji au watapeana zamu? Na wakipena zamu, ni kumnyima fursa waziri kuhudhuria.

Tatizo langu ni moja tu, hakuna kitu cha maana nachoona chaweza kufanyika under jeikei regime, naamini kabisa 'ukikata kichwa nyoka, kinachobakia ni kamba' Tatizo la nyoka ni kichwa chake, kwingine ni kamba tu.
 
mawazo yako yanalogic,mtu pekee wa kujibu ni PM nadhani kama msimamizi mkuu wa shughuri za serikali anapaswa kujibu ni namna gani wamejipanga kuwatumikia watanzania katika kipindi hiki cha Bunge la katiba.Nawasilisha.
 
Kwenye Bunge la kawaida WAziri Mkuu na Kiongozi wa Upinzani wana kipaumbele katika kuzungumza; je kitazuia nini kwenye Bunge la Katiba viongozi hawa kupewa ujiko zaidi kuliko wajumbe wengine?
 
mwanakijiji ilikuwa zamani, saivi umechuja, umefulia, huna jipya.
 
Kwenye Bunge la kawaida WAziri Mkuu na Kiongozi wa Upinzani wana kipaumbele katika kuzungumza; je kitazuia nini kwenye Bunge la Katiba viongozi hawa kupewa ujiko zaidi kuliko wajumbe wengine?

nani amekwambia watapewa ujiko zaidi? acha utabiri wa nyota, umeambiwa watakuwa na hadhi ya wabunge wengine wa kawaida. sema kwa kuwa wewe uko nje ya nchi huelewi ya huku ndio mana unabahatisha bahatisha na kubuni
 
Huu mchakato nilishadokeza kuwa ni mchakato mbovu; hapa najaribu kuonesha jambo jingine. Mawaziri Wote na Manaibu Wao ni Wabunge wa Bunge la Katiba. Hapa nazungumzia Mawaziri wa Serikali ya Muungano na wale wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar! Tofauti na Bunge la Kawaida, hawa hawaingii kama wasemaji wa serikali na hawatosimama kuulizwa maswali na wabunge na watoe majibu. Kwenye Bunge hili wanaingia kama wajumbe wengine tu na wakiwa na sauti kama wabunge wengine.

a. Pamoja na Mishahara yao ya Mawaziri na Ubunge (sijui kama wanalipwa yote) watalipwa pia posho za Bunge hili (kama Rais atakuwa ameridhia). Sawa?

b. Kwa sababu Bunge hili litakuwa na vikao karibu vya miezi mitatu (sijui litakuwa linakutana kwa mfumo upi tusubiri) lakini vyovyote ilivyo Mawaziri na Manaibu Waziri itabidi na wao wajitahidi kuhudhuria vikao hivi kwani ukijumlisha utaona kuwa peke yao ni karibu 1/6 ya bunge la Katiba!

c. Vikao vya Baraza la Mawaziri itabidi vipangwe kuzingatia Bunge la Katiba au vikao vya Bunge la Katiba itabidi viaccommodate vikao vya Baraza la Mawaziri (ambavyo kwa kawaida hufanyika kila wiki). Na kwa vile Bunge linafanyika Dodoma, Mawaziri nao watakuwa wanakutana vipi na Marais wao; kumbuka kuwa hata Waziri Mkuu ni mjumbe wa Bunge la Katiba!

Hapa inabidi kujiuliza mfumo wa utendaji kazi wa serikali zetu utakukuwa vipi wakati wa Bunge hili la Katiba? Au kutakuwa na 'excuses' nyingi za hawa kutohudhuria lakini watakuja siku ya kupiga kura?

Mweh "magenius wetu" hawa...

1. kumbuka makao makuu ya nchi yapo dodoma, hivyo vikao vya baraza la mawaziri vitafanyikia dodoma
2. mwenyekiti wa baraza la mawaziri ni rais au makam wa rais, kwa hiyo waziri mkuu kuwa mjumbe wa bunge la katiba haina madhara wala haina uhusiano wowote na baraza la mawaziri
 
MM mbona unaumiza kichwa, hawa wanahitajika kule kwenda kupiga KURA na kuhalalisha posho zao ili KATIBA ambayo wameshaipanga ipite. Hawaendi kujibu maswali wala kuongoza kitu. Kwahiyo usiumize kichwa kutafuta majukumu yao ama uwakilishi wao....
 
mwanakijiji ilikuwa zamani, saivi umechuja, umefulia, huna jipya.
We Kiumbe una matatizo sana. Si uchangie tu hoja ya mtu!!!!!!!!!!? Kuna haja gani ya kumjadili mtu badala ya kujadili hoja yake? Kama yeye alikuwa zamani mbona wewe hujawahi kuwa na lolote toka zamani na mpaka sasa?Natamani nikutukane sema sio tabia yangu. Wewe una utaifa gani? Mbona hoja ya Malecela sijakuona ukisema cha maana? Pumba tu!!!!!!!
 
Mwanakijiji unayo hoja.tujifunze kujibu hoja
 
1. kumbuka makao makuu ya nchi yapo dodoma, hivyo vikao vya baraza la mawaziri vitafanyikia dodoma
2. mwenyekiti wa baraza la mawaziri ni rais au makam wa rais, kwa hiyo waziri mkuu kuwa mjumbe wa bunge la katiba haina madhara wala haina uhusiano wowote na baraza la mawaziri
uwa nafikiria upeo wako wa kufikiri, sijui wakati mwingine upeo wako upo kwenye foleni umesimama? mbona unapenda kuharibu hoja, njoo na hoja zako kisha tuziangalie. hivi una uhakika makao makuu ya nchi yapo dodoma kweli? ni lini yamehamia huko? mimi najua yapo dar maana ndio serikali ilipo.
 
Back
Top Bottom