Swali la w/end . . . !!

Kongosho,sifa na heshima bado ni ujinga.Nasema hivyo kwa sababu,hata heshima au sifa inatofautiana kutoka jamii moja au nyingine ndo maana hao uliotolea mfano nao wana mtazamo wao na kuna wakati inayodhaniwa ni sifa au heshima inaweza isiwe chochote au kuwa kinyume,lakini utu ni kwa kila mwanadamu hautokani au hauthamanishwi na mtazamo wa jamii yoyote!
 
Last edited by a moderator:
Kama alivyosema SnowBall,

Haya mambo yanategemea utaratibu wa familia pale yanapofanyika mbele ya wanafamilia tu. Ila yanapofanyika kwa wanajamii wengine basi lazima yaangalie taratibu za hiyo jamii na mategemeo ya wanajamii.

Kwangu mimi, Bibi DC huniita kwa jina langu halisi wakati wote. Hili liliwahi kumletea kasheshe kutoka kwa mgeni aliyetutembelea kutoka kijijini kwetu. Alishindwa kuvumilia hadi akamuuliza kwamba kwa nini ananikosea heshima kiasi hicho?

Pia mara moja moja (lakini katika utani) wanangu huniita kwa jina langu....Ila siyo katika formal address!


Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
Heshima kwako babu Dark City,angalau inaonekana hakuna tabu kuitwa jina lako.Ila inashangaza kuona mtu anatoka povu kisha ameitwa jina lake!Kazi ipo!
 
Last edited by a moderator:
Eiyer, kwani morals ni nini??
 
Last edited by a moderator:
Heshima kwako babu Dark City,angalau inaonekana hakuna tabu kuitwa jina lako.Ila inashangaza kuona mtu anatoka povu kisha ameitwa jina lake!Kazi ipo!


Ahsante sana Mkuu Eiyer,

Binafsi nafurahi sana kuitwa jina langu la kwanza. Ila nakereka na watu wanaoshindwa kutumia majina ya watu vizuri. Kwa mfano, kuna watu wamezoea na wanatumia vibaya majina ya watu. Jambo ambalo linasababisha usumbufu kwa watu ambao hatupendi upuuzi wa namna hiyo.

Mfano: Mtu ni James Lyamatu...Huyu ni Doctor (Dr au Prof). Ni kawaida sana kusikia baadhi ya watu wakimwita Dr/Prof James.....na wengine kumwita bila title, Lyamatu....Hii inakera sana. Pia wapo watu ambao wengine ni member humu ndani wanakera kwa kujiaddress kwa vyeo vyao. Utasikia mtu anasema kuwa, "mimi ni Dr, Prof. au Mheshimiwa James Lyamatu". Wakati mwingine wanatoa utambulisho wa namna hiyo mbele ya watu kutoka mataifa tofauti!

Ukiniita vizuri tu, ....James naomba unisaidie kitu hapa....nijisikia furaha sana!!


Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:


Eiyer my kid brother... Nimependa sana majibu haya, naamini kwa mchango huu na mingine iliyofuata walau umepata jibu ni kwanini haistahili.

Hata hivo kuna special cases ambazo nazo zimegusiwa hapo na Kongosho... Na kuna families twatumia sana majina, for instance mimi ni mama wa watoto wawili, but familia yetu to date hatuitanagi mama fulani, siku zote naitwa kwa jina langu halisi na bado haimpi ruhusa ya mtoto wangu kuniita jina langu.

Saizi nimekuwa mtu mzima sometimes naweza mpigia mamangu simu na kumuita fulani binti fulani... Or wewe mke wa marehemu flani, huku nikifuatilia na ujembe wa utani kama vile njia moja wapo tu ya kumchangumsha. BUT when it comes to the end of the day lazima nimuite mama na life goes on huku nikiendelea kumpa heshima yake.
 

Ahsante sana ndugu yangu AshaDii,

Nikishaona michango yako napata amani sana. Tatizo lako kubwa ni kwamba ukimaliza kuchangia tu, nahisi kama thread imefika mwisho!!

Hata hivyo, pengo la michango yako huwa ni kubwa sana....!

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
Ahsante sana ndugu yangu AshaDii,

Nikishaona michango yako napata amani sana. Tatizo lako kubwa ni kwamba ukimaliza kuchangia tu, nahisi kama thread imefika mwisho!!

Hata hivyo, pengo la michango yako huwa ni kubwa sana....!

Babu DC!!

hahaha! Mzee wangu mzima wewe?

Why iwe mwisho? mbona mara nyingi huwa twajadili topics hata pages? lol On a serious note; I appreciate your everlasting acknowledgment... I am humbled.
 
hahaha! Mzee wangu mzima wewe?

Why iwe mwisho? mbona mara nyingi huwa twajadili topics hata pages? lol On a serious note; I appreciate your everlasting acknowledgment... I am humbled.

Sijambo dada yangu...

Naendelea kufurahia hadithi za wajukuu!!

Bora siku hizi unapata pata nafasi ya kutembelea tembelea jamvini...Usirudie kupotea tena...Sawa AshaDii??

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
Sijambo dada yangu...

Naendelea kufurahia hadithi za wajukuu!!

Bora siku hizi unapata pata nafasi ya kutembelea tembelea jamvini...Usirudie kupotea tena...Sawa AshaDii??

Babu DC!!


Kwa heshima yako sirudii tena! lol, na ikitokea nakutwangia kukwambia nimekwama!
 
Kwa heshima yako sirudii tena! lol, na ikitokea nakutwangia kukwambia nimekwama!


Poa kabisa ADii,

Yaani natamani nimwombe Invisible anipe kazi ya kutunza attendance register ili niwe naita majina na kugundua watoro wote!!

I hope hutakuwa mtoro tena....!!

Sasa mbona hukututajia hilo jina lako ambalo huwa unaitwa huko nyumbani kwako...lol???

Babu DC!!
 


Mkuu Maxence Melo ulisema katika ile interview yetu ambayo upo so busy kuweza imalizia kuwa mnahitaji watu wa kujitolea... Naomba msome Mzee DC hapo juu, I think umepata mmoja wapo... lol

Niko kupiga debe hapa Mzee... lol, hua naitwa hivo hivo Asha, almaarufu kama dada Asha.
 
Last edited by a moderator:


Ahsante sana dada AshaDii, a.k.a Da Asha!!

Nimefurahi kusikia hivyo....Hata mie Bibi DC huniita Dii!!

Sasa mbona umenichanganyia madesa.....Nilimwongelea Invisible halafu wewe ukanisemea kwa Max!!

Hivi kumbe mmeshindwa kumaliza mahojiano...lol??

Mwanao akikuita Da Asha unachukia??

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:

Unajua mzee mahojiano yale kwenye ile interview yalinifanya kuweza mfahamu vema zaidi mhojiwa kwa kiasi fulani. Na huyo ndio nilikuwa nawasiliana naye kwenye thread 101. Nimemzunguzima Max for walau naweza piga debe sababu aligusia kwa kina hali upande wa Invisible ni ngumu kujua pa kuanzia. Naamini once imepokelewa na Max, yeye anaweza ifikisha kwa Invisible, wewe hapo unaonaje?

Mwanangu wa kike yupo mischievous, na yupo so lovingly charming tena basi anakuwa kama mgomba (waswahili husema) lol. Sababu nilimzaa so young yupo more like a kid sis than a daughter. Siku moja aliwahi niuliza ni lini ataanza kuniita dada Asha? And i was like "ukome"! I will always be your mother... lol BUT still she is so naughty sometimes ananiita Da Asha hasa kama kaniudhi na nina hasira.
 

Heshima kwa babu;

Wadau hebu jaribuni hii kitu "The Construction of Social Reality/ The Social Constructionism" (Luckman & Berger; 1966) ina insights flan ambazo zaweza toa one among the perspectives
 
im proud of u pacha!
 


Ndo maana nikasema toka mwanzo kwamba ni raha sana kucheza na watoto wanapokuwa wadogo kwani wakishakua wanaanza kufuata mambo ya protokali!!

Kwa wajukuu ndo usiseme....Kwa mtu ambaye hawajawahi kuwa na mtoto wa kwake mwenyewe....haya mambo ni magumu kuelewa kabisa!!

Wabarikiwe wazazi wote wanaolea vizuri bila kukimbia majukumu!!

Babu DC!!
 
Nina mtoto wa kiume wa miaka minne sasa, huyu bwana hata kabla hajanyoosha maneno alikuwa anatuita mimi na dady wake kwa majina yetu, mimi nikapambana na hilo mapema so now ananiita mama, but hubby yeye anadai anapenda mwanae anavyomuita hivyo kwani anadai inaweza kumsaidia kiusalama incase amepotea mahali na vitu kama hivyo

huyu dogo anamwita baba ake kwa jina lake mahali popote na akiwa na mtu yoyote, sometimes ananiita mimi pia kwa jina langu, sion tatzo sana na nikiangalia hii naona mwanangu amekuwa na ukaribu na urafiki fulan uliozid na baba ake na nahisi ni kutokana na hilo

wanaotuzunguka, wameshangaa wee, mwishoe wamezoea...................
 
majina ni kirahisisho cha kurejea tu mtu fulani,mimi kwa watoto wangu ni mama tough wanalijua jina langu vizuri tu!marafiki zangu napenda waniite jina langu la kwanza lakini mume wangu sipendi aniite jina langu,akitumie pet name yangu ndo naona ni nzuri zaid.ndo mana sina hakika sana na kusema ni sahihi mtu yeyote kukuita jina lako,lakini hii sasa ni tofauti na wale wanaotumia vyeo au elimu zao kwa mfano kujitambulisha ,tena inakera zaidi inapokuwa ni katika mazungumzo.things like,my name is Prof Kibakuli Kimejaa,its too rude!and immature to be frank.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…