What????An by the way,where were u?
Heshima kwako babu Dark City,angalau inaonekana hakuna tabu kuitwa jina lako.Ila inashangaza kuona mtu anatoka povu kisha ameitwa jina lake!Kazi ipo!
Kuna kitu nadhani umekichanganya kwenye hii mada pengine ndicho kinabeba muktadha mzima wa neno 'heshima'..Na kitu chenyewe ni Jamii na hayo unayoita mazoea. Mazoea hayaji tu kama mvua lazima yanakuwa na 'backed up' na maisha ya Jamii husika. Jamii ndio inayoamua nini kikisemwa kitakuwa tusi na nini kikisemwa kitakuwa heshima..Unaweza kwenda kinyume na jamii kwa siku moja lakini huwezi kuishi kwenye jamii ile ile kila siku huku wewe ukienda kinyume na jamii inavyosema na kufikiri.
Mwanangu kuniita Jina langu inaweza kuwa 'heshima mbaya' kwa jamii ambazo zimeamua au zinaona hilo jambo ni dharau. Ni sawa tu shuleni kumuita mwalimu kwa jina lake ilhali wewe ni mwanafunzi wake. Lakini kama 'familia' mnaweza kuwa na utaratibu wenu ambao mmeamua kuufuata na kama mnaweza kuufanya bila kuathiri mitazamo ya wanajamii wengine basi inaweza kuwa sawa kwa mimi mwanangu kuniita tu 'wewe snowball nenda nyumbani unaitwa na mama'..
yaani mwanangu aniite Kongosho???
Kuna wakati ataniita hivyo for fun tukiwa tunataniana lakini sio wakati anani-address siriaz.
Kila kundi la wanajamii wana jinsi ya kuonyesha heshima hizo, jinsi ya kumuita mtu ni mojawapo ya kuonesha heshima.
Kuna wakati nilifanya kazi na mtu wa nchi fulani, siku ya kwanza nilitoka povu, kisa aliniita kwa kidole kinachofuata kidole gumba huku kijanga cha mkono kimetazama juu. Niliona ni dharau sana, lakini yeye akasema ndio wanavyoita kwao na hakumaanisha dharau.
Kwa hiyo, nitajali mwanangu kuniita kwa jina maana heshima inajumuisha jinsi ya kumuita mtu kulingana na tamaduni za kundi husika.
Eiyer my kid brother... Nimependa sana majibu haya, naamini kwa mchango huu na mingine iliyofuata walau umepata jibu ni kwanini haistahili.
Hata hivo kuna special cases ambazo nazo zimegusiwa hapo na Kongosho... Na kuna families twatumia sana majina, for instance mimi ni mama wa watoto wawili, but familia yetu to date hatuitanagi mama fulani, siku zote naitwa kwa jina langu halisi na bado haimpi ruhusa ya mtoto wangu kuniita jina langu.
Saizi nimekuwa mtu mzima sometimes naweza mpigia mamangu simu na kumuita fulani binti fulani... Or wewe mke wa marehemu flani, huku nikifuatilia na ujembe wa utani kama vile njia moja wapo tu ya kumchangumsha. BUT when it comes to the end of the day lazima nimuite mama na life goes on huku nikiendelea kumpa heshima yake.
Ahsante sana ndugu yangu AshaDii,
Nikishaona michango yako napata amani sana. Tatizo lako kubwa ni kwamba ukimaliza kuchangia tu, nahisi kama thread imefika mwisho!!
Hata hivyo, pengo la michango yako huwa ni kubwa sana....!
Babu DC!!
hahaha! Mzee wangu mzima wewe?
Why iwe mwisho? mbona mara nyingi huwa twajadili topics hata pages? lol On a serious note; I appreciate your everlasting acknowledgment... I am humbled.
Sijambo dada yangu...
Naendelea kufurahia hadithi za wajukuu!!
Bora siku hizi unapata pata nafasi ya kutembelea tembelea jamvini...Usirudie kupotea tena...Sawa AshaDii??
Babu DC!!
Kwa heshima yako sirudii tena! lol, na ikitokea nakutwangia kukwambia nimekwama!
Poa kabisa ADii,
Yaani natamani nimwombe Invisible anipe kazi ya kutunza attendance register ili niwe naita majina na kugundua watoro wote!!
I hope hutakuwa mtoro tena....!!
Sasa mbona hukututajia hilo jina lako ambalo huwa unaitwa huko nyumbani kwako...lol???
Babu DC!!
Mkuu Maxence Melo ulisema katika ile interview yetu ambayo upo so busy kuweza imalizia kuwa mnahitaji watu wa kujitolea... Naomba msome Mzee DC hapo juu, I think umepata mmoja wapo... lol
Niko kupiga debe hapa Mzee... lol, hua naitwa hivo hivo Asha, almaarufu kama dada Asha.
Ahsante sana dada AshaDii, a.k.a Da Asha!!
Nimefurahi kusikia hivyo....Hata mie Bibi DC huniita Dii!!
Sasa mbona umenichanganyia madesa.....Nilimwongelea Invisible halafu wewe ukanisemea kwa Max!!
Hivi kumbe mmeshindwa kumaliza mahojiano...lol??
Mwanao akikuita Da Asha unachukia??
Babu DC!!
Kama alivyosema SnowBall,
Haya mambo yanategemea utaratibu wa familia pale yanapofanyika mbele ya wanafamilia tu. Ila yanapofanyika kwa wanajamii wengine basi lazima yaangalie taratibu za hiyo jamii na mategemeo ya wanajamii.
Kwangu mimi, Bibi DC huniita kwa jina langu halisi wakati wote. Hili liliwahi kumletea kasheshe kutoka kwa mgeni aliyetutembelea kutoka kijijini kwetu. Alishindwa kuvumilia hadi akamuuliza kwamba kwa nini ananikosea heshima kiasi hicho?
Pia mara moja moja (lakini katika utani) wanangu huniita kwa jina langu....Ila siyo katika formal address!
Babu DC!!
Kuna kitu nadhani umekichanganya kwenye hii mada pengine ndicho kinabeba muktadha mzima wa neno 'heshima'..Na kitu chenyewe ni Jamii na hayo unayoita mazoea. Mazoea hayaji tu kama mvua lazima yanakuwa na 'backed up' na maisha ya Jamii husika. Jamii ndio inayoamua nini kikisemwa kitakuwa tusi na nini kikisemwa kitakuwa heshima..Unaweza kwenda kinyume na jamii kwa siku moja lakini huwezi kuishi kwenye jamii ile ile kila siku huku wewe ukienda kinyume na jamii inavyosema na kufikiri.
Mwanangu kuniita Jina langu inaweza kuwa 'heshima mbaya' kwa jamii ambazo zimeamua au zinaona hilo jambo ni dharau. Ni sawa tu shuleni kumuita mwalimu kwa jina lake ilhali wewe ni mwanafunzi wake. Lakini kama 'familia' mnaweza kuwa na utaratibu wenu ambao mmeamua kuufuata na kama mnaweza kuufanya bila kuathiri mitazamo ya wanajamii wengine basi inaweza kuwa sawa kwa mimi mwanangu kuniita tu 'wewe snowball nenda nyumbani unaitwa na mama'..
Unajua mzee mahojiano yale kwenye ile interview yalinifanya kuweza mfahamu vema zaidi mhojiwa kwa kiasi fulani. Na huyo ndio nilikuwa nawasiliana naye kwenye thread 101. Nimemzunguzima Max for walau naweza piga debe sababu aligusia kwa kina hali upande wa Invisible ni ngumu kujua pa kuanzia. Naamini once imepokelewa na Max, yeye anaweza ifikisha kwa Invisible, wewe hapo unaonaje?
Mwanangu wa kike yupo mischievous, na yupo so lovingly charming tena basi anakuwa kama mgomba (waswahili husema) lol. Sababu nilimzaa so young yupo more like a kid sis than a daughter. Siku moja aliwahi niuliza ni lini ataanza kuniita dada Asha? And i was like "ukome"! I will always be your mother... lol BUT still she is so naughty sometimes ananiita Da Asha hasa kama kaniudhi na nina hasira.
majina ni kirahisisho cha kurejea tu mtu fulani,mimi kwa watoto wangu ni mama tough wanalijua jina langu vizuri tu!marafiki zangu napenda waniite jina langu la kwanza lakini mume wangu sipendi aniite jina langu,akitumie pet name yangu ndo naona ni nzuri zaid.ndo mana sina hakika sana na kusema ni sahihi mtu yeyote kukuita jina lako,lakini hii sasa ni tofauti na wale wanaotumia vyeo au elimu zao kwa mfano kujitambulisha ,tena inakera zaidi inapokuwa ni katika mazungumzo.things like,my name is Prof Kibakuli Kimejaa,its too rude!and immature to be frank.Najua wengi mlio na familia mtakua mnapanga namna ya kuifurahia w/end yenu kwa wale mtakaopata muda wa kufanya hivyo.Wacha leo niwaulize swali hili;Hivi itakuaje pale umefika nyumbani akaja mwanao kisha akakuita kwa jina lako kisha akakusalimu bila kutamka baba au mama,mfano AshaDii au Dark City shikamoo,utachukia?Kama ni ndiyo,kwanini uchukie wakati hilo ni JINA LAKO?Si ndo utambulisho wako?Kama unadhani kutokukuheshimu,kwani heshima iko kwenye jina?Kabla hujaanza kuwaza kama akili yangu ina matatizo,hebu jiulize heshima hasa ni kitu gani na kama inahusiana na jina.Hebu leo tuache kufikiri kimazoea angalau kidogo!!Najua unaweza kushangaa sana,lakini huo mshangao wako ni kutokana na kuaminishwa na jamii kuwa heshima iko kwenye vitu au sifa kama vile,mheshimiwa,bosi,mama,baba,dada,kaka n.k.Hebu nipe mtazamo wako na usipate hasira na kutoa povu kisa mwanao leo kakuita jina lako na kukusalimu!!