Swanglish

FaizaFoxy

Platinum Member
Joined
Apr 13, 2011
Posts
100,246
Reaction score
123,145
Swanglish ni Kiswahili na Kingereza vinapooanishwa vikipenda visipende.

Si ajabu kukumbana na maandiko au maongezi ambayo wengi wetu hujikuta tunaoanisha Kiswahili na Kingereza bila kudhamiria.

Jee, ni wangapi wanafahamu maneno ya Kingereza tunayo wapachikia katika Kiswahili? Ukichukulia kuwa huwa tuna bofya "bombastic" ambazo hata kwa anaeelewa Kingereza lazima akajikumbushe kwenye "dictionary."

Jee, ni wangapi ambao hupachika tu maneno ya Kingereza bila hata kuoana na sentensi wanayoiongea/andika? Hawa huwa hawaelewi na wanapachika tu neno lolote linalowajia iki waonekane wanaelewa au huwa neno hilo wanalielewa kivingine?

Umekumbana na lipi likakufanya ucheke, japo kimoyomoyo? Au umekutana na lipi likakufanya usielewe kabisa ulichoambiwa lakini ukakubali tu mradi yaishe?

Ni sahihi kutumia Swanglish?
 
"okay sawa...."

"still bado....."

wengi tunajisahau kuwa yana maana sawa ila tunayatumia kwa wakati mmoja hapo hapo.
 
Ulimbukeni na kukosa maarifa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sidhani kama upo sahihi. Lugha huzidisha upana wa uelewa na kuna maneno mengi ya Kiswahili yametokana na Kingereza na ukichukulia kuwa elimu yetu (tuliosoma zamani) ilikuwa yote ni English medium, inatuwia vigumu kuwacha kutupia vijineno vya Kingereza japo tunajitahidi isiwe hivyo!

Nnakumbuka mara ya mwisho kumsikikiza Mzee Ali Hassan Mwinyi ilikuwa Ikulu na aliomba radhi kwa kusahau sahau, lakini aliposahu neno alilotaka kuongea kwa Kiswahili alilikumbuka kwa Kingereza.
 
Yet there are men who take (for worship) others besides Allah, as equal (with Allah.: They love them as they should love Allah.But those of Faith are overflowing in their love for Allah.If only the unrighteous could see, behold, they would see the penalty: that to Allah belongs all power, and Allah will strongly enforce the penalty. (Surah Al-Baqara, 165)
 
Ungeandika toka kulia kwenda kushoto ingeleta maana zaidi. Just thinking out loud

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ungeandika toka kulia kwenda kushoto ingeleta maana zaidi. Just thinking out loud

Sent using Jamii Forums mobile app

Qur'an 2:

165. Na katika watu wapo wanao chukua waungu wasio kuwa Mwenyezi Mungu. Wanawapenda kama kumpenda Mwenyezi Mungu. Lakini walio amini wanampenda Mwenyezi Mungu zaidi sana. Na laiti walio dhulumu wakajua watakapo iona adhabu kuwa nguvu zote ni za Mwenyezi Mungu na kuwa Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu! 165
 
Tonaoanisha=tunaoanisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…