Swift Ampiku Rihanna na Kuwa Mwanamuziki wa Kike Mwenye Utajiri Mkubwa Zaidi

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Taylor Swift sasa ndiye mwanamuziki wa kike tajiri zaidi duniani, akiwa na utajiri wa dola bilioni 1.6, akimshinda Rihanna. Mafanikio haya makubwa yanatokana hasa na ziara yake ya "Eras Tour" na umaarufu wa nyimbo zake.
Swift ameendelea kuwa mmoja wa wasanii wenye ushawishi mkubwa katika tasnia ya muziki, akikusanya utajiri huu mkubwa kupitia mauzo ya albamu zake na shoo za moja kwa moja. Hapo awali, Rihanna alikuwa akiongoza kwa utajiri, lakini sasa Taylor Swift anashikilia nafasi ya pili kati ya wanamuziki tajiri duniani, nyuma ya Jay-Z.
Soma, Pia: Forbes 2024: Michael Jordan, JAY-Z, Lebron James, Rihanna watajwa orodha ya Mastaa wenye Utajiri Mkubwa duniani

Mafanikio haya ya Swift yanaonyesha jinsi muziki unaweza kuwa chanzo kikubwa cha utajiri, na kumfanya kuwa mfano wa kuigwa katika sekta ya burudani.
 
Mwanamziki wa kike marekani amempita utajiri tajiri namba moja Africa mashariki na kati mo dewji.

Kweli africa ni masikini isee.
 
Rihana mbona amekuwa white sana au hela zinaleta whiteness?
 
duh noma sana. kweli tanzania ni nchi masikini sana. Anayedaiwa kuwa ndo tajiri nambari moja Tanzania Mohammed Dewji ana utajiri unaokadiriwa kuwa wa dola bilioni 1.5 huku mkata mauno wa US anamzidi kwa kuwa na utajiri wa dola bilioni 1.6.
Ngoja na mimi nipambane nikaingie kwa forbes bilioni dollar list.
 
Taylor swift anajua kutunga na kuimba pia,

Mafanikio yake hayajaja kwa bahati mbaya ila wasanii wa huku Afrika mtu Youtube yake bila aibu kabisa ana upload nyimbo ya kumsifia Samia mpaka unabaki kujiuliza huyu mtu ana akili kweli ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…