Taarab ASLI inavyorudi kwa kishindo

Game Theory

JF-Expert Member
Joined
Sep 5, 2006
Posts
8,546
Reaction score
855
sie wengine tushachoshwa na haya mambo ya dumbing down of original taarab ambayo kwa kiasi kikubwa yanachangiwa na hizi redia stations mpya zilizojaa watangazaji na waandalizi wasiojua kitu kuhusu Taarab wala miziki yetu ya Asli


Naam na hawa chini ndio IKHWAAN SAFAA au al maarufu kama Malindi

 
Yaani umenipa mambo ya kinyumbani mambo ya halisi ya kipwani, ya mziki nyororo wa sauti za vinanda na ghani tamu za akina Rukia Ramadhan, Sihaba Juma. Umenikumbusha wimbo mmoja wa Malindi alioimba Mohd Maulid Machapralla uitwao" mtajirusha wenyewe"
Ngoja nikube ubeti mmoja uonje ladha ya marashi ya karafuu:

Mtajirusha wenyewe, roho na akili zenu.
Kisemeni msizuwe, kilichomtoa kwenu.
Na huku kaja mwenyewe, kajua hamna lenu.
Ya bure yenu mayowe, huyu sasa siye wenu.

kiitikio:
Mtajirusha wenyewe, roho na akili zenu x2
Na mseme, x2 msizuweee kilicho mtowa kwenu.

Yaani raha hizi tunazikosa siku hizi kwa hizi vurugu mechi na matusi wanayoita "modern taarab'.
 
Hapo sijakupa kipande kimoja kitamu cha shairi kilichowahi kuimbwa na kundi hilo na Al marhum ,gwiji, ustadh, Seif Salim katika wimbo wa "kheri Pendo la NdoNdoNdo"

Kheri pendo la Ndo! ndo! la chururu linadhara.
Wacha pupa na vishindo, Mapenzi siyo papara.

shairi:
kusabilia mahaba, siyo kwangu masikhara.
Ukishindwa kuyabeba, itakufika idhara.
Nitakupa habahaba, usije kula khasara.

Halafu hapo unafuata mziki lainiiiiiiiiiii wa vinanda ghani kali kutoka kwa gwiji hilo lililotamba katika enzi za uhai wake kwa tunzi, kuimba na kuweka muzeka.Yaani raha kwenda mbele
 
Naam hapa namsikiliza ABBAS MZEE wa kile kikkundi cha EGYPTIAN anakwambia

Harusi Furaha yaaake....
haina mwanzo wala Mwisho...

Harusi Furaha yakeee
Haina mwanzo wala mwisho...


akh...

halafu ntawasahau vipi CULTURE na usaadhi MUKRIM?
Wazazi wa pande zoote
Huwapamoja kwenye chereko cheroko
 
KAMA UKO dAR BASI KUNA DUKA MOJA LIKO iLALA BOMA naweza kukupa contact lakini pale unakwenda kwa appointment kwa sababu ya msululu wa watu wanaotaka hizi OLDIES
 
Mkuu nimekupata. Mie naona umenifikisha nilipokuwa napataka. Sasa hakuna taarab bali dansi la gambusi. Huyu kijana Mzee Yusuf angejua alifanyalo katika kuua muziki huu nadhani angejuta kuingia katika uga huu. Siku ya kuporomoka kwake kwa umaarufu zinahesabika. Namshauri asikate tamaa kujifunza ni kwa nini wakongwe kama Maulid Machaprala, Chimbeni Kheri na wengineo bado wanavuma? Game nitumie mawasiliano yao
 
mimi mkenya tena mbara lakini napenda raha z pwani
Aidha napenda nyimbo za taarab sana

Nawaomba mashabiki mnipe namna nitaweza kuipata rekodi moja kali sana ya TANGA KUNA RAHA

Hii huniamsha ari ya mahaba na raha

Iwapo mna mmoja wetu atakayenitumia rekodi hii, mie niko tayari kumstiri kiuchumi na gharama \\

Kwa kheri
 
Ukiwaacha malindi kuna wakongwe kama Matano Juma **** Juma bhalo na pete ilo kidoleni iliyomsababishia tifu Zenj akatolewa mkuku yaani ni raha tupu.Mambo ya mod kina bwabwa na welawela vijiwe vyao basi tabu tupu kama si karaha kabisa.HISHIMA ZIRO AIBU TUPU.lakini hata muziki wa dansa kote ni lahaula tupu na ubongo fever.
 
Ukiwaweka kando hao malindi pana majina ambayo ni aghalabu kuyasahau.MATANO JUMA, JUMA BHALO na pete yake iliyomtoa kamasi ZENJ Yaani ni raha tupu. Sio leo mod taarabu za kina bwabwa na kina WELAWELA upuzi kama sio wehu mtupu.hakuna heshima .Taarabu imeenda upogo raha hakuna😡
 
Mbona mnafanya vichekesho? swahili music from Tanzania and kenya from the 1920s to the 1950 , Hivi Tanzania wakati huo ilikuwa au ilijulikana kuwa inakuja ? tuwe wakweli baadhi ya wakati uongo mwingi humletea mtu kufa kifo cha kuhudhunisha.
 
Kuna mtu analoshairi la nyimbo ya ISSA MATONA sina jina lakini kibwagizo chanke ni AJE AHAYA...NA BIBI YAKE HARUUSI NAYE AJE HAPA

Nahitaji mashairi ya nyimbo nzima kama kuna mtu anayo tafadhali hebu nimwagie humu kuna kipande nataka nimtumie mtu ana nisumbua sana
 

EEEEEEE h unanifanza mate yanitoke hio nyimbo leo ni mwaka wa tatu nnaitafuta kwa hamu sijaipata, naomba kama inawezekana ukatutumbukizia humu takarahika pamoja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…