Taarifa juu ya tiba ya Babu

mmmmm " wengi watakuja kwa jina langu wakisema wao ni KRISTO, na watawadanganya wengi........

ni vema watanzania kusoma vitabu vya imani kwani maandiko yanatimia., simamaa pale ulipo usitetereke na Miungu ( kwani kuna MUNGU na miiungu)
 
Pengine hakuna ubishi kuwa watu wanapona kwa kunywa hii dawa. Nasema pengine kwasababu mimi binafsi sijakutana nao. Ubishi uliopo ni kama uponyaji huu unatoka kwa Yesu Kristu au mungu mwingine. Wakristu tuna Utatu Mtakatifu, kwahiyo ninaposema Yesu nawaunganisha Mungu Baba na Mungu Roho pia. Na nimeamua kutumia Yesu ili kutofautisha na hao miungu mingine.

Nimekutana na baadhi ya waislamu wakaniambia wanaenda kwa Babu kwasababu yuko poa hataji jina la Yesu. Yesu anasema katika Isaya 42:8 Mimi ni Mungu nalo ni jina langu. Sitatoa utukufu wangu kwa mtu yeyote.

Ukisikia shuhuda za watu wanasema babu ameniponyesha. Najiuliza anayeponya ni Babu au Yesu. Tunaweza tukasema watu hawajui tofauti as long as imani yao inawatuma kwa Yesu. Lakini babu anatakiwa ampe utukufu Yesu wake maana amekuwa mchungaji kwa miaka mingi kwahiyo hilo neno la Isaya analijua.

Inanipa wakati mgumu anaposema hii ni dawa yangu kama vile nilivyo bold-red. Hakupaswa kusema dawa yake kwasababu kama imetoka kwa Mungu aliyeumba mbingu na dunia angesema hivyo na kumtukuza.

Mtazamo wangu kama wengi wanavyosema tusihukumu na wala babu asilaumiwe but time will tell. Ila ushauri wangu pia kwa wale ambao bado hawajaenda, lakini wana mpango wa kwenda tusikimbilie kwanza kwasababu tu viongozi wetu wanamiminika samunge. Maana je tukigundua hiyo dawa haitoki kwa Mungu tunayemwamini, lile agano tuliloweka na mungu asiyejulikana kwa kunywa hiyo dawa tutatokaje?

Tuombeane jamani na Mungu wetu atusaidie maana anatupenda wote na hataki hata mmoja wetu apotee.
 
Mimi nionavyo,sitaki kuhukumu haraka ninacho jua Mungu anawezakumtumia mtu yoyote kwa wakati wowote kwa jambo lolote,bila kujali chochote,kama aliweza kutumia hata punda asiye mwanadamu,hata babu anawezakutumiwa na Mungu kuleta uponyaji,kama ni nguvu za giza waombaji na wasimame kwenye nafasi zao wazifunge,maana naamini hakuna anaeweza kushindana na Mungu kama jambo halikutoka kwa Mungu ombeni dawa isifanye kazi na Mungu asikia na watu hawatapona..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…