Uchaguzi 2020 Taarifa kwa Umma kuhusu shambulio kwa Mgombea wa Udiwani Kata ya Tungi, Jimbo la Kigamboni

Uchaguzi 2020 Taarifa kwa Umma kuhusu shambulio kwa Mgombea wa Udiwani Kata ya Tungi, Jimbo la Kigamboni

ubongokid

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2017
Posts
2,154
Reaction score
4,184
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU SHAMBULIO KWA MGOMBEA WA UDIWANI KATA YA TUNGI JIMBO LA KIGAMBONI

Ndugu Wananchi;

Uongozi wa Chama Cha Wafanyakazi Tanzania (Tanzania Labour Party-TLP) Wilaya ya Kigamboni unalaani vikali shambulio lililofanywa dhidi ya Mgombea wa nafasi ya udiwani katika KATA ya TUNGI wilaya ya Kigamboni;

Ndugu SETH NICOLAUS MCHAYUNGU

Shambulio hilo ambalo lilifanyika mbele ya watu katika eneo lake la kazi lilifanywa na vijana walioambatana na MGOMBEA udiwani KATA ya TUNGI kupitia Chama Cha Mapinduzi-CCM ambao pamoja na mambo mengine Walichana Bendera ya Chama Cha Tanzania Labour Party iliyokuwa imetundikwa kwenye BAJAJ YA Ndugu SETH NICOLAUS MCHAYUNGU na kuharibu Bajaj yake hiyo ambayo ilikuwa imepaki kituoni kwa ajili ya kupakia abiria huku wakimpatia vitisho vikali.

Tukio hili sio la kistaarabu na linapaswa kukemewa na kulaaniwa na wapenda haki wote nchini na wapenda amani.

Aidha uongozi wa TLP wilaya ya Kigamboni unalisihi sana Jeshi la Polisi kutokuchukulia kwa wepesi taarifa za matukio kama haya yanapofikishwa kituoni kwani tulishangazwa sana na kitendo cha Askari Polisi wa zamu kutokuchukua hatua baada ya kupewa taarifa ya tukio hili.Hii haileti picha nzuri juu ya utayari wa jeshi la polisi kutoa ulinzi kwa watu wote hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi.

Hata hivyo,tunashukuru sana uongozi wa kituo cha miito cha Jeshi la Polisi Makao makuu kwa utayari waliouonyesha wa kufuatilia tukio hili na kuhakikisha kwamba Ndugu SETH NICOLAUS MCHAYUNGU anapatiwa huduma stahiki baada ya kutoa taarifa kituoni hapo.Ieleweke kwamba raia anapokuja kuleta taarifa ya tukio la uhalifu Jeshi la Polisi lisiichukulie kwa wepesi kwani inaweza kuleta madhara ambayo hayakutarajiwa.

Tunatumaini kwamba Jeshi la Polisi Wilaya ya Kigamboni litachukua hatua stahiki dhidi ya uhalifu huu ikiwamo kuwakamata wahalifu hawa na kuwafikisha mahakamani kwa mujibu wa sheria

Aidha uongozi wa TLP wilaya ya Kigamboni umefikisha Taarifa za tukio hili kwa Mkurugenzi wa Tume ya uchaguzi pamoja msimamizi msaidizi wa uchaguzi wa KATA ya TUNGI na ni matumaini yetu kwamba hatua stahiki za kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya Mgombea huyu wa CCM anayeratibu uhalifu.

Tunawashukuru wote waliotupa pole,ushauri na kututia moyo hasa katika kushughulika na adha hii.

Tunapenda kuwajulisha wakazi na wapiga kura wote wa KATA YA TUNGI pamoja na WILAYA ya Kigamboni kwamba tukio hili halitatuvunja moyo wala kuturudisha nyuma,bali limetupa hamasa zaidi,na nguvu zaidi ya kuhakikisha kwamba tunashiriki kikamili katika KUJENGA jamii mpya inayoheshimu haki za Raia.

TLP-UHAI WA MTANZANIA

TUPEANE FURSA,TUWEZESHANE Tanzania ni Yetu Wote

Asanteni sana


Imetolewa na Uongozi wa TLP

Wilaya ya Kigamboni.​
 

Attachments

Halafu wakija kukamata utasikia ni Chadema
 
Mpigwe tu. Mke na mume wakipigana............. kalime.
 
Mkuu hufahamu kuwa yuko kanda ya ziwa akihutubia kwa kisukuma?
Mgombea wa TLP ni jiwe kulingana na tangazo LA Mrema
Uncle Mrema alikunja bilioni kadhaa akaamua isiwe shida. Mgombea anajua njia ya Ikulu ni kama anamsukuma mlevi.
 
Pamoja na kumuunga mkono Magufuli kama mgombea wenu wa Urais?Malipo ni hapa hapa Tanzania!Malipo ya Dhambi ya kuungana na watesi wetu.
 
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU SHAMBULIO KWA MGOMBEA WA UDIWANI KATA YA TUNGI JIMBO LA KIGAMBONI

Ndugu Wananchi;

Uongozi wa Chama Cha Wafanyakazi Tanzania (Tanzania Labour Party-TLP) Wilaya ya Kigamboni unalaani vikali shambulio lililofanywa dhidi ya Mgombea wa nafasi ya udiwani katika KATA ya TUNGI wilaya ya Kigamboni;

Ndugu SETH NICOLAUS MCHAYUNGU

Shambulio hilo ambalo lilifanyika mbele ya watu katika eneo lake la kazi lilifanywa na vijana walioambatana na MGOMBEA udiwani KATA ya TUNGI kupitia Chama Cha Mapinduzi-CCM ambao pamoja na mambo mengine Walichana Bendera ya Chama Cha Tanzania Labour Party iliyokuwa imetundikwa kwenye BAJAJ YA Ndugu SETH NICOLAUS MCHAYUNGU na kuharibu Bajaj yake hiyo ambayo ilikuwa imepaki kituoni kwa ajili ya kupakia abiria huku wakimpatia vitisho vikali.

Tukio hili sio la kistaarabu na linapaswa kukemewa na kulaaniwa na wapenda haki wote nchini na wapenda amani.

Aidha uongozi wa TLP wilaya ya Kigamboni unalisihi sana Jeshi la Polisi kutokuchukulia kwa wepesi taarifa za matukio kama haya yanapofikishwa kituoni kwani tulishangazwa sana na kitendo cha Askari POLISI wa zamu kutokuchukua hatua baada ya kupewa taarifa ya tukio hili.Hii haileti picha nzuri juu ya utayari wa jeshi la polisi kutoa ulinzi kwa watu wote hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi.

Hata hivyo,tunashukuru sana uongozi wa kituo cha miito cha Jeshi la Polisi Makao makuu kwa utayari waliouonyesha wa kufuatilia tukio hili na kuhakikisha kwamba Ndugu SETH NICOLAUS MCHAYUNGU anapatiwa huduma stahiki baada ya kutoa taarifa kituoni hapo.Ieleweke kwamba raia anapokuja kuleta taarifa ya tukio la uhalifu Jeshi la Polisi lisiichukulie kwa wepesi kwani inaweza kuleta madhara ambayo hayakutarajiwa.

Tunatumaini kwamba Jeshi la Polisi Wilaya ya Kigamboni litachukua hatua stahiki dhidi ya uhalifu huu ikiwamo kuwakamata wahalifu hawa na kuwafikisha mahakamani kwa mujibu wa sheria

Aidha uongozi wa TLP wilaya ya Kigamboni umefikisha Taarifa za tukio hili kwa Mkurugenzi wa Tume ya uchaguzi pamoja msimamizi msaidizi wa uchaguzi wa KATA ya TUNGI na ni matumaini yetu kwamba hatua stahiki za kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya Mgombea huyu wa CCM anayeratibu uhalifu.

Tunawashukuru wote waliotupa pole,ushauri na kututia moyo hasa katika kushughulika na adha hii.

Tunapenda kuwajulisha wakazi na wapiga kura wote wa KATA YA TUNGI pamoja na WILAYA ya Kigamboni kwamba tukio hili halitatuvunja moyo wala kuturudisha nyuma,bali limetupa hamasa zaidi,na nguvu zaidi ya kuhakikisha kwamba tunashiriki kikamili katika KUJENGA jamii mpya inayoheshimu haki za Raia.

TLP-UHAI WA MTANZANIA

TUPEANE FURSA,TUWEZESHANE Tanzania ni Yetu Wote

Asanteni sana


Imetolewa na Uongozi wa TLP

Wilaya ya Kigamboni.​
Poleni sana na ccm na watumwa wake walaaniwe.
 
Back
Top Bottom