Taarifa kwa wanafunzi wa uhasibu Arusha

SIMEON KATATANAMA

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2013
Posts
479
Reaction score
277
Kwa wanafunzi wa chuo cha Uhasibu Arusha tembelea www.iaa.ac.tz kupata taarifa muhimu kutoka kwa uongozi wa chuo. Nawasilisha.
 
CHUO CHA UHASIBU ARUSHA
TANGAZO
Kutokana na Chuo kufungwa, Baraza la Uongozi wa Chuo
katika kikao chake cha dharura cha tarehe 03 Mei 2013
kimeagiza wanafunzi wote kuanzia ngazi ya Cheti mpaka
Stashahada ya Uzamili kuzingatia yafuatayo:
1. Kila Mwanafunzi anatakiwa kutuma maombi mapya ya
kujiunga na Chuo.
2. Barua ya maombi hayo ipitishwe kwa Mkuu wa Wilaya
anapoishi mwanafunzi. Kwa mwanafunzi wa Stashahada
ya Uzamili ya Uhasibu barua yake ya maombi ipitie kwa
Mhasibu Mkuu wa Serikali.
3. Katika maombi hayo mwanafunzi anaagizwa kueleza
namna alivyoshiriki katika vurugu za tarehe 24 Aprili
2013.
4. Mwanafunzi awe amekamilisha malipo ya ada iliyobaki
wakati anatuma maombi yake.
5. Mwisho wa maombi ni tarehe 16 Mei 2013.
Maombi yapelekwe kwa anwani ifuatayo:
Mkuu wa Chuo,
Chuo cha Uhasibu Arusha
S. L. P. 2798
Arusha.
08 Mei 2013
 
ungetoa taarifa kamili mkuu wengine tunapata update kwa visimu vyetu vya display ndogo
 
Hayo ni mapito tu, vumilieni kuna siku mtamaliza masomo. Wengine tuliwahi kupewa masharti yanayofanana na hayo, eti barua ipitishwe na mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi wilaya ulikozaliwa. Tulitii tukasoma tukamaliza na maisha yanaendelea.
 
ungetoa taarifa kamili mkuu wengine tunapata update kwa visimu vyetu vya display ndogo

Samahani sana mkuu, hata mie kwa wakati huo sikuwa na access ya kompyuta hila nashukuru kuna mkuu hapo juu katoa maelezo yaliyoko kwenye tangazo hilo.
 

Huu ni uchawi na upunguani kwa kuweka masharti ya kipuuzi kama hayo!

Waache wacheze, hawa waliowafukuza chuoni wameenda kumwaga sumu mpaka vijijini kama ilivyokuwa mwaka 2010 wakati wa uchaguzi mkuu kwani wanafunzi walikuwa makwao, sasa wasubiri kimbunga 2015. Kwa sasa waache wajione wameshinda ila chuki wanayojijengea wataona athari zake 2015.
 
Poleni vijana wa Uhasibu Arusha. Hamkustahili kadha hii, tatizo watu hawataki kukubali walipokosea.
 
pole sana mkuu wa chuo. hivi ile kashfa yako ya uprofesa wa uongo iliishia wap?
 
Ukisikia mambo ya kiseeeeeeeeeeeeeeeeeeeeengeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeerema ndo hayo..viongozi hawajitambui kabisa
 
Siasa zinaanzia pale zilipoishia!! Chuo kilifungwa bila kujua kama wanafunzi walihusika kwa namna gani na vurugu,leo ndiyo wanaambiwa waeleze wenyewe uhusika wao,its a political halloween in the clowns republic,badala ya kurekebisha kile kinachopelekea wanafunzi kuuwawa,tunawakamata wanafunzi kwa kosa la kupinga kuuawa!!!naombeni kwenye fomu zao kuwekwe na sharti la kila mwanafunzi kuthibitisha kuwa yupo tayari kuuliwa na vibaka na polisi,hilo liwe sharti mojawapo la kurudi chuo,ooh God
 
siasa inapoingilia taaluma ni shida kwelikweli....
taratibu za kurudi chuo lazima zi zingatiwe.
 



Na wasi wasi kama taarifa hii haina mkono wa kisiasa na hasa toka kwa RC-Arusha.
Uzuri ni kwamba maamuzi kama hayo yanasaidia sana kuamsha ari ya watu kutetea haki yao.

Kwa wanafunzi wote nawashauri wawe makini kwenye uamuzi watakao chukua katika kutimiza ndoto zao za kielimu kupitia masharti kama hayo hapo juu hasa hili


2. Barua ya maombi hayo ipitishwe kwa Mkuu wa Wilaya
anapoishi mwanafunzi. Kwa mwanafunzi wa Stashahada
ya Uzamili ya Uhasibu barua yake ya maombi ipitie kwa
Mhasibu Mkuu wa Serikali.






Hawa jamaa hapo chini wanafaa kutupa majibu kama walikaa chini na kuja ma madudu hayo!


 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…