Taarifa: waandamana kupinga ujio waBUSH


Hahahaha...I know you're right but they are not wrong either, at least per our constitution. So go on right ahead and wakoromee them at the top of your lungs...you have that right too, don't you? Hey remember it's Friday and it's payday (for some of us)...woopdie doo...Lol
 

Sawa...lakini ukumbuke pia they can't march for every cause. They can't be everything to everybody...that's why in a civilised world we have interest groups....therefore, I support their right to choose whatever cause they wish to protest on.
 

Chuma, the article I posted do not condemn muslims; it says something about a few "fanatics"; while the majority pay the price! It doest not at any definition point to any group. Think very careful, If you will identify yourself in a certain group; as a muslim or a christian; you may feel that pain (self inflicted pain); I always identify myself as a Tanzanian, and religion to me was inherited from my parents, so it becomes irrelevant! The right thing for me is that I believe in God!!
 

Mwanakijiji:

Kuna tofauti kubwa kidogo hapa. Madhehebu ya dini nyingi za kikristu yana hierarchy. Hasa madhehebu yenye asili za Ulaya (Anglikan na Katoliki). Hivyo yasemwayo na viongozi wa dini ya uzito mkubwa sana.

Madhehebu mengi ya kiislamu (Sunni Islam) hayana hierarchy. Katika madhehebu yasio na hierarchy wafuasi wanafuata viongozi wa misikiti au taasisi wanazopenda. Hivyo Njozi, Ponda Issa Ponda na Khalifa Khamisi wana washabiki tu lakini sio wafuasi. Na kuna misikiti hawa jamaa hawakanyagi. Pamoja na Shehe mkuu kutoa maagizo ya kumpokea Bush kwa mikono mitatu, kuna sehemu anajua kabisa hawezi kukanyaga wala kusikilizwa.

Muundo huu wakutokuwa hierarchy unafanana sana na madhehebu mengi ya kikristo yaliopo Marekani ukiondoa Roman Katoliki. Kila pasta ana washabiki wake.

Shia Islam wana hierarchy na maneno ya Ayatolah yana uzito mkubwa sana.

Hivyo hoja zako ni lazima zitilie maanani ni wasikilizaji wa namna gani watakaosiliza ujumbe wako.
 


Na hao few fanatics unawapata pale unapozuia vitu vidogo kama maandamano. Osama kama angepewa nafasi ya kupiga kelele na kuandamana atakavyo katika nchi yake labda asingefika huko alipo.
 
Ukisha kremu kitu bwana kuelewa shida kweli, sidhani kama hawa watu wanaandamana kwa utashi wao, zaidi ya ushabiki na kukremishwa lugha wazizozielewa, sawa sera za marekani zinaumiza wengi duniani, lakini huko nyumbani tunamatatizo mengi sana ya kufanya tuandamane zidi ya hili, mfano.

1.Je wangeandamana kushinikiza balali arudishwe kijibu mashtaka, kufreeze mali ya mafisadi.

2.Wangeandamana kudai katiba mpya.

3.Wangeandamana kupinga matumizi mabaya ya serekali.

4.Wangekusanyika basi na kufanya shuguli za maendeleo

Watu wanajitafutia umaarufu wanawashawishi, then jamaa wanakata mtaa na njaa zote za mchana, du aaaaaaaaaaagh

Mwisho aliyeitisha maandamano ndio anakuwa popula wengine, anony
 
Sawa...lakini ukumbuke pia they can't march for every cause. They can't be everything to everybody...that's why in a civilised world we have interest groups....therefore, I support their right to choose whatever cause they wish to protest on.

You are absolutely right. Mimi nimependekeza. Kwa hivi, hakuna ulazima wowote wa kufuata pendekezo langu. Lakini wakumbuke na mambo mengine yanayogusa maslahi ya nchi basi. langu ni hilo tu.
 
You are absolutely right. Mimi nimependekeza. Kwa hivi, hakuna ulazima wowote wa kufuata pendekezo langu. Lakini wakumbuke na mambo mengine yanayogusa maslahi ya nchi basi. langu ni hilo tu.

Agreed, my brother!!
 
Hapa lets cut the chess right away: waislamu wanaandamana kwa sababu za kidini kwamba Bush anachukia uislamu. Well kama waungwana wengine walivyosema hawa ndugu zetu wana kila haki ya kuandamana kikatiba. And I fully respect their right! Lakini lazima vile vile wajue Tanzania siyo ya waislamu kuna madhehebu mengine na wengine akina Masanja ambao tuna dini zetu za kimila. Kwa hiyo unapopinga Bush asije TANZANIA ni kwamba wewe unayepinga you want to impose your values kwa wengine. Maana siyo wote wanaochukia ujio wake after all anakuja Tanzania haendi msikitini.... Personally, Bush ni capitalist ambaye maslahi ya nchi yake ameyaweka mbele kuliko chochote, (unlike viongozi wetu) lakini siamini kwamba nikichoma bendera ya nchi yake itanisaidia kitu. We need to ENGAGE him and learn his policies and why is he doing what he is doing!

Sitaki kuwaambia waislamu kipi wafanye/au wangefanya, lakini je wanaamini hiyo marginalization wanayoilalamikia itaisha kwa kuandamana? may be yes, may be not. As a heterogenious nation we need to identify elements which unites us more than those which divides us more. Mfano kwa nini hawa wanoandamana, wasinge lobby through JK and US embassy kuwa na mdahalo na Bush (after all anakaa siku nne) wakajaribu kuuliza maswali mbali mbali ambayo wanaona yana manufaa kwao? kama sera za USA dhidi ya waislamu? Jamani matatizo ya siku hizi unaya-solve kwa akili siyo kupigwa na jua la hapa Dar bila vision. na huwezi kuyasolve matatizo bila dialogue. Unafikiri WAMERAKANI WALIKUWA WAJINGA KUMU-INVITE RAISI WA IRAN COLUMBIA University? Ndugu zangu waislamu you should change the way you wage your battles!

Harafu nashangaa hata wasomi wetu wa UD...wameshindwa kweli kuwasiliana na Balozi wa US wakamuomba Bush aje hata Mlimani kwa masaa mawili? It may seem stupid idea, but thats the role of intellectual society than engaging in partisan politics za CCM vs CUF et al.

Kwangu mimi ni Mtanzania as IO said above hayo mengine, ni utashi tuu!

DINI ni kitu chema sana, lakini kikitumiwa vibaya ni POISON ambayo madhara yake ni very fatal sana! As we see around the globe.


Karibu Bwana George na ujisikie Nyumbani!
 
mtakesha hapa na hili yengele!! swali je hawa "kanzu mbovu na kandambili" wamevunja sheria za nchi!!?? jibu kama ni hapana, sasa tatizo liwapi??

mtu anaitwa njozi!! kumbuka hadithi ya mfalme njozi ktk mazungumzo baada ya habari enzi zile utotoni.......

njozi na wenzake ni sawa na al sharpton au jesse jackson hapa "kiwanjani" juu ya masuala ya watu weusi!! si wasemaje wa mtu au taasisi yoyote. ni opportunistics ambao utumia disadvantaged masses ku-push agenda zao kwa personal gain!!!

bush kaona maandamano dume ktk ziara zake na sio hayo maandamano "kigoli" ya watu wenye njaa, wasio hata na agenda ya kueleweka.

nikiwa kama muislamu tena sana, hawa mijitu pumbavu hawaja andamana kwa niaba ya muislamu mimi!!!.
 


Mkuu Bangu,

Naona sasa unarudi mjadala nyuma! wakubwa wanasema kuandamana ni haki yao na malengo ya maandamano pia ni haki yao.

Wao wameamua kupinga ziara ya Bush na wewe andamana kupinga BOT mwingine aandamane kupinga Buzwagi na mwingine kuachwa kwa Karamagi kwenye baraza ndio demokrasia hiyo...
 

Chuma:
You're very wrong.
Kwanza unataka kumziba mdomo Interested Observer asitoe maoni yake kwa kumsimanga.
Two- unaingiza 'u-Us versus Them' hali ukijua kuwa sio waislamu wote walio na msimamo wako uliouonyesha kiwazi katika bandiko lako hapa.

Tafuta zaidi njia za kuwaunganisha waTanzania kuliko kuwagawanyisha katika makundi haya ya kidini.
 

Ok, bwana, hi yo ndo democraz, nimekupata
 
Roses are red..Violets are blue..wouldn't it be nice if you had someone to come home to?
 

Hata Bangu ana haki ya kuwapinga wao kuandamana kumpinga Bush. Yaani hapa manake maandamano rukhsa ili mradi hauchochei wala kusababisha ghasia. Kutoa maoni ambayo si matusi rukhsa. Kila jambo la amani rukhsa.....
 

Unajua mambo mengine lazima tukubali kuwa tunaiga ili tusije onekana kuwa si sio wenzao. Kuandamana na kuchoma Bendera imekuwa ndo fashion. Kwa nini basi wasiandamane bila ya kuchoma bendera. Au wanaogopa kuambiwa kuwa nyie sio wenzetu hatuwapi misaada kwa sababu Bush alikuja hatukuona chochote.
Hivi kabla ya bomu pale Dar kuna mwislam yeyote aliyewahi kuwa deported? Au account yeyote kuwa frozen? Haya yote mliyataka wenyewe mlipokubali kutumika.

Hizi taasisi kama zinaazishwa ili kufandhili na kufacilitate uingizwaji wa mabomu na kuplan kulipua hapa nchini,lazima zifungiwe. Kama pesa zilizokwenye Account ni kwa ajili ya kufadhili watu weknda Pakistani kujifunza namna ya kujilipua au kuingiza mabomu lazima ziwe frozen. Adui siku zote mwombee njaa. Nyie na Bush ni maadui kama unavyosema sasa yeye anahakikisha njaa ya pesa inawapata.

Tatizo pia mnashindwa kuelewa kuwa mnapokuwa pamoja na wapagani na madhehebu mengine wanawaona nyie Waislamu wenzie, lakini mnapokuwa na wao WAARABU WANAWAONA NYIE NI WABANTU MASKINI tu.SIO WAISLAMU WENZETU. Mfano 😀arfur ,Waislam weusi kule hawana thamani,wanakufa na kuteseka.Waislamu wote kimya kwa sababu yanafanywa na Mwislamu mwenzenu!!!Angekuwa bush yuko kule ingekuwa kelele saa hizi.
Unapokuwa na haki haina maana usitumie akili na Busara.
 
Kalam=Interested Observer...Sijamziba mdomo...ndio maana nimempa uhuru awatumie watu wote ktk private msg zao...sasa wewe leo amua kila thread copy n paste ujumbe huohuo...? what does it mean? nimeona nimpe wazo la IT kuwa best way kufikisha ujumbe ampe ADMIN atume to ALL...sio posting kila thread.

Pia mie sijawagawanya wa-TZ, tayari MFUMO umeshawagawanya...Nanyi wakati mnaanza kujadili issue ya maandamano mmekuwa na makengeza ya kutoona Haki za waislam kupinga ujio wa BUSH...ulitaka vipi mwenzetu...?

Nawe unaposema sio waislam wote wenye msimamo wangu, so wewe unawagawa waislam sio...
 
Hata Bangu ana haki ya kuwapinga wao kuandamana kumpinga Bush. Yaani hapa manake maandamano rukhsa ili mradi hauchochei wala kusababisha ghasia. Kutoa maoni ambayo si matusi rukhsa. Kila jambo amani rukhsa.....

Hata mimi nina haki ya kupingana kimawazo na Bangu... kila kitu rukhsa!
 

huku tunakoelekea huu mjadala utaangukia pabaya mie nnaona tuufunge wameandamana kwa mujibu wa haki yao kikatiba na bila ya fujo imeisha imepita
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…