Taarifa: waandamana kupinga ujio waBUSH

huku tunakoelekea huu mjadala utaangukia pabaya mie nnaona tuufunge wameandamana kwa mujibu wa haki yao kikatiba na bila ya fujo imeisha imepita

Ukisema hivyo tutakwambia "unatufunga midomo" iache tu itakufa kifo cha kawaida....
 

kichaka yeye kasema tu anataka kuja tz kuangalia buzwagi yake,na bongozi na ikulu yao wameona bonge la ujiko.
 
Nadhani hawa watu wameacha mambo mengi muhimu yahusuyo nchi yetu ambayo yalifaa zaidi kuandamana kuliko ujio wa Bush. Uchungu wao ingebidi uelekezwe kwenye mambo makubwa ambayo yanaikabili nchi yetu hasa hili suala la Mafisadi. Ingebidi waandamane kuwapinga baadhi ya Majambazi wa CCM ambao wanazidi kuinyonya Tanzania kwa nguvu zao zote.

Ikumbukwe pia walioandamana sio Waislamu peke yao bali pia Jumuiya nyingine za Haki za Binaadamu pale Tanzania nazo ziliandamana kupinga ziara ya Bush kwa hiyo baadhi ya watu msianze kuleta mambo yenu ya kidini hapa.
 

Sawa mtetezi wa Bush...

Muulize Mkapa na Sumaye viongozi gani walikuwa deported? Je kum-deport mtu ni kwa mapenzi au kwa ushahidi kuwa anahusika na Jambo Fulani? Muulize Nyerere aliwa deport masheikh wangapi ktk tanganyika huru? Jumuiya ngapi aliziban?

Una uhakika gani kuwa pesa hizo ni za kwenda pakistan kujifunza kujilipua zaidi ya matashi na chuki zenu binafsi?...kama unakubali Bush ni Adui wa waislam ambae anawaombea DUA waislam wafee NJAA...wewe unafurahio hio? JE waislam hawana Haki kumpinga thru maandamano?

Wewe unachukia nini Bendera ikichomwa?...inakuuma sio...?

Tatizo la Darfur..naona kuna thread maalum imeanzishwa twende kule...lkn kukujibu tu...darfur hizo ni propaganda za WEST(US+EU), wamenyimwa tender ya OIL wameamua ku-create vita...so far Wabongo waliomo humu JF wamekiri ubaguzi wanaopata huko US+EU...kwa rangi zao..najua sio wote(siwezi ku-conclude wanafanya racism huko ulaya na amerika ni wakristo...NO)...pia waarabu kama makundi mengine ya kijamii yanaweza kuwa na tabia hizo...kama ambavyo leo inatokea kenya. So far Uislam sio uarabu...wapo waarabu Wakristo..."
 

Si nilisikia Chadema waliandaa maandamano kupinga ufisadi in the wake of Dr. Slaa's report? Yaliishia wapi? Halafu ujio wa Bush sio jambo la kila siku. Ukipoteza fursa hii ni lini tena utaipata? Ufisadi ulikuwepo, upo, na utakuwepo tu na watu wameshaandamana na watazidi kuandamana kuupinga. Nadhani hapa cha muhimu ni fursa iliyojitokeza na wao wameamua kuichangamkia. Hakuna ubaya wowote hapo.
 

Ni kweli Mazee hakuna ubaya wowote kwa wao kuandamana kwani ni haki yao kabisa ya kikatiba. Hata Bush kila nchi anayokwenda iwe Europe, Asia au hata hapa States kwenyewe watu wanamzomea na kuandamana. Ila nadhani ni muhimu kwa sisi kujiwekea mazingira ya kukemea mambo yanayotokea nchini mwetu kwanza. Unajua Chadema kuandamana kupinga ufisadi ni vizuri lakini Dini fulani ikiandamana kupinga ufisadi huo, habari na ujumbe unaweza kuwafikia watanzania wengi na kutiliwa maanani zaidi. Kwa hiyo hii ni kama changamoto kwa wanadini zote kuandamana kuwapinga mafisadi kwa njia zote.
 

Bush hana cha mkristu ama muislamu yeye anatafuta malighafi kwa nguvu.
Ni bahati mbaya tu mafuta mengi yanapatikana uarabuni ambako ni waislamu wengi ndio inaonekana ana vita na waislamu.Bush hana vita na uislamu yeye vita yake ni kukusanya mali nyingi iwezekanavyo.
Palestina ni kumsingizia tu Bush hiyo vita ni siku nyingi hata kabla Bush hajazaliwa.

Tusiwe wanafiki tuseme ukweli tupu
Hivi tifu likitokea kama lile la zanzibar mbona destination ya hawa wanaopinga marekani hua ni marekani ama uingereza kwanini isiwe Saudia,Ilan ili ukapinge vizuri marekani.

Mnawaona wasomali wanapinga kweli marekani na uingereza lakini wakipata chansi hao uingereza ama marekani hata akienda kwingine lakini macho yake ni huko kwanini isiwe SAUDIa???
 
Sijakuelewa hapa unamaanisha nini.
 
Yani watu wengine humu ndai senior members lakini mnaandika upuuzi, inasikitisha sana. Its clear kuwa Bush anataka resouces, the most impotant of which is energy..aka OIL na at the moment the middle east is wea there is abundance, also Darfur, South America,Iran..Sasa he has to subdue Islam kupata anachotaka that is why waislamu wanamchukia, and by as moderate a definition as could be envisaged, HE is THE ENEMY of ISLAm.thts a fact. Sasa kilam2 anahaki yaku protest na kuchoma bendera ya Nchi ambayo inakiuka haki zao na kuwapersecute. NYIE kina Mkjj inaonekana the concept of Muslim botherhood is beyond u. Refer to Mohamed's Last Sermon.

Eti "Uswahili", comments za namna hii zina demonstrate ethe utmost level of ignorance and dare I say, even foolishness.

Huyo Sheikh mkuu na BAKWATA as a whole sio representatives of Islam, its a mechanism to keep Muslims in CHeck... NO rightly guided muslim anaweza kwenda kula futari kwa the US STATE.. which is represented by its Embassy in TZ. Tena bora ukale nyumbani kwa Bush Crawford Texas kuliko kwenda ubalozini maana nisawa na kwenda White House... wakati waislamu wenzio wanauliwa..

Watu wengine humu JF wanajifanya vinara wa Haki na Kupamana na Ufisadi lakini it is clear from their points of view, ukiwapa uongozi leo, wategeuza nchi kuwa Autocacy.. LET ME TELL U THIS I WUD RATHE SEE UFISADI, THAN LIVE UNDER OPPRESSION.. Waislamu, wakristo, wapagani, wabuddhist,wasankisrist,ma scientologists. Wote wanadeserve kusema wanacho taka.... Nanyie mnaojifanya synics humu ndani kwakuwa mock waislamu mnaonyesha ur deprived logic and power of reasoning... Nawaonea huruma.
 

Nakubaliana nawe kuwa sekta zaidi ya vyama inabidi zitoe shinikizo kwa serikali dhidi ya ufisadi. Na dini ni mojawapo ya sekta muhimu ktk taifa letu na dunia kwa ujumla. I'm glad kwa hili tuko pamoja.
 


Wewe bwana unajulikana na udini wako.

nchi zote hata za Ulaya bush hupata wataki mgumu sana. safari yake ya kwanza UK ilibidi simu zote zizimwe na watu wazuiwe kupita.

watu karibu milioni mbili waliandama hawakuwa waislam ni watu wanaoumia kuona Human Rights haziwi protected hasa na Bushi.

kuna watu wengi wameandika vitabu na thesis kuhusu Illegality ya vita ya Iraq ambayo ni matokeo ya Bush.

kama umesoma International Law hakuna sehemu inayosema nchi moja inaruhusiwa kuivamia nyingine hadi ndani mwake bush kafanya hayo na hakuwa na baraka za umoja wa Mataifa,watu kama Robin cook waziri wa mambo ya nje ya uingereza aliamua kujiuzulu kutokana na unyama wa bush. waziri clear Short nae alijiuzulu.

America ilipoingia Iraq siku ya kwanza walitoa bendera ya Iraq na kuweka yao then wakaitoa ndani ya dakika kumi huo ni udikteta.

Itakuwa ni ajabu na miujiza na bush atashangaa kwenda nchi bila kuzomewa. hiyo inamtosha kuona kuwa Africa bado tuko gizani lakini inashangaza mtu kama mwanakijiji ambaye unaishi Marekani hujui haki ya kuandamana na unamuogopa Bush kama Mbowe.

fuatilia harakati za Senetor Obama na Clinton kwanini Democratic kampeni zao zina nguvu? sikiliza hotuba ya week hii ya hilary Clinton kwenye kampeni zake,msikilize Obama au uko busy kusoma Tanzania Daima tu?

wamarekani wanalalamika miaka yao saba iliyoharibu sifa ya Marekani.

hotuba za John McCain kwenye kampeni zake akiwa anatoka chama cha Bush-Republican lini na wapi alimtaja Bush? anaogopa kuharibu kampeni zake.

wamarekani wanaomba bush aondoke leo wanaona november na january 09 ni mbali.

jiulize kwanini kampeni za sasa watu wanamjadili obama na Clinton kwa nguvu sana? kwanini Obama anachangiwa na wapenzi wake hadi dolla milioni moja kwa siku kwa ajili ya kampeni?

kwanini California Clinton alipata kura nyingi eneo la wageni hasa wahispania?kutokana na sera nzuri za mume wake Bill Clinton.

uko wapi ndugu yetu? hujui hata siasa za marekani? kuna watu walijiua siku bush alipoenda Buckingham palace.

jiulize sana Tony Blair kaachia uongozi kabla ya muda wake baada ya kuona amejiharibia na anazomewa kila siku kwa kushirikiana na BUSH, wananchi wake na chama chake zikamlamizimisha kuondoka.

Mwanakijiji jifunze kwa wenzako kama Mkuu wa Kanisa la Anglikana la Uingereza-Archbishop DR.Roman William ambaye ameona umuhimu wa serikali ya UK kutumia sheria ya kiislam huyu ni mtu mwenye phd ya kikristu sio wewe mwimbaji wa kwaya, pls kuwa open minded.
siku tatu zilizopita ulisema husukumwi na udini ila maslahi ya nchi vipi leo umefanya U-TURN?

kwa maana hii tuelewe kuwa unampiga vita Kikwete kwa vile muislam na kumfagilia Mbowe kwa ukiristu wake?
 
Hayo ni maandamano yaliyoandaliwa na Ponda yule illiterate mwanaharakati wa kiislamu na self appointed defender of Islam. Hana maana hata kidogo. Hivi unategemea nini yeye kaenda shule ambapo anaandika kutoka kulia kwenda kushoto wakati serikali inaandika kutoka kushoto kwenda kulia. Lazima they will clash. Bush anatuletea 700 mill. USD wao kwa upumbavu wao wanataka kutuvurugia hawana akili kabisa. They are throwing stones while they are in glass house.
 

Unajua mtu anaweza kusema maneno mengi bila kusema kitu. Ni wapi nimepinga haki ya wanaoandamana? Usikurupuke kama kawaida yako na mambo ya udini ambao unakusukuma wewe; nimejenga hoja nyepesi na kwa vile hutaki tuhoji yanayofanywa na kikundi cha Waislamu basi wote tugwaye kwa sababu tutaambiwa wadini! too bad! Tutawahoji kama tunavyowahoji wakristu, wapagani, wapinzani, wana CCM n.k hakuna anayeogopwa, kupendwa, kupendelewa au kuonewa!

Angalia tena nilichoulizia na utajua kuwa sijahoji kwanini waandamane au kusema kuwa hawastahili kuandamana!
 
Mwanakijiji unasema hapendelewi mtu na anahojiwa yeyote lini ulihoji kauli ya papa Benedict dhidi ya waislam mwaka jana? kama ulivyotoa kauli juu ya makahama ya Kadhi?

Lini umemuhoji Mbowe kwa mapungufu yake ya kikabila ndani ya chama?au kuweka vimwana wake? hujui athari za ukabila? mwambie atizame Kenya, kama unavyomuhoji Kikwete? mbona unapendelea wazi wazi kwa Mbowe nani hakujui? unapendelea Chadema nje ndani, unampendelea Slaa why not Mwaikyembe?

nimekushauri uwe open minded kama Archbishop Dr. Roman ni vyema ukafanya utafiki kabla ya kupayuka na kubwabwaja. asante mkuu.
 

Kwa hiyo tuseme unamuamlia njia anayotaka kuufikisha ujumbe? Pengine yeye ameona hiyo njia ndio iliyo bora zaidi!

Mimi sijawagawa waislam, bali wewe umeamua kuwasemea waislam wote inavyojionyesha katika bandiko lako hilo. Lisome tena kama unadhani ninakusingizia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…