Taarifa ya tume ya Corona imetoa mapendekezo zaidi kuliko hali halisi ya ugonjwa kwa sasa nchini

Taarifa ya tume ya Corona imetoa mapendekezo zaidi kuliko hali halisi ya ugonjwa kwa sasa nchini

comte

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2011
Posts
9,019
Reaction score
6,825
Nimeikuta mahali kutoka kwa mwananchi wa kawaida kutoka kijijini kwetu, amezungumza haya kama maoni yake binafsi:

"Taarifa ya utafiti wa uviko -19(covid -19) inatoa mapendekezo zaidi na sio hali ya sasa ya corona nchini, na hali ya corona kwa siku zilizopita na athari zake.

Binafsi nashangaa sana Profesa kutoa taarifa dhaifu kiasi hicho kama mtu asiye na utaalamu wa masuala ya utafiti.

01. Taarifa haijaeleza hali ya Corona kwa sasa nchini. Hii ingetusaidia kujua tupo katika hatari kiasi gani. Lakini wao hawakufanya hivyo.

02. Tulitarajia kuona taarifa ikifafanua kwa kina madhara makubwa ya kiafya yaliyotokana na Corona katika taifa letu kwa kushindwa kufuata njia za kitaalamu kwa muda mrefu. Lakini hamkufanya hivyo.

03. Taarifa ingeeleza, namna mlivyofanya utafiti kwa kuchukua baadhi ya waathirika wa Corona waliopona na ambao bado wanaumwa na kuwafanyia utafiti kisha kuja na majibu ya utafiti huo.

04. Na kwakuwa tayari watu walikuwa wanatumia nyungu(kujifukiza). Ninyi mngetoa sababu za utafiti wenu kwanini watu wasitumie nyungu, na madhara ya nyungu hizo kisayansi ili kuwakinga wasiendelee maana huenda hazisaidii. Hakuna utafiti wa kitaalamu unaofanyika duniani bila kuanza na njia ambazo jamii husika ilikuwa ikizitumia. Na hii ni njia bora ya kuwatoa watu katika imani ya nyungu waliyokuwa nayo na kuwapeleka kwenye njia sahihi, bila kufanya hivyo bado hujaisaidia jamii husika.

05. Taarifa ingeeleza namna walivyozifanyia tafiti chanjo zinazosemekana kuzuia corona hata wakati wa taarifa hiyo wangezitolea ufafanuzi. Wanasema kuruhusu chanjo. Je, Wamefanya utafiti gani wa kutushauri tutumie chanjo? Au wamekopi taarifa za watu wengine? Badala ya kuja na majibu chanjo ipi itumike kwa ajili ya watanzania, wao wanakuja na mapendekezo mengine kabisa, inamaana hata chanjo hizo hawajazifanyia utafiti.

Leo ukiwauliza chanjo ipi sasa tutumie? Wanayo majibu hapo? Kitaalamu hakuna chanjo mpaka sasa inayoweza kuzuia corona. Sasa kama maprofesa hao wangekuja na majibu pia athali zitokanazo na chanjo hizo na sio kusema chanjo iruhusiwe pasipo kutoa athali zitakazotokea moja kwa moja au kwa kizazi kijacho. Huo ni udhaifu mkubwa sana wa kamati hiyo. Sasa ni nan atakayetupatia majibu ya chanjo ipi itumike kama kamati yenyewe imeshindwa? Au ndio tusubiri wanasiasa watuchagulie? Au tunafuata kile mataifa mengine na who yatakavyosema?

Basi tu, ila mnaudhi sana mpaka tunashindwa kuelewa tuna viongozi wa namna gani. Hii nchi ni kupokezana tu, leo kwenu kesho kwetu.

Kazaneni sana na maamuzi hayo. Kama makusayo ya mapato kwa mwezi yameshuka, ni vyema mkakazana hata kukusanya kodi kwa nguvu kuliko kujipendekeza kiasi hicho ili tupate pesa za bure kutusogeza mbele.

Mithali 26:28 "Ulimi unenao uongo huwachukia wale uliowajeruhi, na kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu "

Kama kweli chanjo hizo zingekuwa zinafanya kazi, kwann watuzuie kwenda huko kwao kama kweli wana kinga.

Kama kweli una ulinzi, kwanini uogope mwizi?

Wao wazungu wamechanjwa, kwanini waogope waafrika kwenda kwao kama kweli chanjo zinafanya kazi?

Mali zipo Afrika, hata mngejikausha wangewatafuta tu.

Niwatakie majukumu mema lakini

Mithali 27:1 "Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa maana hujui yatakayozaliwa na siku moja"
 
Huyo mwananchi wa kawaida wa kijijini kwenu aliweza kuisoma ile taarifa yote kwenye yale mavitabu au alisoma ile samare tu iliyosomwa kwa waandishi wa habari?
 
Huyo mwananchi wa kawaida wa kijijini kwenu aliweza kuisoma ile taarifa yote kwenye yale mavitabu au alisoma ile samare tu iliyosomwa kwa waandishi wa habari?
sijui bhana yeye kaandika hayo labda kutokana na summary yao
 
sijui bhana yeye kaandika hayo labda kutokana na summary yao
Kama ni kwa kutumia summary ambayo iliandaliwa ili iwe rahisi kwa hadhira yote kuwa na uelewa kiurahisi, basi hata hiyo taarifa kinzani haina maana
 
Kama hiyo ni dhaifu njoo na ile yakwako ya nyungu, tuone uimara wake.
 
Huyo mwananchi wa kawaida wa kijijini kwenu aliweza kuisoma ile taarifa yote kwenye yale mavitabu au alisoma ile samare tu iliyosomwa kwa waandishi wa habari?
Kijijini sasa hivi wako wananchi wa kawaida wengi tu graduates ambao hawajapata ajira kibao unashangaa nini?

Hiyo ripoti haiko kitaalamu imelipua lipua tu kufikia conclussion hewa
 
Kijijini sasa hivi wako wananchi wa kawaida wengi tu graduates ambao hawajapata ajira kibao unashangaa nini?

Hiyo ripoti haiko kitaalamu imelipua lipua tu kufikia conclussion hewa
Kwa hiyo mawazo yametolewa kwa marengo na mtazomo wa asieyekuwa na ajira au ni mawazo huru kwa maslahi ya taifa,nikimnukuu P .
 
Kazi ya tume haikuwa kutoa status ya sasa ya COVID 19 Pandemic, kwenye TOR ilikuwa ije na mapendekezo nn cha kufanya ili kukabiriana na janga hili sawa na mazingira yetu. Na ndio sababu wame come up na mapendekwzo kadhaa. (Rejea press realise yao). Kumbuka awali Tanzania ilikuwa kama kisiwa kisicho na habari juu ya pandemic hiyo licha ya kupiga watu kadhaa.
 
Tumechanjwa chanjo kadhaa tangu utotoni kwanini hii ya sasa ilete mjadala mrefu?.

Mzungu kama anataka kummaliza mtu mweusi anazo njia nyingi tu.

Leo pekee wamekufa watu elfu nne India hapo hujaongelea Brazil na kwingineko.

Sijui ni vitu gani vipo ndani ya hizo sindano lakini naamini wanaotengeneza hizo chanjo na wao wamepoteza ndugu zao kwa maradhi haya.

Tumejawa na dhana nyingi ambazo msingi wake ni uoga na kuishi leo tukiongozwa na fikra za jana.
 
Kijijini sasa hivi wako wananchi wa kawaida wengi tu graduates ambao hawajapata ajira kibao unashangaa nini?

Hiyo ripoti haiko kitaalamu imelipua lipua tu kufikia conclussion hewa
Sijakataa kuwa kuna graduates wengi tu vijijini ila point yangu ni kuwa ameweza kumaliza kuisoma ile report yote kama ilivyo au ame conclude kutokana na ile samare iliyotolewa kwa waandishi wa habari. Hapo tu
 
Muulize mwanakijiji kuwa kamati ingepata wapi hizo takwimu wakati mzee alipiga marufuku na marufuku hiyo haijatenguliwa?
Muulize tena kuwa ,,kamati ingesuggest vipi aina ya vaccine bila kuendesha zoezi la upimaji ambalo pia mzee alizuia isipokuwa kwa watu maalum tu?
Mwambie mwanakijiji kuwa situation ya corona hapa Tanzania bado haijulikani baada ya lile katazo kuwa madaktari wasiseme corona, waseme changamoto ya upumuaji.

Mwambie kuwa wananchi waliachwa tu ili watakaokufa wafe na watakaopona wapone kwani hawawezi kufa wote- au amesahau?
Anataka video ?
 
Kijijini sasa hivi wako wananchi wa kawaida wengi tu graduates ambao hawajapata ajira kibao unashangaa nini?

Hiyo ripoti haiko kitaalamu imelipua lipua tu kufikia conclussion hewa
Mataga bado hamjakaa sawa, mh rais anainyoosha nchi na kuhakikisha anafanya mambo kitaalamu
 
Kazi ya tume haikuwa kutoa status ya sasa ya COVID 19 Pandemic, kwenye TOR ilikuwa ije na mapendekezo nn cha kufanya ili kukabiriana na janga hili sawa na mazingira yetu. Na ndio sababu wame come up na mapendekwzo kadhaa. (Rejea press realise yao). Kumbuka awali Tanzania ilikuwa kama kisiwa kisicho na habari juu ya pandemic hiyo licha ya kupiga watu kadhaa.
Unawezaje kutoa maelekezo mapya bila kuonyesha udhaifu wa maelekezo ya awali? Sisi wananchi tunawezaje kuamini maelekezo ya awali hayakuwa bora kuliko haya yaliyotolewa na kamati ya sasa??
 
Hii report imetumika kama Mhuri kuhalalisha maamuzi yatakayotolewa.
Under remote control kutoka kule
 
Tumechanjwa chanjo kadhaa tangu utotoni kwanini hii ya sasa ilete mjadala mrefu?.

Mzungu kama anataka kummaliza mtu mweusi anazo njia nyingi tu.

Leo pekee wamekufa watu elfu nne India hapo hujaongelea Brazil na kwingineko.

Sijui ni vitu gani vipo ndani ya hizo sindano lakini naamini wanaotengeneza hizo chanjo na wao wamepoteza ndugu zao kwa maradhi haya.

Tumejawa na dhana nyingi ambazo msingi wake ni uoga na kuishi leo tukiongozwa na fikra za jana.
Hakuna chanjo hata moja iliyotengenezwa kwa mwaka mmoja! Ni kuanzia miaka 14 kwenda juu. Waliojitolea kufanyiwa majaribio ya chanjo hufuatiliwa kwa zaidi ya miaka 10 ili kuona madhara ya muda mrefu kama yapo. Hii ya corona haikuwa hivyo ndiyo maana tunaikataa!! Ukweli ni kwamba hii siyo chanjo bali ni majaribio ya chanjo.
 
WEWE UNASEMAJE?SOCIAL ISSUES

Katika mjadala unaoendelea wa kamati iliyoundwa kwa ajili ya kushughulikia suala la Corona wadau wengi wanadai kamati imeonesha udhaifu mkubwa sana. Ripoti yao imeacha mambo muhimu sana na yanayogusa ishu nzima ya korona nchini.

Kamati iliyoundwa ilijumuisha wasomi wakubwa na wanaoaminika lakini bado kazi yake haikuwa ya kuridhisha. Yaani hata ule tu utaratibu wa jinsi utafiti unavyofanyika haukufuatwa.

Baadhi ya mambo ambayo hayakujibiwa na ripoti na yanagusa hisia za wengi na yanayofanya ripoti ionekane haijakamilika ni kama haya hapa chini. Mambo haya kamati haikuyazingatia japo ni mambo nyeti kwa nchi yetu.

[emoji2389]Kamati ilipaswa kueleza hali ya corona nchini kwa siku hizo zilizopita ilikuwaje

[emoji2390]Kamati ingeeleza hali ya corona kwa sasa nchini iko vipi

[emoji2391]Pia ingeeleza athari au madhara ya kiafya ambayo tumeyapata hadi sasa kwa kushindwa kufuata njia za kisayansi kwa muda mrefu.Tumepata madhara au vifo kiasi gani. Hii ingesaidia kujua tupo katika hatari kiasi gani.

[emoji2392]Kamati ingetueleza njia zilizotumika kufanya utafiti. Kama wamekutana na wagonjwa wa corona au waliokwisha ugua wakapona. Au madaktari wanaouguza wagonjwa wa corona n.k.
[emoji2393]Kwa kuwa watu walikuwa wakitumia nyungu basi ilitegemewa wao waje na sababu zao za kwa nini watu wasitumie nyungu bali wapate chanjo. Wangeeleza madhara ya kutumia nyungu na wangesema kama watu waachane nazo maana hazisaidii. Hakuna sababu waliyoieleza ya kwa nini tupatiwe chanjo na siyo kuendelea na nyungu. Huo ni udhaifu wa ripoti
[emoji2394] Katika utafiti wao wangeanza na njia ambazo jamii tayari ilishaanza kuzitumia waoneshe mapungufu yake ili kuwashawishi watu watumie njia mpya sasahivi.

[emoji2395]Wangetueleza jinsi walivyozifanyia utafiti chanjo hizo wanazozipendekeza za corona na zina usalama kiasi gani. Wanasema tutumie chanjo hizo je wamefanya utafiti gani kuhusu hizo chanjo hadi kututhibitishia usalama wake ilihali nchi zingine zinasitisha na kusitasita kuzitumia kutokana na athari hasi.

[emoji2396]Halafu wangebainisha wazi ni chanjo gani tuitumie kama nchi ambayo ni salama zaidi badala ya kupokea maelekezo kutoka WHO ambayo kwa sasa haiaminiki tena maana inanunulika na kutumika kufanikisha ajenda za kishetani. Inamaana kamati hajifanya utafiti wowote lakini wanataka watanzania watumie chanjo hizo?

[emoji2397]Wangeeleza athari zitokanazo na kutumia chanjo hizo ili watu wajue na wafanye uamuzi. Siyo kweli kuwa hazina athari kabisa. Siyo tu kuwaambia watu watumie pasipo kueleza athari zitakazoletwa na chanjo hizo .Suala hapa siyo kupinga uagizaji wa chanjo ila ni namna chanjo hii ilivyoharakishwa upatikanaji wake bila kupata muda wa kutosha kuitafiti Kama ina madhara kwa afya. Huo ni udhaifu mkubwa wa kamati hiyo. Kama kamati haikupendekeza aina ya chanjo ya kuitumia hapo inamaana tusubiri kuchaguliwa na wanasiasa, WHO au tuige kutoka mataifa mengine.

[emoji647]Na kama kweli chanjo hizo zinafanya kazi kwa nini wazungu wanawazuia waafrika kwenda ulaya na marekani? Kwani wao si wamechanjwa? Why waogope? Maana nasikia watu wote hata wototo wanachanjwa huko kwao. Kamati iende ikakae tena au iundwe nyingine, ni maoni. Wasomi wametuangusha sisi WANYONGE[emoji23] Afya ni kitu nyeti sana kuliko misaada ya kifedha toka kwa wazungu

Baadhi ya wabunge wametahadharisha madhara ya kukurupuka linapokuja suala la chanjo. Chanjo si kama dawa zingine za kutibu maradhi. Chanjo ni viumbe hai (virusi vya corona) wanaopandikizwa ndani yako lakini wakiwa wamepunguzwa makali ili wauchochee mwili kujijengea kinga yake. Mwili ukijenga uwezo huo na kupigana na viumbe hao na kuvishinda basi unakuwa umejijengea kinga ya kudumu dhidi ya viumbe wa aina hiyo mbeleni.Mwili hutunza kumbukumbu, endapo utashambuliwa tena siku zijazo utaachilia kinga iliyotumika kupambana na adui wa kwanza na akashindwa endapo wanafanana na wasasa.

Sasa endapo kama chanjo iliyotengenezwa ikawa na athari mbaya kwenye mfumo wa genatics itaathiri vizazi vyote baada ya hapo. Wanaweza kuanza kuzaliwa binadamu wa ajabu ajabu. Siyo kitu cha kuharakisha,au dharula kutokana na unyeti wake. Kinahitaji muda wa kutosha kufanya utafiti.

Nilikuwa najaribu tu kuwaza kwa sauti. Shea ili iwafikie wahusika tupone.
__________________

Shea na marafiki katika magroup mbalimbali.
 
1. Kamati ingeelezaje wakati hamkuwa mnatoa data
2. Hali ya sasa hivi itaijuaje wakati bado hampimi kutoa data...
 
Back
Top Bottom