Taasisi za Serikali zinasaidia kupotosha ufahamu wa watu kuhusu COVID-19. Hata Vyuo vikuu!

Taasisi za Serikali zinasaidia kupotosha ufahamu wa watu kuhusu COVID-19. Hata Vyuo vikuu!

robinson crusoe

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2020
Posts
762
Reaction score
1,236
Kinachotokea nchini ni mchanganyiko ni ukosefu wa maarifa toka kwa wahusika wanaotakiwa kufanya hivyo. Kama alivyosema Mganga mkuu wa serikali, kuna watu wanataka kusikia kinachosemwa na viongozi ndo wachukuwe hatua za kujikinga. Bahati mbaya wanaotakiwa kusema hawasemi ukweli.

Masikitiko makubwa ni pamoja na wenye ufahamu wa juu kabisa; taasisi za utafiti na elimu ya juu. Wapo NIMR, wapo UD, wapo SUA, wapo UDOM, wapo MUHAS, n.k. Hizi ni taasisi zilizostahili kusimamia ukweli na maelekezo ya kitaalamu na kitaaluma. Bahati mbaya nyingine hawa watu wanapotosha watu kwa makusudi.

NIMR wanawauzia watu mchanganyiko wa viuongo vya chakula usiokuwa na taarifa za kitaalamu eti ni kinga ya COVID-19. UD nao wamekuja na hadithi hiyo hiyo ya mafuta ya kichupa cha kujifukiza kilichojaa vitu visivyokuwa na taarifa za kitabibu. Wakati huo wataalamu wa vyombo vya udhibiti serikalini wako kimya, wakishuhudia utapeli wa wataalamu. wenye lengo la kibiashara tu.

Hizi ni taasisi zilizostahili kuja na uvumbuzi wa kuwatia kiburi wanasiasa, badala yake wote wanashiriki utapeli, na kupotosha wananchi kwa lengo la kuuza chupa nyingi, huku watu wakiteketea. Mainjinia wako wapi kututengenezea ventilators? Wafamasia wako wapi kuthibitisha dawa hizi au kuzikataa?

Sasa taasisi za serikali zimejaa umbumbumbu! Hatuoni tofauti ya mpiga ramli tapeli na profesa wa chuo kikuu!
 
Nani kakwambia BONGO tuna mainjinia
Pia kakwambia BONGO tuna
Hao unaowaita mafamasia
 
Baada ya kuwa “tumeiondoa” Korona kwa maombi maalumu ya siku tatu, ilikuwa ni uzuzu kufungulia mipaka yetu 100% na kuruhusu kila “mtalii” akimbilie huku bila hata kumdai cheti alichopima Korona

Yaani sijui Magufuli alidhani Mungu ni wetu peke yetu kuzidi yule wa Vatican?

Ila hatujachelewa sana. Tuanze kuzuia wageni bila kuja na negative certificates. Turudishe karantini za wagonjwa angalau tupunguze cross contaminations. Tuanze kutangaza cases japo tujue wapi ni hotspot areas

Hii kitu isikie tu. Mtaani kwetu jana tumezika mtu wa tatu kwa changamoto ya Korona ndani ya siku 13 tu

EA2201EE-5BC8-4A61-8266-A44B8EF5644B.jpeg
 
Hapa Kila mtu apambane kivyake, maana hakuna tamko, sawa hatu elewi ila hata na picha hatuisomi
 
Hapa Kila mtu apambane kivyake, maana hakuna tamko, sawa hatu elewi ila hata na picha hatuisomi
Wee unazani hata kama anatoa TAMKO
Litakuwa la namna gani?
Fanya kama wee ndo mwandishi wa hiyo spichi/speech.
Niandikie hapa kama unaweza tafadhali.
 
Taasisi zimewezesha wizi wa kura mpaka vijijini, hazina jeuri kwenda tofauti na mwenyekiti
 
Kinachotokea nchini ni mchanganyiko ni ukosefu wa maarifa toka kwa wahusika wanaotakiwa kufanya hivyo. Kama alivyosema Mganga mkuu wa serikali, kuna watu wanataka kusikia kinachosemwa na viongozi ndo wachukuwe hatua za kujikinga. Bahati mbaya wanaotakiwa kusema hawasemi ukweli.

Masikitiko makubwa ni pamoja na wenye ufahamu wa juu kabisa; taasisi za utafiti na elimu ya juu. Wapo NIMR, wapo UD, wapo SUA, wapo UDOM, wapo MUHAS, n.k. Hizi ni taasisi zilizostahili kusimamia ukweli na maelekezo ya kitaalamu na kitaaluma. Bahati mbaya nyingine hawa watu wanapotosha watu kwa makusudi.

NIMR wanawauzia watu mchanganyiko wa viuongo vya chakula usiokuwa na taarifa za kitaalamu eti ni kinga ya COVID-19. UD nao wamekuja na hadithi hiyo hiyo ya mafuta ya kichupa cha kujifukiza kilichojaa vitu visivyokuwa na taarifa za kitabibu. Wakati huo wataalamu wa vyombo vya udhibiti serikalini wako kimya, wakishuhudia utapeli wa wataalamu. wenye lengo la kibiashara tu.

Hizi ni taasisi zilizostahili kuja na uvumbuzi wa kuwatia kiburi wanasiasa, badala yake wote wanashiriki utapeli, na kupotosha wananchi kwa lengo la kuuza chupa nyingi, huku watu wakiteketea. Mainjinia wako wapi kututengenezea ventilators? Wafamasia wako wapi kuthibitisha dawa hizi au kuzikataa?

Sasa taasisi za serikali zimejaa umbumbumbu! Hatuoni tofauti ya mpiga ramli tapeli na profesa wa chuo kikuu!
Ccm wameharibu nchi
 
Cha ajabu hata nchi wanazozingatia maelekezo ya wataalamu bado watu wanakufa na corona. Suluhisho pekee ni CHANJO
 
Eti nani? UD, SUA, MUHAS, bhla! Bhla!.....
Hivi vyuo vimeshakuwa kama shule fulani ya sekondari inayomilikiwa na dhehebu la kidini. Nidhamu inawekwa mbele kuliko taaluma. Kuna viongozi wamepewa kwa kuwa tu ni wanyenyekevu kwa wanasiasa, halafu ni wakali kwa watumishi wenzao! Weeee! Muulize yule profesa Mkandara alivyokuwa analinda aendelee kuwa VC bila kujali udumavu wa wana taaluma wa UD.

Hakuna kitu hapo! Kuleni uchafu wao munaita eti ni dawa ya COVID-19.
 
Kinachotokea nchini ni mchanganyiko ni ukosefu wa maarifa toka kwa wahusika wanaotakiwa kufanya hivyo. Kama alivyosema Mganga mkuu wa serikali, kuna watu wanataka kusikia kinachosemwa na viongozi ndo wachukuwe hatua za kujikinga. Bahati mbaya wanaotakiwa kusema hawasemi ukweli.

Masikitiko makubwa ni pamoja na wenye ufahamu wa juu kabisa; taasisi za utafiti na elimu ya juu. Wapo NIMR, wapo UD, wapo SUA, wapo UDOM, wapo MUHAS, n.k. Hizi ni taasisi zilizostahili kusimamia ukweli na maelekezo ya kitaalamu na kitaaluma. Bahati mbaya nyingine hawa watu wanapotosha watu kwa makusudi.

NIMR wanawauzia watu mchanganyiko wa viuongo vya chakula usiokuwa na taarifa za kitaalamu eti ni kinga ya COVID-19. UD nao wamekuja na hadithi hiyo hiyo ya mafuta ya kichupa cha kujifukiza kilichojaa vitu visivyokuwa na taarifa za kitabibu. Wakati huo wataalamu wa vyombo vya udhibiti serikalini wako kimya, wakishuhudia utapeli wa wataalamu. wenye lengo la kibiashara tu.

Hizi ni taasisi zilizostahili kuja na uvumbuzi wa kuwatia kiburi wanasiasa, badala yake wote wanashiriki utapeli, na kupotosha wananchi kwa lengo la kuuza chupa nyingi, huku watu wakiteketea. Mainjinia wako wapi kututengenezea ventilators? Wafamasia wako wapi kuthibitisha dawa hizi au kuzikataa?

Sasa taasisi za serikali zimejaa umbumbumbu! Hatuoni tofauti ya mpiga ramli tapeli na profesa wa chuo kikuu!
Taasisi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu inaishia kukorogea watu viungo vya chakula ili kutibu corona. Upuuzi kabisa!
Hizi ndo facts tunazostahili kujadili hapa JF. Tatizo wengi tunaandika baadaye tunakimbilia kunywa viungo vya pilau eti ndo dawa ya Corona. Vyuo vikuu vyetu hovyo kabisa!
 
Back
Top Bottom