Taazia: Hamza Rijal mchezaji wa zamani wa malindi anamkumbuka Mohamed Msomali

Taazia: Hamza Rijal mchezaji wa zamani wa malindi anamkumbuka Mohamed Msomali

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
TAAZIA: HAMZA RIJAL MCHEZAJI WA ZAMANI WA MALINDI ANAMKUMBUKA MOHAMED MSOMALI

2016%2B-%2B1

Mohamed Msomali
(Picha kwa hisani ya Vijana Wapenda Soka wa Kariakoo)

ASALAAM ALAYKUM!
In Lilahi wa Ina Ilahi Rajiuna.

Mohamed Msomali Katutoka
na Hamzah Rijal

Katika mchezaji ambaye namkumbuka kwetu huku Afrika Mashariki mwenye _Quality_ ya Boby Moore wa England na Frantz Backenbeur ni Mohammed Msomali na Kadir Farah.

Msomali akiweza kuzuwia mpira kwenye Box akaanza safari taratibu, mwili wake ulikuwa mwembamba lakini akiweza kucheza rafu usiweza kuamini.

Marehemu Kilambo alikuwa na nguvu na akitisha yeye na Kapera, mara mmoja Yanga na Cosmopolitan, Kilambo kishachafua sawasawa kina Jamil, Aden, Marando, Iddi Balozi ikawa wapo taabani, Msomali akampa fundisho Marehemu Kilambo alichukua mpira kisha akafanya umemponyoka, Kilambo hakujuwa kama ametegewa kwenda kupaua aliekewa kile tunaitwa Kisiki, Kilambo alikuwa mzima akarudi kiwanjani lakini alijua kakutana na mwamba mwenzake.

Bahati mbaya sana Tanzania kuwa na watu kama Msomali, Emil Kondo, Sharifu, Hemed Seif, Khalid Abeid kwa nyakati zile ambao kwa leo wangesaidia sana pale midfield ambayo haina ubunifu.

Msomali akiweza kucheza namba 4 au 6 na mara nyengine akicheza 5. Kwenye Taifa kabla ya Combination ya Omar Zimbwe na Goboss ilikuwa unastaladha pair ya Zimbwe na Msomali.

Mwaka wa 1999 nilikutana na Marehemu Msomali pale Morogoro nikiwa kuna Mkahawa karibu na Stand ya Mabasi, Msomali alikuwepo hapo kenda kula hali yake wakati huo, sikuamini nilipomuona Star ambaye kama nilivyokwisha kutaja alikuwa anaitumikia Taifa na Cosmopolitan haikunifurahisha sana.

Msomali kama Allan Ball kwa umbo lakini akichezesha wenzake na mara nyengine unaweza ukamzungumza kama Johan Cruyff pale anapozuia mpira kisha akatoa pasi akakuambia umrejeshee palepale ambao kazongwa na wapinzani, wakati wake ni yeye na Kadir Farah wa Kenya ndio peke yao wakifanya hivyo, ila Kadir Farah alikuwa na speed, Msomali hakuwa na hio speed.

Cosmopolitan imeondokewa na Taifa Star nayo imeondokewa, Allah amjaalie Janahnatul Firdaws, Ameen.


tS8q9uHbt-5_Y4Z_FM00W8_gJTjMX2xgVcwu0fZuXWu5FQIzwxo78n6ARH45YyXMeKHcJaGel-2DAwCsmtZn-O34-F0iwjhFW84ToBZlPGUq57M2UiFVKhcVOAM_mPhQtRIGU8Tc7eyHvbK9sS-9NZ3iPoAAwNPngoM3gQqU5isi51EH5WbHZOcwm4DReY713BQ7CqijMGS6CGv17BedvvRYmqGyY19Xq6M3fUbvdkWN5C3P7FP-rJz-azge5sZP4ziiza7etXz-rXfxBEybcDNaFKzA-CkX4psT--wFu-vClDSpie5wg09a5x3-G1dlic-E3EUYO2Jrn2_koMkDksuq2SOYNttWO4McOlZ990rD4t15Q2AJQi5eeNR9OmEnTX4Jr89zIAGieODlCGxl46QaxF-JNwjUkR0J4HKiSxayQ1G9W7ztO7PVHK2abEqT19oelMiBXDrNF6uEMASmXd5NxpcwES2EPcR2Coq-x2a666n-vY9Z9j9eRgVx__ZjnQd6NyB42TSGay9BsjXsmpbq22V2jwBSM-uT-rPgSwiVK_XlQQeoOwWKavjIOE7jgt5j8Q_0x6Sjmg86S7kYfXz2MjXpTZ9psodS2OskTiqpSiki8A=w876-h657-no

Kushoto wa kwanza ni Mohamed Msomali akicheza timu ya Kombaini ya East African
Cargo Handling Services katika miaka ya1960/70


Rafiki na ndugu yangu Hamza Rijal ni mchezaji wa zamani wa Malindi Football Club Zanzibar.

Kaniandikia binafsi mistari michache kunieleza habari za Mohamed Msomali lakini nimeona niweke hapa kwa faida ya wasomaji na wapenda soka kwa ujumla.

Kwanza nimecheka nilipokuwa namsoma Hamzah khasa pale alipoeleza staili ya uchezaji wa Msomali katika kupunguza nguvu za wapinzani wake.

Nimecheka kwa saabu yeye Hamza akicheza nyuma na alikuwa ‘’no nonsense player.’’
Alikuwa kama Msomali bingwa wa kuwaadhibu, ‘’strikers.’’

Sasa ungekuwa unamjua Hamza nje ya uwanja kwa ule upole na ustaarabu wake kisha ukamuona uwanjani anavyowaparamia, ‘’strikers,’’ ungejiuliza inakuwaje huyu mtu akawa hivi?

Njiwa nje ya uwanja na tai ndani ya uwanja?

Sijashangaa hata kidogo kwa ''tasnifu,'' hii yake ya Mohamed Msomali kwani Waingereza wana msemo wao, ‘’Birds of a feather fly together.’’

Hamzah Rijal amepata elimu yake ya juu Libya na Scotland. Baba yake marehemu Zubeir Rijal alisoma Chuo Kikuu Cha Oxford katika miaka ya 1940.


HHR6GirmuWGH7m-Y6JP_BSouEEUjZHjxSFqDUBp8MVVy5B1p2z6Ov6KBdpMzXM-mjsBNkvfRMZSNVwokdzZrbQtwpEstpx5Xlut7hdRU-EYuW2siCUz9O5Iy08BHnBy-xNbXQlrnpdd8AQQghED-ToHCqberrP3utTBWtw_Gr-Ynn18_q1dOPhMeBMYCRWVMrupY7xioapn72yS-iWOArVR2DQz9uGMdMU8iisMwbMw9cKM3zOBKxClvLjKhFy49uYrNt0PRxx7vXv0xiYVkAxb7tzrUm6dB5Q1AooNDEFPfhFhFLLwwwGFYkbY2YzS0nuiFXHgM--eVFVHklT3Tgz9BoXhJp7XtBLPL1aUCEivq3YpIt3tWPxUt8OdEyHXH8f8aCZD88-XmlbzYZaTX_NM34pfwxROG8r6STAp5SyWYTniW9BMACXfpWCkqz8yITkmR6FRHVxJbyFEPDNzlyzbzrbCnPl3Eq24yw2bjdzvjy4NoliijT_TCv_i_rnVu-3kw73EP3TQ8QPDqLOgs3UE2Wu0xT8uYU3ausl7yvkZnxAzhn3qyWtywKZRkCr3o8aTTQ226zyysOzUvjjjN61SUp7UvGvqatbjeai2g4NxlV83oYA=w409-h657-no

Hamzah Rijal
 
Nimependa Lugha ya Kiswahili ilivyotumiwa kiusanifu kwenye kujenga picha ya Umahiri wa Mohamed Msomali kwa kulinganisha na wachezaji wengine wa Ulaya na wa eneo hili la Afrika ya Mashariki. Asante sana Hamza Rijali kwa kutumia Lugha hii yetu adhimu kwa ufasaha!!
 
Nimependa Lugha ya Kiswahili ilivyotumiwa kiusanifu kwenye kujenga picha ya Umahiri wa Mohamed Msomali kwa kulinganisha na wachezaji wengine wa Ulaya na wa eneo hili la Afrika ya Mashariki. Asante sana Hamza Rijali kwa kutumia Lugha hii yetu adhimu kwa ufasaha!!
Allen,
Hamzah Rijal
ni Mzanzibari.
Anasema Kiarabu ''fluently,'' pia ni sheikh:

2016%2B-%2B1


eI6XW9pR0DzIu-7KJtvimdf3pzKNpf3_07JFGOtgp6aLhL1xtE9lBJLDaiLuwxzhmh929JUyefy1SntP_D4ZWfuNf9TK9cJBJEA5jSFKe4oWlOqRh-Mr7NXur_k1mNfL1cPTHY3HuOENMnFISGy1dkzRzntOE8vzxAmrA0iqvKk5y9SUfmQD5jehKgPv9hn8EubBkUjQG_KEPS67hqSQgVnTk3xqWOpbSlweEIRypwvVjV5LVxg568em5601mS5sQmSKW51u8SM-08e1313N-aqq5fwD31_qyKWz-soogl-UtcmvmMYlD3_1knSKrNgME1NJmkVQjA2BYcDJ0NDHO5DpBlgoJM-vuJ53ZDU-0X1hewYhhaJ4I_3Um0yGw3daLgWFpR8s5KQK28BZUg-HuafyxCVFsfEHxU_xCcEPtz84SM4wfXEMaQV53qt2Z-8gPCLC2kMV3bRos_FlyI2nk3RcUNvcr8-RR-v0wz6sKbO-Wens3p5pXqQvA8BlmdAOt_Q5IdXNNoeGuRCbbc3Bw1ki7r47woFBO624FOR2ISa4YRWnFxNf-gdi6Yszn2MCQDqVoRJYBA-KU734KZFZ7C7OBF5noAKTh-E-Li_4WtI0jjxvRA=w692-h657-no


Hamza Rijal akifanya kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani katika Zanzibar Cable.
 
Hamzah Rijal ni Mzanzibari.
Anasema Kiarabu ''fluently,'' pia ni sheikh:
Na ni mbobezi wa sayansi ya mazingira na huiwakilisha Tanzania katika mikutano ya Conference of the Parties(COP)ya UN Climate change. Ni mtoto wa Mwalimu wangu,Lumumba College,Maalim Zubeir Rijal(rehma za mungu zimfikie)
 
Hakika nyakati "ngumu" hudumu,Lakini watu "wagumu" hawadumu.Upumzike kwa Amani Msomali.
Nilimsoma sana kwenye Maktaba ya Mzee wangu ktk kitabu maarufu cha "Ijue Simba na Yanga".Simkumbuki mwandishi wa kitabu,lkn kimeandikwa miaka ya 1970.

Humo imezungumziwa Cosmopolitan na hawa kina Msomali.Kina Manara na Kibadeni wakiwa ktk picha ya pamoja na bugaloo na platform laizoni.Huku ukurasa mmoja mzima ukimuelezea mtu mmoja anaitwa Mangara Tabu Mangara(Mzee Mohamed Said unajua habari za huyu mtu?)

Nimependa Kiswahili kilichotumika...Hilo neno "Staladha" humaanisha nini?
 
Asante kwa kumbukumbu nzuri Sheik Mohamed Said
 
Kumbukumbu nzuri..hivi serikali yetu ilikuwa haioni umuhimu wa kuwatumia hawa wazee wetu kuinua sekta ya michezo hadi waishie kuwakumbuka na kutoa sifa kedekede pale wanapofariki
 
Inna lillahi Wa Inna ilaihi raajiuun, wakati mwingine natamani ningeishi dunia yao, Dah zama zimepita sana!
 
Back
Top Bottom