Tabia hii ya kulamba vidole kwa mate na kuufungua mfuko wa plastiki inakera

CDG

JF-Expert Member
Joined
May 31, 2015
Posts
200
Reaction score
97
Nimefuatilia sana wafanyabiashara wadogo wadogo (Magenge ya Matunda, unga, n.k.) wengi wao hulamba vidole kwa Mate yao na kuufungua mfuko wa plastiki.

Inatia kinyaa na kusababishiana maambukizi ya Magonjwa kama Kifua kikuu (T.B.), Kikohozi n.k.

Binafsi huwa namweleza hapo hapo, siyo wote tunaweza kufanya manunuzi Supermarket (Shopping Mall) lakini kwa maudhi haya itakubidi tu.

Je, wewe unafanyaje kuwaelimisha Wajasiriamali hawa?
 
mimi inanikera wakati wa kusafiri seheme za kula unakuta mtu anakata nyama huku anapokea hela na mikono hiyo hiyo au wauza chapti huwa wananikera sana


Nb:hamna kitu kichafu kama hela kina shikwa na kila mtu na wakati wowote
 
Reactions: CDG
Msiwe mnawaangalia. Wageuzie mgongo.... ili upunguze stress
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…